Hawa Mamelodi wapewe tu kombe lao

Half american

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2018
Posts
45,122
Reaction score
111,813
Hii timu kwa msimu huu imezidi kuwa tishio kwenye CAF champions league.

Uwanjani wanakupa kila unachokitaka, mpira mzuri, umiliki wa mpira, magoli mazuri na matokeo mazuri. Naweza kusema wamekamilika mpaka sasa kwa michezo ambayo tumeshaishuhudia ndani ya Ligi ya mabingwa Afrika.

Nnawiwa kuiongeza kwenye list ya timu ninazoshabikia huenda ikanipunguzia maumivu ya Arsenal 🀧.

Hii ni Yanga ya bondeni.

 
Hapana mkuu ule udakaji na Ile visit Tanzania huoni tumetukanishwa..? Visit Tanzania so to see more keepers like him or what..???πŸ€“
πŸ˜‚ watutake radhi watanzania
 
Wanadundaaaa sio kupiga tena
Na wanadunda kweli kweli
Hao wangekutana na Simba wangeogaaa..
Nasikia waliulizwa wanataka wakutane na timu ipi wakaprefer wydad kuliko Simba..
Kumbe unaskia? Endelea kusikia hivyo hivyo ila kwa hii mamelodi ya msimu huu inakanda vilivyo. Simba ingekufa home and away tena mapema sana. Weka ushabiki pembeni
 
Hao wangekutana na Simba wangeogaaa..
Nasikia waliulizwa wanataka wakutane na timu ipi wakaprefer wydad kuliko Simba..
Hapana dada
Kwa hawa jamaa wa mamelody tungeoga magoli nje ndani aisee, balaa la hawa jamaa sio.

Wydad wabovu sana walee, ni uzembe wa simba tuu kwa mkapa kumaliza game mapema
 
Ila yule kipa wa Simba Jana Kama aliambiwa hivi "jirushe upande mmoja tu!!".. nae bila hiana akatuonyesha sambasoti ama sogodati..🀣
Yaani alikuwa kama mtu anajifunza kuogelea kwa mara ya kwanzaπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…