Haki ya maandamano.

Azizi Mussa

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2012
Posts
9,198
Reaction score
7,536
Hivi hakuna maandamano yeyote yaliyopangwa kufanyika mwezi ujao ili tuhudhurie maana naona mwezi huu kimyaaa! Any way natania tu wakubwa.

Leo tutafakari kidogo haki ya maandamano.

Ninavyofahamu mimi ni kuwa; haki yeyote ile ya mtu, huishia pale haki ya mtu mwingine inapoanzia. Unaweza kukosoa au kutukana hapa ukipenda.

Sasa hebu fikiria "Scenerios" zifuatazo:

1.Unarudi kazini usiku saa mbili umechokaaaa! karibu na nyumba yako kuna mtu anauza pombe, kafungulia mziki kwa sauti kubwaaaaa, halafu ukimwambia apunguze au audhibiti usisambae ili uweze kulala, anakuambia anachokifanya ni haki yake, halafu anaendelea mpaka saa nane usiku.Unajisikia je? je! unadhhani ni sawa? unajifunza nini kwa haraka?

2. Mwanao anaumwa sana, anaonekana anashindwa kupumua, umeshauriwa kumuwahisha hospitali maeneo ya mjini, umekopa hela umekodi taxi kumkimbiza, unafika njiani unakuta njia haipitiki, unauliza kuna shida ganilunaambiwa mbele kuna maandamano, mwanao anapoteza maisha.Unajisikia je! unatafsiri je dhana ya haki za watu?

3. Umechukua ka-mkopo benki baada ya kuomba ajira kwa miaka mitano bila mafanikio.Umeanza kuuza vinjwaji barabarani.siku moja watu wanavamia kakibanda kako wanakunywa vinjwaji vyote kwa hoja ya kuwa yalikuwa ni maandamano. Utatafsirije kinachoitwa haki ya kuandamana?

Nadhani kwa scenerio hizi chache sasa naweza kuuliza swali la msingi.Hivi ikiwa lengo la maandamano ni kufikisha ujumbe kwa watu fulani, hakuna njia nyingine inayoweza kutumika na ikafikisha ujumbe bila kuleta madhara kwa watu wengine ili haki ya mtu mmoja isiwe kizuizi na kikwazo kwa haki za wengine, au haki za kundi fulani zisiwe kikwazo cha haki za wengine?

KARIBUNI;


 
Post zako zinanifunza kitu kimoja tu katika msemo wa watu wenye hekima kuwa ''kisebusebu na kiroho papo''...........
 
Au kwa lugha nyingine, kwa nini ufikishaji ujumbe kwa njia ya mikutano ya hadhara, press conference na mikutano ya kawaida isiwekewe mazingira mazuri zaidi kama njia kuu za ufikishaji habari na maandamano yakawekewe mazingira magumu zaidi kwa kuwa njia hiyo ina hasara kubwa kuliko faida na wakati kundi moja linaitumia, linaathi haki za wengine?
 
mwambie mbowe hayo maneno aupasue!

others don't think about others.
 
Post zako zinanifunza kitu kimoja tu katika msemo wa watu wenye hekima kuwa ''kisebusebu na kiroho papo''...........

Haufikiri kwamba kama ungejadili mada ingekuwa poa zaidi kuliko kunijadili mimi hasa ukizingatia kuwa mada hainihusu kwa namna yeyote! samahani lakini kama nitakuwa nimekukwaza.

 
Mkuu heshima kuu kwako iwe mkutano wa hadhar iwe barua au simu au hata radio lengo ni ujumbe ufike kwa wakati lakin unanoga zaid na unachukuliwa hatua haraka kma umekuja kwa haraka pia; maandamano ndio njia sahih ya kufikisha meseji kwa haraka hasa kwa watawala dhalimu na makupe wenzao kama act; tlp;udp nk so tutaandamana mpaka mwisho kwani kwenye maandamano hatukuwahi kuiba cha mtu wala kuharibu cha mtu ; tunapita kwenye barabara zilizo tengenezwa kwa kodi zetu kaka
Haufikiri kwamba kama ungejadili mada ingekuwa poa zaidi kuliko kunijadili mimi hasa ukizingatia kuwa mada hainihusu kwa namna yeyote! samahani lakini kama nitakuwa nimekukwaza.

 
Vijana wa kitanzania tupo tupu sana kichwani sijui shida ni nini..!? Eti hapa ni mtu kakaa kuleta mjadala wa kijinga kama huu na ukute anajiona GT..
 
Hivi ni kweli kila maandamano lazima yaishie kwenye fujo? Haiwezekani kuwa na maandamano ya amani?? Tuangalie pia kwa upande mwingine kwa nini kusiwe na utaratibu wa watu kuruhusiwa kuandamana kwa amani? Kwa sababu ilishasemwa maandamano ni haki ya kikatiba!
 
 
Vijana wa kitanzania tupo tupu sana kichwani sijui shida ni nini..!? Eti hapa ni mtu kakaa kuleta mjadala wa kijinga kama huu na ukute anajiona GT..

na bado aliye comment hapo kumkomoa mwingine anajiona yuko mtimilifu sana kichwani mwake...
 
na bado aliye comment hapo kumkomoa mwingine anajiona yuko mtimilifu sana kichwani mwake...

Tatizo kila mtu anamshangaa mwenzake jinsi alivyo wa ajabu.Kazi kweli

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…