Hivi aliyeweka hii clip alirekodi mwenyewe au amepewa aitoe humu JF? Napata wasiwasi na uhalali wa hii clip, lakini nadhani kama imerekodiwa na mtoa mada ni vema akawa wa kwanza kuisaidia polisi katika uchunguzi wake huenda naye ni mmojawapo katika mipango hiyo
Tunashukuru kwa taarifa na tunazidi kumwombea kwa Mungu ampe nafuu na apone haraka. Matukio haya yanalenga kuwanyamazisha waandishi wa habari msiripoti mambo muhimu ya maslahi kwa Taifa lakini msirudi nyuma kamwe, tunawaombea na ukweli utasimama daima.
Inasikitisha sana kuona raia wakiuawa ama kuteswa kwa vitu vizito na vyenye ncha kali wakati serikali ikishindana kuunda tume ambazo binafsi sioni umuhimu wake. Nampa pole sana ndugu yetu, Mungu atamponya na majeraha yote ili arudi kuungana na familia yake.
Kimsingi kila chama kina utaratibu wake wa kujieneza, ikiwa unaona utaratibu unaoutoa humu jamvini utakisaidia chama basi ukawape ushauri huo na wewe uwe mstari wa mbele kuonyesha mfano kwani kuwa kiongozi si kutumikiwa bali kutumika na kuonyesha njia.
Hivi mtu akiondoka katika nafasi aliyonayo ndio anaona zaidi makosa ya wenzake ambayo naye ni chanzo! It is very interesting, hizi ndo siasa za Tanzania.
Hivi mtu akiondoka katika nafasi aliyonayo ndio anaona zaidi makosa ya wenzake ambayo naye ni chanzo! It is very interesting, hizi ndo siasa za Tanzania.
Eti hatambui mchango wa mwalimu, hivi na masters uliyonayo unashindwa kujua nyumba inajengwa juu ya msingi. Kwa namna ulivyoandika thread hii ninawasiwasi na elimu yako
Nadhani mtoa tamko ametoa kwa nia njema kuitakia mema nchi yetu, tumevumiliana miaka mingi lakini sasa huyu mdudu wa udini anayetutafuna sijui ameletwa na nani tumuombe Mungu atunusuru na uchochezi wowote wa kidini.
Naona hii huu ni upuuzi kujadili mtu ambaye wakati upo katika chama chake unamsifia na kumkashifu wa chama kingine leo hii umehamia huko unawasifia na kuwaponda ulikotoka huu ni ulimbukeni na kutafuta sympathy kwa watanzania katika mambo binafsi. Huu ndio mfumo wa siasa za Tanzania ambao badala...
Wewe ndio hujadili hoja, pia vibudu umeshakula sana pamoja na kuwa wanachinja waislamu. Labda ishauri serikali yako iweke mabucha ya kwenu msiopenda kula vibudu na wale wanaokula vibudu ili uone raha.
Hivi ndugu unatumia ubongo wako na kuufikirisha kweli au ni ulimbukeni wa kushabikia udini? Hivi siku zote hizi nakula nyama unafikiri nahitaji hiyo yenye udhu au ibada ya mtu mwingine? Kwa mimi binafsi hakuna wa kuniamulia kuwa nyumbani mwako ule nini lakini nilichozungumza au kujadili ni kuwa...
Kwa mtazamo wangu kila mtu aamini kwa imani yake kama anadhani ndio itamuokoa, mimi nina uhakika na imani yangu ndio maana siwezi kng'ang'ania watu wengine waamini kile ninachoamini mimi. Hakuna ibada ambayo ni ya watu wote na ya hadhara kuliko ile ya kutolea dhabihu kwa Mungu hivyo kuchinja...
Soma MT 11:2-6; MT 1:1, LK 2:10-11; LK 9:20-22 utaona injili imemtaja YESU kuwa ndiye kristo na Mwana wa Mungu, wafuasi wake utawaitaje? Si vema kubisha usichokiamini ni sawa nami nikubishie kuhusu Mtume Mohamad S.A.W wakati ni imani yako. Jambo la msingi kwenye suala la imani tuvumiliane na...
Nashangaa watu kung'ang'ania kuchinja badala ya kujadili mambo ya maana, hivi udini unawasaidia nini? Mimi sioni tatizo, mkichinja sisi tunakula lakini hakuna sehemu yoyote ambayo Mungu amehalalisha muislamu au mkristo kuchinja. Kama naandaa kitoweo kwa ajili yangu hakuna mtu wa kuniwekea...
Good analysis, naomba sasa uendelee kumpatia input mbunge wetu ili aweze kutoka na kitu kizuri kwa manufaa yetu endelea kutoa ushauri ili kuboresha hoja ya msingi, hata hivyo ikiwa mh. Nassari anaona comments na ushauri humu basi afanyie kazi ili siku za mbeleni aandae hoja yenye umakini zaidi.
Kimsingi si lazima ukubaliane na kila hoja kutokana na mtazamo wako, lakini ni vema vile vile kuelewa maudhui na dhima ya mtoa mada na au mtoa hoja. Hapa mtoa hoja anasema dhima kuu ni mjadala wa kutafuta ufumbuzi wa changamoto za baraza la mitihani ili kuboresha kiwango cha elimu hapa nchini...
Barubaru,
Mimi ningekushauri kuwa ushauri huu uutoe serikalini ili itekeleze nawe ushuhudie kama hizo hospitali na shule za kikristo zitakufa au zitashamiri na sio kulalamika humu JF wakati hakuna msaada zaidi ya maoni tu, chukua hatua.
Kwa uelewa wangu ni kuwa hata kihistoria wakoloni...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.