Hayo yote tuyafanyayo, tumeweka Benchmark wapi?

MIXOLOGIST

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2016
Posts
15,524
Reaction score
39,116
Mama Tanzania,

Chochote tufanyacho kama nchi, we are not re-inventing a new wheel, maana yake hicho kitu kuna sehemu kimefanywa, kimefanywa vizuri na kwa ubora na watu wa hiyo sehemu wakayaona manufaa yake.

Je, kuna ubaya gani kujifunza kutoka kwa wenzentu? Borrowing a leaf, benchmarking from a successful story? Je ni kweli bandari kama Rotterdam, Shanghai na Singapore zinafuata mfumo tunaotaka kuuendea?

Ni nini kinachotushinda sisi wenyewe kujiratibu? Hakuna tiba? Uwezo wetu wa akili umefikia mwisho? Ni maslahi mapana ya nchi au ya mtu?

Je haya tunayoyafanya siyo kama muendelezo wa yale aliyoyafanya Chief Mangungo?

Mungu tunakuomba urudishe utimamu wa akili wa taifa letu. Amen.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…