Kuna kipindi miaka ya nyuma nikienda na mzee shambani Kabuki. Nilikuwa ndio nimemaliza f4. Mzee alikuwa na Nissan double cabin kipindi hicho. Kulikua na mvua kubwa, kutoka shambani mbele kidogo tu gari ikakwama.
Sasa kule kabuku Kuna kambi ya jeshi, gari imekwama katikati ya barabara, wakatokea wanajeshi wanafunzi Lori zima na maafande wao nadhani walikuwa wanaelekea kabuku mjini.
Kuona gari imekwama wakashuka wakamwambia mzee ingia ndani ya gari, na Mimi nilivyo bwege nikaingia wakaisukuma ile gari mpaka sehemu salama. Mzee alivyo mstaarabu akapaki akashuka awashukuru, lilikuwa kosa kubwa, wale jamaa walinibeba Hadi kwenye kidimbwi Cha maji machafu wakaniogesha na matope mwili mzima. Dah sitakaa nisahau.