jaman wapendwa nataka kulima mpunga huko kahama,,lakn sijui nianzeje kwa gharama kias gan,sjui muda wa kupanda na kuvuna,lbei ya mbegu kwa heka moja.naomba msaada
Jaribu Kufanya Utafiti Kwanza Usije Ukaangukia Pua ... Jiridhishe Kwanza Ni Maeneo Gani Yenye Maji Ya Uhakika ... Ulizia Wenyeji Kwanza Ni Maeneo Gani Yanayotoa Mavuno Mazuri ... Tafuta Mkulima Mzoefu Wa Huko Kahama Muombe Akufafanulie Gharama Za Kukodi Shamba Kwa Hekari Moja ... Gharama Za Kuvuruga Shamba La Hekari Moja Kwa Awamu Mbili ... Gharama Ya Kupandiwa Mpunga Kwa Hekari Moja ... Gharama Ya Kupalilia Mpunga Kwa Hekari Moja ... Gharama Ya Kuweka Mtu Wa Kuwania Ndege Kwa Hekari Moja ... Gharama Ya Kuwalipa Wakataji Wa Mpunga Kwa Hekari Moja... Gharama Ya Kuwalipa Wakusanyaji Wa Mpunga Kuupeleka Mahali Pakupigia Kwa Hekari Moja ... Gharama Ya Kuwalipa Wapigaji Wa Mpunga Kwa Hekari Moja ... Gharama Za Kusafirisha Magunia Ya Mpunga Kuyapeleka Kwenye Stoo ... Mkuu Acha Niishie Hapo Kwa Leo Ole Wako Uende Kichwa Kichwa Utakula Za Uso Na Utabakia Kusema Kilimo Cha Mpunga Ni Kigumu Na Hakina Faida ... !