Eti taifa stars walifunga!?!!!!?

Mzalendo Mkuu

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2010
Posts
735
Reaction score
191
Tanzania imekuwa ni nchi ya utani na mambo makubwa. Inasemekana sehemu kubwa ya wachezaji WALIFUNGA RAMADHANI!!!! Ni utani. Funga na mpira WAPI na WAPI?
 
Ni kweli kuna Uhuru wa kuabudu. Kwangu mimi ni BORA kocha angechagua wachezaji wa timu ya pili WASIOFUNGA kuliko hao wasiokula. Mpira ni nguvu, mpira ni chakula. Tulitegemea kupata nini kutoka kwa mchezaji ALIYENGA RAMADHANI? Ni comedy tu ndiyo tunaiwezea.
 
Hujasikia wachezaji wanaofunga kwenye ligi za Ulaya huko?

Mbona haitolewi kuwa sababu ya timu kufungwa (au kushinda?)
 
hatuna approach ya kisayansi ya michezo, wazungu wanakua na dietitian anayewamonitor wachezaji waliofunga na mambo yanaenda vizuri tu, so, yeah kama hatuna watu wanaofanya mambo kitaalamu, urahisi ni kuchagua wachezaji wasiofunga na kuanzisha mambo ya udini kama kawa..
 
Uganda hakukuwa na waliokuwa wamefunga?ni njia ya kujifaliji tu,miaka 6,sasa kila cku tunajenga timu!
 
Hujasikia wachezaji wanaofunga kwenye ligi za Ulaya huko?

Mbona haitolewi kuwa sababu ya timu kufungwa (au kushinda?)


Hao kina Demba Ba na mwenzake Papiss Cisse wamekiri kuwa huwa wanafunga lkn siku ya mechi hawafungi kwa kuelewa umuhimu wa mechi. Nitashangaa sana ikithibitka kuwa kina Kiemba walifunga jana na bado kocha akawapanga
 
Hujasikia wachezaji wanaofunga kwenye ligi za Ulaya huko?

Mbona haitolewi kuwa sababu ya timu kufungwa (au kushinda?)

Ulaya hata kama wapo wachezaji waliofunga huwa ni Wangapi? Kunaweza kuwa mmoja ambaye atacheza 45mn.

Shida ya Tanzania ni kuwa robo tatu ya wachezaji ni wale wa kufunga. Ndiyo maana kipindi cha kwanza walikuwa na nguvu na baadaye wakawa ndembe.....
 
Tafuteni sababu nyingine ya kushindwa sio kufunga, starting 11 ya siku ile waislam walikuwa wanne tu Kaseja, Salum Abubakar, Mrisho Ngassa na Amir Kiemba. Kati ya hao waliofunga ni wawili tu Kaseja na Kiemba, Ngasa na Salum Abubakar hawakufunga tuliwaona wakinywa maji afterall ni wavuta bangi wamfungie nani?

Waliobaki ni wa dini nyingine.

NB Shomari Kapombe na Mwinyi Kazimoto ni wakristo ila wana majina yanayo shabihiana na uislam
 
Hao kina Demba Ba na mwenzake Papiss Cisse wamekiri kuwa huwa wanafunga lkn siku ya mechi hawafungi kwa kuelewa umuhimu wa mechi. Nitashangaa sana ikithibitka kuwa kina Kiemba walifunga jana na bado kocha akawapanga

Kumkataza mtu asifanye kazi kwa sababu tuu ya ku-practice dini yake ni ubaguzi at its best.

Wakati timu na mameneja wanajaribu kuelewa na ku-accomodate mahitaji ya kidini ya wachezaji wewe ndiyo kwanza unashangaa?

Nitakushangaa sana kama utashangaa kama "ikithibitka kuwa kina Kiemba walifunga jana na bado kocha akawapanga".

Mbona Edin Dzeko wa Man City alifunga mabao manne dhidi ya Spurs mwaka juzi wakati akiwa amefunga?

Of course, kuna dilemma ya whether mchezaji ambaye hajala wala kunywa kwa masaa karibu 18 kucheza kwa kiwango cha hali ya juu kwa dakika tisini lakini ni muhimu kuelewa kuwa kufunga ni special moment kwa kila Muislamu wakiwemo wachezaji.

Kwa hiyo, badala ya kushangaa ni bora kuangalia timu na mameja wanaweza ku-balance mambo vipi kwa faida ya pande zote mbili.
 
