Albert Msando: Polepole asihishutumu Serikali Kuhusika na Utekaji, mbona hata yeye aliwahi kutajwa kuhusika na utekaji

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Mkuu wa wilaya ya Ubungo Albert Msando akizungumza kupitia kipindi cha Medani za Siasa cha StarTV kinachoongozwa na Mwandishi wa habari Edwin Odemba ameeleza kuwa Serikali haihusiki na utekaji kama anavyodai aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole

“Serikali haiteki Watu, Polepole asihishutumu serikali kuhusika na utekaji, Mbona hata yeye huko nyuma aliwahi kutajwa kuhusika na utekaji” amesema Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Albert Msando

Soma pia GE2025 - Albert Msando: Ni kweli Ufisadi upo nchini lakini Rais Samia anapambana nao


Your browser is not able to display this video.
 
Kwa hiyo kama yeye aliwahi tajwa ndo asiseme kuhusu Serikali kufanya utekaji?

Huyu jamaa tangu achukuliwe TISS ya voda fasta kaanza kuwa na funza kichwani.
 
"tukae tuzungumze au nitasema" hili ni la kulitazama
 
Hata kama alihusika na utekaji ndo hasikemee utekaji?!
 
Huyu chawa yuko busy kutafuta promotion!
 
Upo wakati unakuja , hata uyu atakua na nafasi ya kusema haya , tufike mda penye hapana tuseme hapana na penye ukweli tuseme ndio , taifa letu sote ndungu zangu, tusifurahi mmoja wetu humizwa hii sio afya kwa nchi.

Kwa kweli na kwa hili mie sikubali na sito kubali bado nafasi ya kuliponya hili taifa ipo asema Bwana
 
Kwani huyu boya ji nani ?? Anajipendrkeza hivii......mbona DC wa Magu Kwimba etc hawasemi ? Haimuhusu akae kimyaaa
 
Alafu mtu kama uyu anachaguliwa mlinzi wa amani wilaya ati , uyu Bwana hivi huwa anajua kuna kesho? kuna kesho wakuu aya manafasi yasiwadanganye hata kidogo ,hata kidogo asema Bwana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…