mwanamwana
JF-Expert Member
- Aug 1, 2011
- 1,410
- 4,988
Chama cha Demokraska na Maendeleo CHADEMA kupitia kwa Katibu Mkuu wake Bw. John Mnyika leo Aprili 02, 2025 kimetangaza kutengua uteuzi wa Bw. Julius Mwita, aliyekuwa Katibu wa Sekretarieti ya Chadema.
Taarifa hii ni kulingana na vyanzo vyetu vya kuaminika kutoka ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA.
Kutenguliwa kwa Katibu huyo wa Sekretarieti ya Chadema kumekuja muda mfupi baada ya mzozano mkali ulioibuka mtandaoni, ukihusisha makada na wanachama wa Chadema, mara baada ya kuvuja kwa mawasiliano ya kundi sogozi la WhatsApp, lenye Viongozi mbalimbali wa sasa, wastaafu na wanachama wa Chadema waliokuwa wakipanga mikakati mbalimbali ya kudhohofisha na kupingana na vuguvugu la Chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania ya No Reforms, No election.
Katika Wingi wa ujumbe wao mfupi uliopigwa picha "screenshot" na kusambazwa kwenye mtandao wa X,na kile kinachotajwa kama 'huenda' ndiyo ikawa sababu ya kuenguliwa kwake, Mwita ameonekana akieleza kuwa;
"Iko hivi wakuu, ni bora kwenda (Kwenye kikao kilichoitishwa na Chama kikikusisha wanaotaka kuwania Ubunge), tutafute na watu wengine ambao wanaweza kufanya interview (Mahojiano) na Media (Vyombo vya habari) na kutoa maoni tofauti. Sasa tutawakimbia mpaka lini?na ni wapi na kwa namna gani tutaonesha kuwa hatuwaungi Mkono?"
Mwita ameendelea kuandika kusema kuwa " Hiki kikao (Kikao cha Chama na wanachama wanaotaka kuwania ubunge 2025) ni mwiba kwao na kama boss wao anaona wamemsaliti. Matokeo yakiwa makubwa itakuwa na maana kwamba watu wanaotaka ubunge ni wengi na ikiwa watakasirishwa nao, jamii haitaweza kuwaelewa."
"Ukiwaacha wakakutana na watu wachache, hisia itakayojengwa ni kuwa watu wameelewa na kuunga mkono No reforms, No election"Hii itajenga tafsiri kuwa UJINGA wao umekubalika kwa kila MwanaChadema na ndio maana hakuna wanaoutaka Ubunge" ameandika Mwita kwenye moja ya Ujumbe wake uliopigwa picha na kusambazwa mtandaoni.
Katika Ujumbe mwingine alioonekana Bw. Mwita kuusambaza ulisomeka kusema " waheshimiwa tumeletana hapa sisi kama wabunge tunaozungumza lugha moja ili tuwe na mkakati wa pamoja, lengo ni angalau tufikie 55.Karibuni na leteni majina ya wengine tunaoelewana (Tunaopinga No Reforms, No election)
Aidha Mwita katika picha zilizosambazwa mtandaoni ameonekana akihoji kusema "Namna gani uchaguzi unazuiwa, ikiwa serikali na CCM na wengine wanaendelea na maandalizi? Vipi ikiwa uchaguzi utafanyika na Chadema ikashindwa kuuzuia, nini hatma ya Chama kwa miaka mitano ijayo?" Amenukuliwa Mwita ambaye kibarua chake kimeripotiwa kukoma hii leo.
Taarifa hii ni kulingana na vyanzo vyetu vya kuaminika kutoka ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA.
Kutenguliwa kwa Katibu huyo wa Sekretarieti ya Chadema kumekuja muda mfupi baada ya mzozano mkali ulioibuka mtandaoni, ukihusisha makada na wanachama wa Chadema, mara baada ya kuvuja kwa mawasiliano ya kundi sogozi la WhatsApp, lenye Viongozi mbalimbali wa sasa, wastaafu na wanachama wa Chadema waliokuwa wakipanga mikakati mbalimbali ya kudhohofisha na kupingana na vuguvugu la Chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania ya No Reforms, No election.
Katika Wingi wa ujumbe wao mfupi uliopigwa picha "screenshot" na kusambazwa kwenye mtandao wa X,na kile kinachotajwa kama 'huenda' ndiyo ikawa sababu ya kuenguliwa kwake, Mwita ameonekana akieleza kuwa;
"Iko hivi wakuu, ni bora kwenda (Kwenye kikao kilichoitishwa na Chama kikikusisha wanaotaka kuwania Ubunge), tutafute na watu wengine ambao wanaweza kufanya interview (Mahojiano) na Media (Vyombo vya habari) na kutoa maoni tofauti. Sasa tutawakimbia mpaka lini?na ni wapi na kwa namna gani tutaonesha kuwa hatuwaungi Mkono?"
Mwita ameendelea kuandika kusema kuwa " Hiki kikao (Kikao cha Chama na wanachama wanaotaka kuwania ubunge 2025) ni mwiba kwao na kama boss wao anaona wamemsaliti. Matokeo yakiwa makubwa itakuwa na maana kwamba watu wanaotaka ubunge ni wengi na ikiwa watakasirishwa nao, jamii haitaweza kuwaelewa."
"Ukiwaacha wakakutana na watu wachache, hisia itakayojengwa ni kuwa watu wameelewa na kuunga mkono No reforms, No election"Hii itajenga tafsiri kuwa UJINGA wao umekubalika kwa kila MwanaChadema na ndio maana hakuna wanaoutaka Ubunge" ameandika Mwita kwenye moja ya Ujumbe wake uliopigwa picha na kusambazwa mtandaoni.
Katika Ujumbe mwingine alioonekana Bw. Mwita kuusambaza ulisomeka kusema " waheshimiwa tumeletana hapa sisi kama wabunge tunaozungumza lugha moja ili tuwe na mkakati wa pamoja, lengo ni angalau tufikie 55.Karibuni na leteni majina ya wengine tunaoelewana (Tunaopinga No Reforms, No election)
Aidha Mwita katika picha zilizosambazwa mtandaoni ameonekana akihoji kusema "Namna gani uchaguzi unazuiwa, ikiwa serikali na CCM na wengine wanaendelea na maandalizi? Vipi ikiwa uchaguzi utafanyika na Chadema ikashindwa kuuzuia, nini hatma ya Chama kwa miaka mitano ijayo?" Amenukuliwa Mwita ambaye kibarua chake kimeripotiwa kukoma hii leo.