Hawa funza wametoka wapi?

Maiti aliyefukiwa asipoguswa na nzi hatatoa funza nijuzeni

Iron Lady,jibu ni ndio maiti atakayefukiwa na kukingwa kabisa na inzi wasiweze kutaga mayai juu yake basi haitatoa funza(maggots).Si maiti tu hata kwa chakula ama nyama inayooza ikiwa protected vema kutokana na flies haitozalisha funza kamwe.
 
 
Iron Lady,jibu ni ndio maiti atakayefukiwa na kukingwa kabisa na inzi wasiweze kutaga mayai juu yake basi haitatoa funza(maggots).Si maiti tu hata kwa chakula ama nyama inayooza ikiwa protected vema kutokana na flies haitozalisha funza kamwe.
maembe . unakuta umenunua embe unaona nje zuri ndani ukikata lina funza sasa huyu nzi katua saa ngapi ndani ya embe nijuzeni na hapa.
 
maembe . unakuta umenunua embe unaona nje zuri ndani ukikata lina funza sasa huyu nzi katua saa ngapi ndani ya embe nijuzeni na hapa.

Iron lady, hao ni inzi wa embe kitaalamu huitwa Bactrocera dorsalis hufanana sana na manyigu na wana alama ya T mgongoni wanazishambulia embe kwa kuzimeng'enya zikiwa katika hatua za mwanzo za ukuaji na kuingia ndani yake wanapoingia ndani inzi hawa hutaga mayai mengi sana ambayo yatabadilika na kuwa funza,funza hawa mara nyingi hula nyama za ndani za embe na kupelekea embe kuharibika ama kuoza kabisa,na hata kama embe itafanikiwa kuiva na kuonekana nzuri kwa nje bado ndani yake si nzuri kutokana na uwepo wa hao funza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…