Ajali Leo tena

monaco

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2012
Posts
2,184
Reaction score
1,779

Katika maeneo baada kidogo ya nangulukulu Km1 hivi,basi likiwa kinatokea nangulukulu kuelekea Dsm lilikutana na Lori lililokuwa kimekaa katikati ya barabara kutoka Dsm kuja nangulukulu,dereva alipotaka kulikwepa akakutana na Lori lingine linakuja upande aliokuwepo,ikabidi arudi pembeni kuepusha ajali ya USO kwa USO,alipokuwa anarusisha gari njia kuu gari ikateleza ikagoma kurudi njia kuu ikateleza Kama linavyoonekana ktk picha!jamani haya malori haya!hakuna mtu aliepoteza Maisha kikubwa abiria wote walikuwa wamefunga Mkanda,mikanda imesaidia sana sana jamani!tulivyofika hapo tukawapa msaada wa kuwapakia baadhi ya abiria!wengine walipelekwa hospitali ya kilwa!
 

Attachments

  • ImageUploadedByJamiiForums1427049455.306501.jpg
    81.3 KB · Views: 1,108

Lori limekaa katikati ya barabara.....alipojaribu kulikwepa akakutana na lori lingine linakuja upande wake! Mkuu chanzo cha ajali waachie wataalamu wa ajali,tunashukuru kwa kutupa taarifa ya ajali!
 
Hii habari yako haijakaa vzr. Tulia halafu uje upya. Bado utakuwa wa kwanza kama nia yako ni hiyo.
 
Basi gani hili........?......ukiwataja wanaweza kujifunza kitu..........
 
Nahisi dereva wa basi alikuwa mwendokasi sana na hakuchukua tahadhari ya kutosha. kwa maelezo hayo inaashiria au nahisi kwamba hilo eneo ni kwenye kona kiasi cha dereva kutoona mbali gari inayokuja mbele yake. Na kama ni eneo la kona alitakiwa awe mwendo mdogo sana jambo ambalo nahisi hakulizingatia. Kama sio kona basi ni mzembe kupindukia. Na kama huu ndio ukweli basi madereva mwtatumaliza, you are so useless and so dangerous animals.
 
Lori limekaa katikati ya barabara.....alipojaribu kulikwepa akakutana na lori lingine linakuja upande wake! Mkuu chanzo cha ajali waachie wataalamu wa ajali,tunashukuru kwa kutupa taarifa ya ajali!

Nilikua na mawazo lakini yamepotea kidogo,mchango wako umenifanya nicheke sana,kweli kiswahili ni kigumu kwa huyo jamaa!
 
...mpaka uchaguzi uishe tutapoteza wengi sana na ivi maccm yana hofu ya ukawa nmmmhh...
 
Ubarikiwe kwa kuujulisha uma habari hii ila tumuombe sana Mungu baba atuepushie haya majanga jamani yanatisha kwani hata maisha yanaendelea kushuka thamani ... Tufanyeje jaman??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…