Ipo siku nitawaambia wanangu

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
361,270
Reaction score
832,274
Siku moja, wanangu watakapokuwa na umri wa kutosha kufahamu kile kinachomsukuma mzazi, nitawaambia....

Niliwapenda kiasi cha kuwasumbua kuhusu mlikokuwa mmeenda, watu mliokuwa nao na saa ngapi mngerudi nyumbani. Niliwapenda vya kutosha kiasi cha kuwa na wasiwasi juu ya afya yenu. Niliwapenda vya kutosha kuchagua kutumia muda wangu kwenu, kwa matumaini kwamba masomo yataleta furaha ya kutimiza ndoto zenu za muda mrefu. Niliwapenda kiasi cha kuwalinda kupita kiasi. Niliwapenda kiasi cha kutotoa visingizio kwa tabia yenu mbaya na ukosefu wa heshima.

Niliwapenda vya kutosha kuchagua kujiweka wa mwisho, kila siku. Niliwapenda vya kutosha kupuuza kile 'kila mzazi mwingine' angefanya. Niliwapenda kiasi cha kuwaondoa watu niliowapenda maishani mwangu ili niweze kuwalinda ninyi

Niliwapenda kiasi cha kuwaruhusu kujikwaa, kushindwa na kuanguka, ili mjifunze kusimama peke yenu. Lakini zaidi ya yote, niliwapenda kiasi cha kukuhatarisha kunichukia kwa maamuzi niliyoyafanya nikitumaini kwamba nilikuwa nafanya kilicho bora kwenu, na hiyo ndiyo ilikuwa sehemu ngumu kuliko zote.
Niliwapenda kwa moyo wangu Wote, kwa nguvu zangu zote kwa kila jema na kwa kila kitu.. Zaidi ya yote niliwapenda kama sehemu ya uhai, furaha na tumaini langu


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ujumbe murua sana huu
 
Gurkha ni nini?
 
Mama yetu katupenda kiasi cha kuzikabidhi bandari zetu kwa mjomba.
 
Shukrani Mshana Jr, ujumbe wako pamoja na kuwa unaonekana kulenga "wanangu", kimsingi unatuhusu sote sisi (sote tuna wazazi). Ujumbe huu na uwe pamoja nasi J'pili hii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…