Kikombe cha chai

decomm

JF-Expert Member
Dec 10, 2013
726
657
MBEYA VIJIJINI

Mwalimu 'mwenyeji' wa darasa la kwanza ameandika ubaoni:-

"Kikombe cha chai"

Mwalimu anawaambia wanafunzi:-

Mwalimu: 'wanafunzi somemi ubaoni'
Wanafunzi: 'Ikikombe kya kyai'

Mwl: 'Hapana siyo ikikombe kya kyai, semeni ikikombe kya kyai'

Mwl: 'Haya someni wote'
Wanafunzi: ' Ikikombe kya kyai'

Bahati nzuri kukawa na mwanafunzi mgeni aliyetoka mkoa mwingine. Akanyoosha kidole.

Mwl: 'Enhe wewe mwanfunzi mgeni unasemaje?'
Mwanafunzi: 'Samahani mwalimu, inatamkwa KIKOMBE CHA CHAI'

Mwl: 'Sawa kabisa, mmemsikia mwenzenu amesoma vizuri?'
Wanafunzi: 'Ndiyoooo'
Mwl: 'Enhe, someni wote'
Wanafunzi: 'Ikikombe kya kyai'
Mwl: 'Aaaargh! Siyo IKIKOMBE KYA KYAI, semeni ikikombe kya kyai!
Wanafunzi: 'Ikikombe kya kyai'
_____

Ulimi ukielemewa na lahaja, kutamka maneno ya lugha nyingine mara nyingi inakuwa si rahisi kutamka sawasawa.

decomm!
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…