Umesema ukweli kabisa....pamoja na mabaya yake yote jk ni mtu muungwana na mstaarabu sana...nimeshuhudia mara kadhaa akivuka kigamboni kwenda kumsabahi mzee wake jumbe...hao wengne syo watu kabisaJinsi Mzee Jumbe alivyokuwa treated ni aibu sana kwa Taifa hili
Mzee Jumbe alionwa kama mhalifu wa kivita
ata akina Mwinyi,Mkapa na huyu MAGUFULI wote hawakumthamini Mzee Jumbe
Kidogo JK aliheshimu utu wa Mzee Jumbe
Lkn sasa kafariki utaona unafiki wao
Nyerere alikuwa kiongozi mbaya sana kupata kutokea Africa
Ukipingana nae kwa hoja kesho huruhusiwi tena kutoka chumbani kwako
Kama kweli kuna JEHANAM basi yawe makazi ya kudumu ya Mwl Nyerere
JK is my best President everUmesema ukweli kabisa....pamoja na mabaya yake yote jk ni mtu muungwana na mstaarabu sana...nimeshuhudia mara kadhaa akivuka kigamboni kwenda kumsabahi mzee wake jumbe...hao wengne syo watu kabisa
Hakuna tena raha ya kuishi ..kama mtu utanyimwa uhuruJK is my best President ever
Ninyime uchumi nipe uhuru wangu.
Kuna raha gani kuendesha new model Benz lkn unalazwa mahabusu Keko kila jioni sababu tu umekataa kauli fulani ya Rais MAGUFULI?
Nipe uhuru wangu hata mchicha nitakula!
Ngd Rangimoto asante kwa hili shairi. Nauliza hywamunachapisha kwenye moja ya magazeti. Naomba lichapwe kwenye mwananchi.View attachment 381574
1
Hodi hodi kisimani, nina habari si nzuri,
Babu yetu Kigamboni, ameitwa na Qahari,
Jumbe si wa duniani, kaenda ile safari,
Tutawaona dhahiri, wanafiki uwanjani.
2
Maisha yake huzuni, yajulikana dhahiri,
Katiwa kizuizini, ati si mtu mzuri,
Akatengwa Kigamboni, marufuku kusafiri,
Tutawaona dhahiri, wanafiki uwanjani.
3
Alo yasema zamani, hadharani bila siri,
Kayatia kitabuni, mzee huyu jasiri,
MUUNGANO wa yakini, akafanya tafasiri,
Tutawaona dhahiri, wanafiki hadharani.
4
Ikazuka tafarani, heri ikazaa shari,
Vyombo havielewani, vidau na manowari,
Kaskazi mkondoni, imechafuka bahari,
Tutawaona dhahiri, wanafiki hadharani.
5
Katolewa mjengoni, urais ndo kwaheri,
Hakurudi na nyumbani, sasa miaka dahari,
Meli yake Magogoni, hakugusa Zanzibari,
Tutawaona dhahiri, wanafiki hadharani.
6
"Kweli" itie shimoni, uichinje na buchari,
Ama itie motoni, jua tabaki ngangari,
Ipo siku tabaini, "kweli" ilivyo nawiri,
Tutawaona dhahiri, wanafiki hadharani.
7
Turejee MAONI, ya katiba nashauri,
Mtaona naamini, Jumbe alivyoshamiri,
Miaka ni thelathini, mawazo bado ngunguri,
Tutawaona dhahiri, wanafiki uwanjani.
8
Salamu toka kijani, tumepoteza hodari,
Kutoka serikalini, Jumbe kafa jasiri,
Tuwasute bila soni, zikome zao ghururi,
Tutawaona dhahiri, wanafiki uwanjani.
9
Salamu za upinzani, Jumbe hakuwa hatari,
Haki alivyoamini, huletwa kwa kusubiri,
Ndio sababu jueni, isizuke halibari,
Tutawaona dhahiri, wanafiki hadharani.
10
Wapinzani ahsanteni, na mtupe ikirari,
Siku gani hasa lini, mlikipanda kihori,
Mkenda kwake nyumbani, kumpa japo habari
Tutawaona dhahiri, wanafiki hadharani.
11
Sasa niko tamatini, kufunga langu shairi,
Kuuliza natamani, mjibu pasi dosari
Alofia gerezani, vipi watamstiri?
Tutawona dhahiri, wanafiki uwanjani
12
Mizinga iwe ugani, na mbwembwe za askari,
Msafara mazikoni, pikipiki na magari,
Watu wale biriani, ya mchele wa pishori,
Tutawaona dhahiri, wanafiki uwanjani.
