Ikiwa ni mwendelezo wa kile ulichokifanya Canada na maeneo mengine ambayo labda hayakuripotiwa au ilifichwa katika mikataba ambayo imekuwa ikisaini katika nyakati tofauti. Kuna Matukio mengi yamekuwa yakiripotiwa kwa Raia wa kitanzania kufanyiwa matukio ya either kuzuriwa au mali zao kudhuriwa.Nafikiri ingekuwa busara tukio ulilolifanya Canada basi liwe replicated na Tanzania pia.Isiwe wao tu ndiyo wana umuhimu kuliko rai wako hata wao wanahaki ya msingi.
Hivi yale yaliyotokea Nyamongo na madhara yake yamezungumziwa kwenye huo mkataba uliosaini?makubaliano gani yanawalinda wakazi ya maeneo ambayo hawa mabwana wanafanya shughuli zao? Wamekuwahi ili nasisi tufikie huku.
Wakati mwingine tunashawishika kuuliza maswali ambayo yanakera au kuwakwaza watu wengine ila we have too!
Mimi naunga mkono hii na niliweka thread hapa kwamba tuweke kabrasha hapa la kila mwenye ushahidi wa corruption ya viongozi na wengine wanaokula nao ili haya yaje yakabidhiwe DPP. Nashangaa moderator na wakuu wa fforum waliing'oa nusu saa baada ya kuiweka!
Bila ya kuwaadhibu vikali hawa hapo baadaye hatutaondokana na jinamizi hili. Kila aliyeiba, aliyesababisha mauaji, aliyedhulumu......hakuna msamaha.