"Wanasiasa wengi wa upinzani Afrika ni kama watoto wa Kitanzania waliokuwa na ndoto za kuwa madaktari, marubani, wahadisi n.k., hadi walipopewa hesabu ya kidato cha pili, wakaamua bora wauze chipsi."— Alloyce, P.R. 😄
Niko kwenye miaka ya ishirini na kitu sasa. Si kijana mdogo tena, lakini pia si mtu mzima kwa maana ya “kamilika.” Na kuna jambo moja ambalo limekuwa likijitokeza kimya kimya ndani yangu — kama mawimbi yanayopiga ufukwe wa akili bila kupumzika: Je, huu ndio utu uzima tulioahidiwa? Maisha haya ni...