Ufunuo wa Yohana 14 : 13 Nikasikia sauti kutoka
mbinguni ikisema, Andika,
Heri wafu wafao katika Bwana
tangu sasa. Naam, asema Roho,
wapate kupumzika baada ya
taabu zao; kwa kuwa matendo
yao yafuatana nao.
1 Wathesalonike 4 : 13-18
4.13 Lakini, ndugu, hatutaki
msijue habari zao waliolala
mauti, msije mkahuzunika kama
na wengine wasio na matumaini.
4.14 Maana, ikiwa twaamini ya
kwamba Yesu alikufa akafufuka,
vivyo hivyo na hao waliolala
katika Yesu, Mungu atawaleta
pamoja naye.
4.15 Kwa kuwa twawaambieni
haya kwa neno la Bwana,
kwamba sisi tulio hai,
tutakaosalia hata wakati wa kuja
kwake Bwana, hakika
hatutawatangulia wao
waliokwisha kulala mauti.
4.16 Kwa sababu Bwana
mwenyewe atashuka kutoka
mbinguni pamoja na mwaliko, na
sauti ya malaika mkuu, na
parapanda ya Mungu; nao
waliokufa katika Kristo
watafufuliwa kwanza.
4.17 Kisha sisi tulio hai,
tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja
nao katika mawingu, ili tumlaki
Bwana hewani; na hivyo tutakuwa
pamoja na Bwana milele.
4.18 Basi, farijianeni kwa
maneno hayo.