JK for Mtwara


jidanganye tu.
 
Nilisikia Rais wa China anakuja huku kwetu. Usikute ni kupalilia njia ikiwa ni maandalizi ya mkubwa huyo. Mjue China ilishahakikishiwa (sijui walisaini mkataba) kuwa permanent investors kwenye ukanda wote wa Tanzania Kusini.
 
Nyie mnaoongea nyote mpo dar wala hajui kinachoendelea Mtwara, mwache aje ajionee mwenyewe kama ulikuwa upepo unaopita au la. Ukweli ni kwamba watu wanalishughulikia hili kwa hoja. Hivi nyie mnajua gesi asilia ni nini? na kwa nini watu wa Mtwara tuonaoijua tunasema gesi asilia ya Mtwara itakuja dar kama bidhaa na si vinginevyo. Tega sikio na ufumbuwe macho nitakujuza hivi karibuni hapahapa jamvini.
 
Rais Jakaya Kikwete amekuwa punching bag hata kwa wajinga na wapumbavu nchini. ONLY wajinga na wapumbavu ndiyo wanaweza kulalamika na kuhoji sababu ya Rais wa nchi kwenda kutembelea eneo na wananchi wake nchini. ONLY IN TANZANIA.

Kitu cha ajabu unakuta hata watu wengine wanachokilalamikia hawakifahamu. Kuna watu nafikiri wanaweza kuugua kama itapita siku bila kuwa critical kwa kila Rais Kikwete anachokifanya.

Kwa kuchelewa kupata Freedom of expression and opinion nchini, kuna watu wanakuwa kama wamebarehe ukubwani. Wanarukia kila kitu ili mladi tu waonekane wametia neno wakati ni upuuzi tupu.
 
atakua ameambiwa na mshenga wake mh.mkuchika kwmba aje tu mambo yapo shwari ss ngoja tuone nn atakuja nacho
 
mbowe ndie anashinda ofisini
Madhara ya kutumia masaburi!!
Haina ubishi,ndugu uwezo wako wa kufikiri urefu wake ni kutoka kwenye macho yako mpaka kwenye tip ya lipua lako!!
Muda mwingine si lazima kutudhihirishia jinsi gani ulivyo mburulula,unatuchosha!!
 
hivi huyu jamaa anatuliaga ofisini kweli?

katika hizi zama za teknolojia mpya za mawasiliano , Cell phones, Internet, Fax, Skype, nk huna haja ya kukaa ofisini kwako ulipozoea ili ufanye kazi. Unaweza kuwa popote ukapiga kazi. Unless uwe unahitaji ku sign makaratasi ambayo hjata hivyo unaweza ku sign popote ulipo yakatumwa kwa courier. hebu tuachane na mitazamo ya mwaka 47 ya kukaa ofisini. Angekaa ofisini mngelalamika tena kwamba rais haenda ground kuona kwa macho.
 

wasiwasi wangu anaenda kupiga dili za gesi sababu sio kawaida kwenda sehemu zilizo nyuma kimaendeleo,zake fastjet ni arusha na ulayaulaya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…