Je unaweza kutumia PHP kudevelop android apps?

hero7

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2014
Posts
220
Reaction score
70
Habari, ningependa kuuliza /kujua
Je PHP unaweza kuitumia kudevelop android app without any other language?
 
Yes, Zinaitwa Hybrid App, unatumia Web technology, Mfano Facebook ilikuwa Hybrid kwenye Android Kabla ya Kuwa Native App
 
Hapana, hybrid Apps zenyewe zinatumia HTML, CSS na Javascript.
Officially lugha ya Android ni Java na C kama unahitaji baadhi ya function ziwe na spidi zaidi.

PHP unaweza kuitumia kutengeneza backend ya mobile app yako, yaani ile server inayoongea na App kuipa data.
 
ex:nahjat tengeneza app ya android ambayo itakuwa inafanya kazi record za wanafunzi na kuzihofadhi pamoja nasura like regestration app ila nahtaj itambue binadamu na mnyama.
 
Ilikuwa lazima na mimi niache comment yangu pamoja na kwamba hapo juu wameelezea vizuri sana.

Kwa ninavyofahamu mimi ni kwamba haiwezekani kabisa kutumia PHP kwa ajili ya kufanya chochote zaidi ya serverside scripting, inamaanisha kama mpango wako ni kufanyia kazi php kwenye sehemu nyingine zaidi ya server yako, basi hilo litakuwa tatizo.

Kwa nia ya kujenga application ni lazima uelewe Java kama unataka utengeneze application za simu zenye standard nzuri lakini pia unaweza ukatumia HTML CSS NA JavaScript kujenga website yako lakini kama nilivyosema hapo mwanzo, standard tofauti.

Lakini Kusema kwamba PHP haikusaidii kabisa kipindi unajenga application ni uwongo kwa sababu hata google wanatoa huduma yao ya Google Cloud Messaging(soma hapa A Simple Chat Application in Android Using GCM and Server Side – PHP. | CoderzHeaven) inayotumia PHP kuwaruhusu watu kutumia cloud yao kama uwanja wa chat applications.

Kwa hiyo kukujibu swali lako kama unaweza kutumia PHP kutengeneza application yako, mimi nasema HAPANA!, PHP peke yake haitoshi kujenga application yako.

HABARI NZURI

Kuna software kama PhoneGap zinazokuruhusu kutengeneza app walau uwe unabadilisha project ya HTML na PHP(webisite yako) kuwa mobile app, ni open source(bure)(ahsante Adobe) na rahisi sana kuitumia
 
Kwa ufupi PHP ni server scripting language. Kilichopo content iliyo na PHP inaExecute kwenye server tu! Isipokuwa kinachoonekana kwenye Device/Browser ni HTML/JSCRIPT/CSS
 
Ula pia kama tayari wajua C# kuna Xamarin ambayo inakusaidia kutengeneza Cross-platform applications i.e Android,iOS,Mac OS,Windows phone apps
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…