13
Huenda hadi mwishoni, kabaki kuwa guberi,
Mumzike kihaini, mithili ya makafiri,
Mkumbuke na hisani, viumbe mtahayari,
Tutawaona dhahiri, wanafiki uwanjani.
Dotto Rangimoto Chamchua(Njano5)
call/whatspp 0622845394 Morogoro
Kama sasa hiviHakuna tena raha ya kuishi ..kama mtu utanyimwa uhuru
Watu tumefungwa midomo sio upinzani wala ccm. Afadhali ya upinzani ccm wanaogopa kitumbua kuingia mchanga. Poor my country. The beautiful ones are not yet born. Waliyemtegemea kawa mbovu kupita waliotangulia wote. Kwa heri uhuru wa kuongea. MUNGU BARIKI NA ONGOZA UKUTA UFANIKIWE. Lakini hakuna marefu yasiyokuwa na ncha.Kama sasa hivi
Ukiandikiana na mpenzi wako Whatsap Kama Magufuli ndiyo kasababisha sukari ipande bei wakiona polisi unafungwa
Hamna uhuru wa kujieleza
CCM ndogo wanaumia zaidi!Anacho kisema MTUKUFU hapingwi na yyt yule!Watu tumefungwa midomo sio upinzani wala ccm. Afadhali ya upinzani ccm wanaogopa kitumbua kuingia mchanga. Poor my country. The beautiful ones are not yet born. Waliyemtegemea kawa mbovu kupita waliotangulia wote. Kwa heri uhuru wa kuongea. MUNGU BARIKI NA ONGOZA UKUTA UFANIKIWE. Lakini hakuna marefu yasiyokuwa na ncha.
Kwani wanajali Mkuu?Nasikia aliacha wosia kuwa akifa jeneza Lake lisifunikwe na bendera ya ccm wala taifa.. Hii ni pigo lumumba aisee
Ni sawasawa na baba anayeacha buku ya chakula halafu anategemea pilau la nyama ya kuku!CCM ndogo wanaumia zaidi!Anacho kisema MTUKUFU hapingwi na yyt yule!
Nilikuwa naongea na afisa wa CCM Lumumba kaniambia kuwa hata kuhamia Dodoma kwa serikali hii HAKUKUWEPO ktk mipango ya CCM na hawajawahi hata kujadili
Juzi akiwa Mwanza kaagiza Busisi kuwe na daraja refu lkn hamna hata sehemu kwenye bajeti katenga pesa yyt kwa ajili hiyo
Mtu kama Mzee Jumbe kwa mambo haya ya serikali hii angejiuzuru
Upo sahihi kabisaNi sawasawa na baba anayeacha buku ya chakula halafu anategemea pilau la nyama ya kuku!
Mkuu kuna mtu kijijini alivyofariki, alivyokuwa anazikwa watu walisema shimo liwe refu sana kiasi cha kutoweza kusikia hata honi zikipigwa. Yote hii ni shauri ya majivuno. Sasa huyu watu wasije ombea angekuwa kwenye ile ndege ya Malasia. Km hata wenzio hawakupendi ni wanafiki what do u expect. Kwa kweli waliodhani wamepata kumbe imekula kwao. Tuwe na subira Mola atawezesha yote. Ndivyo ninavyojipa moyo. Kwani sie tulimkosea nini? Up rising iko njiani.CCM ndogo wanaumia zaidi!Anacho kisema MTUKUFU hapingwi na yyt yule!
Nilikuwa naongea na afisa wa CCM Lumumba kaniambia kuwa hata kuhamia Dodoma kwa serikali hii HAKUKUWEPO ktk mipango ya CCM na hawajawahi hata kujadili
Juzi akiwa Mwanza kaagiza Busisi kuwe na daraja refu lkn hamna hata sehemu kwenye bajeti katenga pesa yyt kwa ajili hiyo
Mtu kama Mzee Jumbe kwa mambo haya ya serikali hii angejiuzuru
Halafu lugha yake sio nzuri hata. Eg mfyatue watoto ni kudhalilisha.Upo sahihi kabisa
Rais kinacho mjia kichwani anakisema tu kama tupo kwenye kampeni
Huyu ni Donald Trump wetu
Kwqnza mtoto ambaye nitapata leo akifikisha miaka 9 ndiyo yy anaondoka madarakani!Sasa mtoto wa miaka 9 atasoma sekondari?Halafu lugha yake sio nzuri hata. Eg mfyatue watoto ni kudhalilisha.