CCM Zanzibar kimewaonya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wa chama hicho watakaounga mkono hoja ya kuundwa Serikali ya mseto, kinyume na azimio la Butiama la mwaka 2008, kwamba watachukuliwa hatua za kinidhamu.
Katibu Mwenezi wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai, alisema hayo visiwani hapa jana alipokuwa akizungumzia maazimio ya kikao cha Halmashauri Kuu Maalum ya CCM Zanzibar, kilichokutana juzi, chini ya Mwenyekiti wake, Rais Amani Abeid Karume.