Democracy:this is why i love you

mafinga kwetu

Member
Nov 21, 2010
35
3
SAY YES AND THE OTHER ONE CAN SAY NO…AND BOTH CAN BE RIGHT AND PEACEFUL…
Mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA,Dr.Wilbroad Slaa,akimnadi mgombea ubunge katika Jimbo la Ubungo kupitia chama hicho,John Mnyika.Wapiga kura wengi bila shaka walikubaliana na ombi la Dr.Slaa kwa kumchagua Mnyika kuwa mbunge wao mpya.
JK alipokuwa akimnadi Basil Mramba aliyekuwa mgombea Ubunge kwa tiketi ya CCM katika Jimbo la Rombo mkoani Kilimanjaro.Kwa bahati nzuri au mbaya,wapiga kura walikuwa na mtazamo tofauti.
Mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA,Dr.Wilbroad Slaa,akimnadi mgombea Ubunge kupitia chama hicho katika Jimbo la Karatu,Mchungaji Israel Natse.Wapiga kura jimboni hapo waliafikiana na Dr.Slaa na kumchagua Mch.Natse kuwa Mbunge wao mpya.
Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM,Jakaya Kikwete,akimnadi Mgombea Ubunge kwa tiketi ya chama hicho katika Jimbo la Nyamagana mkoani Mwanza,Lawrence Masha.Huko nako wapiga kura walikuwa na mtazamo tofauti.Demokrasia ikaamua.
Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Jakaya Kikwete,akimnadi mgombea Ubunge kwa tiketi ya chama hicho katika Jimbo la Ilemela mkoani Mwanza,Anthony Diallo.Wapiga kura walikuwa na mrengo tofauti.
Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM,Jakaya Mrisho Kikwete,akimnadi mgombea Ubunge kupitia tiketi ya chama hicho katika Jimbo la Monduli,aliyewahi kuwa Waziri Mkuu,Edward Lowassa.Wapiga kura wa jimbo hilo walikubaliana na ombi la Jakaya Kikwete kwa kumrudisha bungeni Mh.Lowassa.


Read more: BongoCelebrity
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…