Ziwa Nyasa limeporwa kikamilifu?

S V Surovikin

JF-Expert Member
Aug 8, 2015
13,625
32,751
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Iko hivi, kipindi kulivyoibuka vita ya maneno kati yetu na Malawi niliangalia mpaka wetu na Malawi kupitia picha za satellite nikaona mpaka huo umepita katikati ya ziwa Nyasa.

Siku chache mbeleni nikaangalia tena nikaona mpaka upo pale pale lakini sehemu hiyo/mpaka huo ukiwa umebadilishwa rangi kuwa nyekundu.

Kuchorwa mpaka huo kwa rangi nyekundu ni kuashiria kuna mzozo ambao umoja wa mataifa haujaelewa ni nani hasa mwenye haki na eneo hilo kati ya Tanzania na Malawi.

Tangu 2015 sikuwahi kuchungulia tena eneo hilo, ila leo nimeangalia mpaka huo kupitia camera za satellite nikashtuka baada ya kuona mpaka huo umehamishwa alafu wakabadili na jina la ziwa hilo na kuliita ziwa Malawi 😠

Yaani kwa kifupi lile ziwa hatuna mamlaka nalo tena! Tumeporwa kilomita nyingi sana za mraba huku serikali yetu ikiwa haijui kinachoendelea juu ya ziwa hilo lenye utajiri wa gesi, mafuta na spish za samaki zaidi ya 1500.

Mpaka huo umehamishwa kutoka katikati ya ziwa hadi kwenye fukwe za nchi yetu huku wakibadili kabisa jina la ziwa letu na kuliita ziwa Malawi kama inavyoonekana kwenye picha.

Screenshot_20210601-142529.png


Linganisha na mpaka ambao tuliachiwa na wakoloni katika picha hii.

_92848451_50f57301-de12-4a3f-a678-37a0449e7e19.jpg


Ikumbukwe kwamba miaka michache kipindi cha serikali ya Jakaya kikwete tulikuwa na mzozo Malawi kuhusiana na hili ziwa hadi kukatokea vitisho vya kuingia vitani kila nchi ikidai italinda mpaka wake. Malawi wakidai ziwa lote ni lao huku Tanzania tukidai mpaka wa wakoloni ambao ulipita ndani ya ziwa huku sisi tukiwa na eneo lenye upana zaidi ya Malawi.

Hii maana yake nini? Sisi ni wapole sana au hatupo tayari kulinda mipaka yetu?

Kwanini wazungu wameridhia kumega nchi yetu na kuikabidhi Malawi?

Naomba serikali yetu tukufu itoe maelezo kuhusu hili jambo maana sio dogo.

Tukiendelea kunyamaza kuna siku watasema mkoa wa Mbeya ni wao
 
Hao maaskari wanaolindaga mipaka walikuwa wapi hadi wamalawi wahamishe mipaka?

Inamaana hamna wanajeshi kabisa kwenye hilo ziwa!? Kama ni hivyo, basi hatuko salama!!
Mkuu achana na wanajeshi wanaolinda mpaka maana unaweza kuta wapo lakini Malawi inapambana kimyakimya kwenye mashirika ya kimataifa ili ionekane ina haki zaidi siku wakiamua kuwatimua wanajeshi wetu/kama wapo ipate uungwaji mkono wa kimataifa.

Wewe huoni mabeberu wanaoamua mipaka ya kimataifa wameshachora mpaka mpya kuipendelea Malawi?
 
Mbona mimi last December nilipoenda likizo, nilitembelea mpaka Matema beach ambako tuliogelea, tukapanda kwenye boti ya mota na kuanza kuzunguka kuingia ndani km nyingi tu lkn hakuna aliye tubugudhi. Inawezekana hiyo ni mipaka ya kwenye makaratasi tu.

Hakuna nyaraka yoyote ya kisheria ambayo imempa mamlaka Malawi ya kumiliki ziwa lote upande wa Tanzania na nusu upande wa Msumbiji.
 
Mbona mimi last december nilipoenda likizo, nilitembelea mpaka matema beach ambako tuliogelea, tukapanda kwenye boti ya mota na kuanza kuzunguka kuingia ndani km nyingi tu lkn hakuna aliye tubugudhi. Inawezekana hiyo ni mipaka ya kwenye makaratasi tu. hakuna nyaraka yoyote ya kisheria ambayo imempa mamlaka malawi ya kumiliki ziwa lote upande wa Tanzania na nusu upande wa msumbiji.
Mambo ni mdogomdogo mkuu. Kama ramani imebadilishwa kuna siku ya tutapigwa marufuku.

Jirani akimega kiwanja chako usipomchukulia hatua kali, atavunga jamii ikishazoea kwamba eneo alilomega ni lake ndipo anakuja kuweka uzio.
 
Wamalawi wanajidanganya
Huwezi kudai maji yaliyopakana na vijiji vya nchi nyingine kuwa wakienda kuchota maji kwenye ziwa hilo basi wako nchi jirani.
Hatuwezi kukubali ujinga huo!

Ila ubaya wa hii kitu, mabeberu wanaweza kuitumia kutublackmail ili tuwape concensions kadha wa kadha la sivyo watambue kuwa ziwa lote ni mali ya Malawi
 
Mbona mimi last december nilipoenda likizo, nilitembelea mpaka matema beach ambako tuliogelea, tukapanda kwenye boti ya mota na kuanza kuzunguka kuingia ndani km nyingi tu lkn hakuna aliye tubugudhi. Inawezekana hiyo ni mipaka ya kwenye makaratasi tu. hakuna nyaraka yoyote ya kisheria ambayo imempa mamlaka malawi ya kumiliki ziwa lote upande wa Tanzania na nusu upande wa msumbiji.
Uko sahihi,au inawezekana anachokoza tu kutaka kuona tutafanya Nini??.
 
Back
Top Bottom