Amkata mke wake

Brigedia Chan-ocha

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2014
Posts
1,353
Reaction score
2,849
Mkazi wa kiseke jijini Mwanza Amemkata Mke wake usiku akiwa amelala kwa sababu ya wivu wa mapenzi, Mume wa Mwanamke huyo aligundua kuwa mke wake ana mahusiano na mwanaume mmoja hapa kiseke, usiku wakiwa wamelala mwanaume aliamka na kuchukua panga na kumkata ambapo damu nyingi zilimtoka mwanaume huyo.

Katika kuonyesha jinsi wanawake walivyo na huruma, mara baada ya polisi kufika na kumkamata mwanaume huyo, mama huyo aliwasihi polisi wamwache mme wake akisema kuwa mambo hayo yatamalizwa na wazazi wa pande zote mbili, polisi waliafiki suala hilo na kumwachia mwanamume huyo.
 
Michepuko haiepukiki!!!pamoja na kampeni zote za dini na watu wa afya
 
kwa hiyo mwanamke kamtetea ili amkate vizuri huruma nyingine majanga
 
Sasa kamkata halafu mwisho wa siku aje amtibie na kuendeea kuishi naye si wehu huo.
 
kamkata nywele??

sema basi hata kwa tafsida bana!!
 
wanansheria wengi wa kitanzania hawajui kucheza na fursa...

jambo kama hili lilikuwa la kuchangamkia mpaka kieleweke...

hapo CV zao zingeongezeka positively..
 
kumbe unaishi mwanza nitakusalimia hapo nikienda rorya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…