Mwanaharakati Dkt. Wilbroad Slaa amesema moja ya mambo yaliyomsukuma kujiunga kufungua kesi dhidi ya Waziri wa Mambo ya Ndani ni kuwa kutokana na umri wake kama mzee ameona akikaa kimya hatokuwa ametendea haki watoto na wajukuu zake.
Soma: LHRC, TLS, Dk. Slaa wamfungulia Kesi ya Kikatiba Waziri...
Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Benson Kigaila amesema tabia ya serikali kushiriki kuvunja sheria inatakiwa kupingwa na kila Mtanzania anayetaka utawala wa sheria, hadharani na sirini. Haya mambo lazima yapingwe kwa nguvu zote kwani yanahatarisha misingi ya demokrasia...