Wenzako waliokuwa na mawazo kama yako hasa kabla ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa siku hizi hawatoi hoja kama hizi. Mfano Mtwara Mjini CUF imepata mitaa 36, CHADEMA imepata 16 na NCCR imepata 5. Nachingwea CUF imepata vijiji 13, CHADEMA imepata 12, CUF kina Diwani 1 na CHADEMA Madiwani 4. Nanyumbu CUF imepata vijiji 9, CHADEMA imepata vijiji 6, CUF kina Diwani 1 na CHADEMA Diwani 1.
Sumbawanga Mjini CHADEMA kimepata Mitaa 102 kati ya 165. Kanda ya Serengeti (Shinyanga, Simiyu na Mara) CHADEMA kimeshinda kwa 48% katika Mitaa na Vijiji vyote kwa ujumla. Je, huko kote ni Kaskazini?