Barabara ya Morogoro imezibwa

John Kachembeho

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2013
Posts
560
Reaction score
389
Somewhere karibu na Kibaha barabara ya Morogoro imezibwa kwa mawe na wananchi. Sababu kuna mtu amekufa jirani na barabara kama siku tatu zilizopita, taarifa ikatolewa polisi hakuna hatua iliyochukuliwa, sasa wananchi wameziba njia kushinikiza polisi wauondoe mwili wa marehemu!
 
Aisee Tanzania inaelekea wapi?? Watasema wako busy na bunge la katiba ha ha ha!!! Ndiyo maana wajumbe wanazidi idadi tarajiwa. Mpaka nguvu ya umma ifanye kazi ndipo wawajibike. Wangesikia CDM wako na mkutano wangejaa na wa kuazima DSM na Morogoro wangefika kurusha mabomu.
 

siku 3 mwili upo barabarani? Tushapoteza dira na utu vilevile.
 
kwenye matochi wapo kila maficho ya barabara. kwenye huduma wako busy au hawana magari. hawa ndio polisi wetu.
 
Vipi tunaweza ona angalau kidogo tu!! Hata mchoro unatosha
 
Nchi ya watu masikini wa pesa, roho na utu..Badara ya kuchimba kabiuri na kusitiri Mwili wa marehemu mnautizama siku tatu then mnaamua kuandamana ili wengine waje kuwasaidia kuuzika!!..wajinga sana!!
 

jina la hiyo sehemu ni ipi?
 
Nchi ya watu masikini wa pesa, roho na utu..Badara ya kuchimba kabiuri na kusitiri Mwili wa marehemu mnautizama siku tatu then mnaamua kuandamana ili wengine waje kuwasaidia kuuzika!!..wajinga sana!!

Na wewe kha! Yaani mwili uzikwe haijajulikana ni nani, sababu ya kifo, ndugu zake ni nani na wako wapi? Usisahau huyo ni kiumbe ambaye ana ndugu na jamaa. Polisi ni lazima wahusike kwa uchunguzi
 
Nchi ya watu masikini wa pesa, roho na utu..Badara ya kuchimba kabiuri na kusitiri Mwili wa marehemu mnautizama siku tatu then mnaamua kuandamana ili wengine waje kuwasaidia kuuzika!!..wajinga sana!!

Kama chadema wameamua kubaki na mkanda wa mabomu
 
Na wewe kha! Yaani mwili uzikwe haijajulikana ni nani, sababu ya kifo, ndugu zake ni nani na wako wapi? Usisahau huyo ni kiumbe ambaye ana ndugu na jamaa. Polisi ni lazima wahusike kwa uchunguzi

Imagine mwili wa ndugu yako uhukute umelazwa pembeni ya barabara siku tatu huku wenyeji wamekataa kuuzika utajisikiaje?
 

Mkuu KIBAHA ipi hiyo? Maili Moja, Picha ya Ndege? Kwa Mbonde? Kwa Mathias? Tanita? Miembe 7? Msikitini? Kwa Mfipa? Kongowe? Misugusu? Hizo ndio Kibaha the busiest? Huyo mtu kafia wapi?
 
sehemu ni KILUVYA KWA KOMBA, marehemu sio kwamba aligongwa bali inasemakana alitumbukia mtoni yapata siku 3, hata hivyo kwa mujibu wa wanao mfahamu marehemu wanasema alikuwa na tatizo la kifafa. wananchi waliamua kufunga barabara kutokana na maiti kuonekana ikielea kwenye maji tangu jana na hakuna jitihada zozote za zilizofanywa na polisi ili kiiopoa hadi wananchi walipochukua hatua ndipo polisi wapofika na kuiopoa. kwa sasa hali ni shwari magari yanapita kama kawaida
 
Police wetu sijui hata niseme nini. Waweza sema hawakua na gari na bla bla kibao.
 
Zidi kumuomba mungu hii awamu ya nne ipite salama, maana usitarajie lolote katka uwajbikaji sekita zote zimesiziiiii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…