Hujasikia wachezaji wanaofunga kwenye ligi za Ulaya huko?

Mbona haitolewi kuwa sababu ya timu kufungwa (au kushinda?)

Kuna kali ya mwaka ilitokea ans I was waiting for it kwa muda mrefu sana.

Kwa kawaida kwenye ligi za Ulaya Man of Match huwa anapewa a bottle of champagne.

Basi nikawa najiuliza huwa inakuwaje kama Man of the Match hanywi alcohol kwa sababu mbalimbali kama dini yake?

Siku moja nikawa naangalia post-match interview ambapo Yaya Toure (Muislamu) alikuwa Man of Match.

Alipokabidhiwa champagne aliikataa na kumpa mchezaji mwenzake aliyekuwa pembeni mwake akisema: "I don't drink because I am a Muslim, so you keep it."

Ndipo hapo waandaaji wa ligi wakashtuka pamoja na kuwa ligi hiyo imekuwa na wachezaji wa Kiislamu tokea mwaka 1992.

Sijui kama walidhani a Muslim player will never be a Man of the Match au walikuwa wanapokea tuu hizo champaigne.

Hata hivyo, baada ya Toure kuikataa "live" wamebadilisha na sasa Man of the Match anapewa kikombe kidogo to the detriment ya manufacturer na aliyekuwa ana-supply hizo champagne.
 
Ulaya hata kama wapo wachezaji waliofunga huwa ni Wangapi? Kunaweza kuwa mmoja ambaye atacheza 45mn.

Shida ya Tanzania ni kuwa robo tatu ya wachezaji ni wale wa kufunga. Ndiyo maana kipindi cha kwanza walikuwa na nguvu na baadaye wakawa ndembe.....

Una maana kuwa wakati wa mfungo wa Ramadhani basi michezo yote isimame kwa sababu "robo tatu ya wachezaji ni wale wa kufunga"?

Yaani tokea miaka yoooote ndiyo kwanza naona watu wakijadili timu kufungwa kwa sababu wachezaji walikuwa wamefunga.

Ina maana huko nyuma walikuwa hawafungi?
 

shomari ali kapombe na mwinyi kazimoto sidhani kwenye profile zao za Twitter na FB Wameji identify kuwa ni Muslims na shomari namjuwa tokea morogoro ni muislam
 

New Castle United, msimu uliopita, ulitenga chumba maalum cha kusalia kwa wachezaji wake saba ambao ni Waislam.

Wakati wenzetu wanapiga hatua kwenye kutoa uhuru wa kuabudu, sisi tunataka kurudi nyuma

Liverpool FC kwenye tovuti yake imeweka makala juu ya wachezaji na Ramadhani baada ya Kolo Toure kusema yeye anafunga.

Makala hiyo inayoitwa "How we prepare players for Ramadan" katika mfumo wa mahojiano na daktari wa timu Zaf Iqbal ambae nae ni Muislam, inajaribu kuonyesha namna gani timu inachukua hatua kufacilitate performance ya wachezaji wakati huo huo kuhakikisha pia hawabani uhuru wao wa kuabudu

Sisi kwetu tujiulize, makocha na madaktari wamechukua hatua gani?
 
Reactions: EMT
Tanzania imekuwa ni nchi ya utani na mambo makubwa. Inasemekana sehemu kubwa ya wachezaji WALIFUNGA RAMADHANI!!!! Ni utani. Funga na mpira WAPI na WAPI?
Mbona Iraq wanafanya vizuri U-20 wakiwa wote wamefunga?
 
Hao kina Demba Ba na mwenzake Papiss Cisse wamekiri kuwa huwa wanafunga lkn siku ya mechi hawafungi kwa kuelewa umuhimu wa mechi. Nitashangaa sana ikithibitka kuwa kina Kiemba walifunga jana na bado kocha akawapanga

Huko kwenye ligi za Ulaya, wapo wachezaji tele wanaofunga huku wanacheza

Demba Ba alimwambia kocha kuwa anafunga na akiona hachezi vizuri amuweke benchi, ila yeye hawezi kufungua (source: BBC Sport - Premier League: How Muslims are changing English football culture )

Abou Diaby, Fredrick Kanoute, Mahammadou Diara, Karim Benzama......wote wanafunga wakati wa Ramadhani na kocha huwa anawapanga
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…