Kwa muda nafikiria,fumbuzi sijapatia,
Madhila yanotukia,lini mwisho kufikia,
Huru yakatuachia,mazuri kuyafurahia,
Huwa nawaza ni nani,kumfunga paka kengele.
Kwa siku zinavyosonga,ni mengi yanaibuka,
Tunashindwa kuyapinga,tunazidi kuteseka,
Akili zetu mefunga,na kuwaza tumechoka,
Huwa nawaza ni...