CECAFA KAGAME CUP 2011 Finals in Tanzania

Japo mie si mwanayanga lakini naona wako vizuri, tatizo leo siko uwanjani naangalia kwenye TV, Yanga wakikaza hivi hivi wanaweza kushinda maana wanafika golini mara kwa mara, Line up leo sijaipata vizuri labda niitaje tu bila mpangilio; Berko, Godfrey Taita, Cannavaro, Marwa, Mrope, Nurdin Bakari, Rashid Gumbo, Davis Mwape, Asamoah ameingia badala ya Tegete, Makasi, Oscar Joshua,
 
El.Mereikh wamejifunga tena dk35. Yanga 2:1E M
 
Sio siri Yanga mkiwatunza vizuri wachezaji wenu mashindano ya klabu bingwa mnaweza kufika mbali hasa pale upepo wa timu kubwa kubwa usipowapitia.
 
Mpira ni mapumziko, Yanga 2-1 El Mereikh..
 
Yanga hamna aliyefunga yote El Mareikh wamejifunga 2-1 ina maana magoli yote matatu yanga hawajafunga hata moja kwa ufungaji lakini.
 
Simba hamna kitu acheni maneno ya kitoto, Yanga wanawasubiri unamuona hapa Jogoo la Jangwani likikiminja ni kuku cha Kariakoo? Jamaa wanasema wanamsubiri mnyama ha ha ha ha
 
Kipindi cha pili kimeanza, bado mabao ni yanga 2-1 El Mereikh.

Na kule Morogoro APR 1-0 Ports.
 
Kipindi cha pili kimeanza na Yanga wamekosa goli la wazi hapa.....Mwape!
 
Simba hamna kitu acheni maneno ya kitoto, Yanga wanawasubiri unamuona hapa Jogoo la Jangwani likikiminja ni kuku cha Kariakoo? Jamaa wanasema wanamsubiri mnyama ha ha ha ha
Ahahahaaah!!
 
yanga wamezidiwa, jamaa wanamiliki mpira vizuri kipindi hiki cha pili!
 
Nsajigwa anafunga ndoa leo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…