Helloww guys💁♀️
Last weekend nilikuwa mahali fulani hivi na rafiki zangu wawili wa kike ni katika kubadilisha mawazo na ku-share experiences mbalimbali za kimaisha na changamoto zake,.lakini kubwa lilikuwa ni kurefresh na kufurahia maisha japo kiduchu(baada ya hustles nyingi)...
Sasa katika mawili matatu,rafiki'angu mmoja aliuliza hivi "hivi jamani wenzangu,mnawezaje kukabiliana na hisia za mapenzi zinapokujia?unawezaje kumanage na kuepuka vishawishi na ikiwa uko "totally single" au mpenzi wako yuko mbali na hautamani wala huwezi kucheat(hata ukiwa single unaweza kuji-cheat pia)mnawezaje eti??
Mimi sikuwa na jibu kwa wakati huo kwakweli zaidi ya kumtania "tafuta bebi tuu dia usingo tuachie akina mc"🤗
Sasa,em niambieni hivi wewe unawezaje kuepuka kufanya dhambi hiyo hisia za kuplay "cuve game" zinapokujia(kwa wale singo na ambao hawataki kujisaliti/kusaliti wenza wao)???
Mimi zikininyemelea nasali novena😎