Chama Cha Mapinduzi(CCM) kupitia aliyekuwa mgombea wake,Dr.Dalali Kafumu(pichani) kimeibuka mshindi katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Igunga mkoani Tabora.Dr.Kafumu ameshinda kwa kupata jumla ya kura 26,488 huku kikifuatiwa kwa karibu na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) kilichojipatia kura 23,260.