Pia chadema msisahau kutoa shukrani kwa mganga wenu ramli yake aliyawapigia imewasaidia sana
Pia chadema msisahau kutoa shukrani kwa mganga wenu ramli yake aliyawapigia imewasaidia sana
hizi ni hasira za kushindwa anguko la ccm limeshakaribiaPia chadema msisahau kutoa shukrani kwa mganga wenu ramli yake aliyawapigia imewasaidia sana
Mkazo mkubwa uwekwe vijijini. Kila jimbo lihakiki matawi na misingi yake na ihakikishwe kuwa kila mahali penye shina au nyumba 10 za CCM nao chadema wanao msingi na uongozi pale. Kila kanda ijitathmini kutumia matokeo ya uchaguzi huu!Naongezea mpaka sasa hivi nguvu ya ccm iko vijijini naomba kwa nguvu kubwa ihamie vjijini ili watu waelimishwe wajitambue maana wameshatishwa sana kuwa wakichagua upinzani kutakuwa na vita hivyo tukiweza kuwatoa hiyo hofu ukombozi U miknoni mwetu iwe kazi rahisi 2015 tukiweza huko ni kazi rahisi itakayobaki ni kumsukuma mlevi,naomba sana hii iwe kazi muhimu naamini tutashinda bila shida.
Ninaomba kutoka kwa mtu anayeaminika anipe mawasiliano ya simu ya Mbowe. Niliomba kwa tumaini Makene lakini sikupata jibu hadi sasa ila ninaamini ni kwa sababu amekuwa busy.
Ninajambo la muhimu la kuwashauri lakini siwezi kuliweka hapa mtandaoni kwa hofu ya panya wezi ccm. Wananusa, wanakwiba, halafu kutumia hawajui wanaishia kuboronga na hivyo kuharibu mipango na malengo mazuri.
Ccm wamekuwa wakiiba mikakati ya wapinzani na kuishia kuiharibu ajili si viwango vyao. Sasa nina masuala makubwa ya kuwashauri UKAWA lakini siyo hadharani na ukoo wa panya wakisikia. Ninaimani mwenye nazo ila anayeaminika, atanipm. Wateka nyara wa mawasiliano samahani sana kaeni mbali na hili haliwahusu.
Ngumu lakini, kumpenda mtu kama mtemi Andrea Chenge?!Kuongeza, Ni wakti wa KUWAPENDA ahta MAADUI ZENU hasa CCM, maaana kw akufanya hivyo ndio mtaweza kuwamaliza na kuwafuta kabisa.
ni kweli mkuu, lakini pia cdm na ukawa kiujumla wajitaidi kuwajengea uwezo viongozi wote waliochaguliwa kupitia ukawa, ili waweze kuwatumikia wananchi wote kwa usawa bila kujali itikadi zao.Kubwa zaidi katika hizo semina elekezi mtoe maonyo makubwa sana kwa hao viongozi kujiepusha na rushwa ili wananchi waone tofauti yao na wale wa CCM. Wajue wazi kuwa sehemu nyingine sio kuwa Chadema imeshinda kwa kupendwa sana maana wapo walioichagua bado hawaijui vizuri bali rushwa ya wale viongozi wa CCM ilikuwa kero kwao.
Wafamisheni kuwa chama kinayo mamlaka ya kuwafukuza uanachama viongozi watakaobainika kuwa wala rushwa hivyo heshima mbele ya wananchi itakomaa.
exactly, cdm wanapaswa kuufanyia kazi ushauri huu.1. Kwa kuongezea muwe karibu na viongozi waliochaguliwa kuwaelimisha zaidi juu ya sera za chama utekelezaji na matumizi ya rasilimali watu fedha kidogo ya eneo iliyopo itumike kwa uadilifu mkubwa ili kujenga ngome imara ya ukawa eneo husika
2: kuwashirikisha wananchi wote bila kujali itikadi zao katika kujiletea maendeleo yao kwa kuwashirikisha kila jambo lolote linalowahusu waliamue wao kwa ajili ya utekelezaji. Ukweli ni kuwa kuna mahali wana ukawa ndio wameingia kwa mara ya kwanza na kama zari wakashinda. Hapo kwa vyovyote vile mgombea wa ukawa atakuwa hajaelewa sera na itikadi za chama kimojawapo cha ukawa kwani huenda wananchi walichagua kwa hasira so magamba yanaweza kutumia mwanya huo kuondosha hasira au kumnunua na kiongozi yule na hatimae kupoteza nafasi hiyo muhimu. Hapa natoa angalizo kwa cdm mwanga kwani alieshinda kijiji cha kighare usangi anazo tabia za kubadilika badilika kwa kifup ana price tag
3. Kujenga upendo na kuhudumu kwa uadilifu mkubwa, kumbukeni maeneo yote wanaukawa walishika yatapata vikwazo vikali vya kichumi kutoka chama dola na dola yenyewe ili kuwakomoa wananchi hao so rasilimali kidogo iliyokuwepo itumike vizuri kwani hili lipo kwenye ilani ya uchaguzi ya chadema2010 ilikuwa na jukumu la kupunguzo michango na gharama za maisha
haa haa amewasaidia kufanyaje kamanda?Pia chadema msisahau kutoa shukrani kwa mganga wenu ramli yake aliyawapigia imewasaidia sana
Mganga wa ccm Sheikh Yahya alishafariki ndiyo maana ccm inafanya vibayaPia chadema msisahau kutoa shukrani kwa mganga wenu ramli yake aliyawapigia imewasaidia sana