Biashara ya majeneza

pantheraleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2013
Posts
692
Reaction score
887
Habari wana JF wenzangu wa nguvu? Mimi ni mfanyabiashara wa siku nyingi,ila sijawahi kufanya biashara ya majeneza. nasikia ni biashara ambayo inalipa lakini nayo ina msimu. Kuanzia mwezi wa 10 hadi wa 12. Na miezi ya katikati ni kuskilizia na kupata lakini si ka miezi niliyoitaja hapo juu. Naomba wataalamu wa hii biashara wanipe idea ya hii biashara. Nahitaji kufanya ndio maana naulizia. Karibuni.
 
Uombapo mafanikio katika biashara hii maana yake unaomba watu waongeze kasi ya kufa. Inanikumbusha mchonga majeneza mmoja alinusurika kupigwa alipowaambia wateja wake "karibuni tena siku nyingine".
 
Unaweza ukatamani kuua watu ili biashara itoke!
Achana na hiyo biashara hiyo miezi ulioitaja ni miezi ya Ajari Nyingi kuongezeka barabarani kutokana na watu wengi kusafiri kwa mapumziko na sikukuu za mwisho wa Mwaka!
 
Hapana mzee. Ila ni biashara ambayo kwa upande mwingine inatusaidia kuhifadhia maiti na kusafirisha na hata kuzika kwa sisi wakristo.
 
sijaelewa we ni fundi kapenta au? au unataka ununue uuze? hebu jaribu kuanza iyo biashara pale unapokaa
 
labda ungeanza kufa wewe kwanza uzikwe katika jeneza la kwanza utakalotengeneza
kisha ukiwa huko kuzimu utaona faida za hiyo biashara.
 
labda ungeanza kufa wewe kwanza uzikwe katika jeneza la kwanza utakalotengeneza
kisha ukiwa huko kuzimu utaona faida za hiyo biashara.

Umenielewa vibaya kaka. Ni mawazo tu nilikuwa nahitaji ila sio kejeli. Hata wewe ukifa utazikwa na hilo hilo jeneza.
 
huku TZ Hizi biashara zinafanywa na wakora, ambao akili zao haziko vizuri. Hata ile ya Mortuary!
 
Mm Ni Fundi seremala miaka 8 sasa.hakuna kazi Nisio ipenda kama Kutengeneza jeneza.
 
huku TZ Hizi biashara zinafanywa na wakora, ambao akili zao haziko vizuri. Hata ile ya Mortuary!

Kwahiyo mkuu hii biashara haifanywi na watu wenye akili timamu,wasingekwepo mngepatia wapi hayo majeneza?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…