babykailama
JF-Expert Member
- Mar 5, 2012
- 251
- 243
Zitto vs Muhongo; nani ni Political Stunt Engineer
1.Muhongo anajulikana ni mwanachama wa CCM, Zitto ni CHADEMA (kwa utambulisho wa kadi na gwanda) na ni CCM (kwa maisha yake)
2. Muda mfupi, Muhongo alipoingia tu akaona uozo wa Muhando na Mafisadi huko TANESCO na akasema Mkurugenzi akae pembeni kupisha uchunguzi kamili; Zitto kakaa Bungeni muda wote na akiwa mwenyekiti wa POAC hajawahi kusema kuwa kuna migao ya umeme isiyo ya lazima wala kupiga kelele juu ya mateso na uhujumu unaofanywa na wenye majenereta dhidi ya TANESCO na Taifa letu. Na kusimamishwa kwa Muhando kunamkosesha usingizi Zitto hadi kesho!
3. Muhongo anasema Bodi mpya ya TPDC ifanye kazi yake barabara ikiwa ni pamoja na kupitia mikataba yote na kutoa mapendekezo yao tayari kwa hatua zinazopaswa kufuatwa kwa mujibu wa sheria. Zitto hataki anabaki kusema tu mikataba iwekwe wazi, wapi na bila kusema baada ya kuwekwa wazi nini kitafanyika.
4. Zitto anasema Bodi (tena mpya ) ya TPDC ni wale wale hivyo hawana moral authority kupitia mikataba hiyo; lakini hasemi Bunge (hilo hilo akiwemo yeye) la zamani hawana moral authority kupitia nyongeza za marekebisho ya Sheria ya Mafao waliyoyapitisha wao au mambo mengi tu ambayo wameyapitisha au kuyajadili na kuyasema karibu kila mwaka.
5. Zitto aliwahi sema aliingia Siasa kwa bahati mbaya, na akaueleza umma yuko njiani kuacha siasa aende kusoma. Hakuacha siasa tena badala yake tumemwona akifanya hata siasa chafu kiasi cha kuwachukuwa wenzake wa CHADEMA na kuwapeleka kwenye Leka Dutigite kwa kisingizio cha kuwanyanyua Wasanii kisha kuwacha njia panda waonekane kuwa wao wamemwandaa yeye kugombea Urais ili alete mtafaruku CHADEMA na alifikia hatua ya kusema hapa kuwa analiamini gazeti kuliko maneno ya wenzake akina Mh. Halima Mdee.
6. Tumemsikia Dkt. Muhongo kila mara akiueleza umma hapa Chuo Kikuu Mlimani na katika makongamano ya wasomi akizungumzia na kupigania kwa vitendo umuhimu wa elimu hasa tafiti, matumizi ya sayansi, teknolojia na ubunifu kwa nchi yetu na Bara la Afrika hadi ulimwengu ukamtambua akawa wa kwanza kupata tuzo ya Mwingereza, Prof. Robert Shackleton (the Robert Shackleton award), akifanya tafiti hadi Wasomi wa Kitanzania wakamkubali na kumpa tuzo ya Kitaifa ya Utafiti Bora (The Tanzanian National Award for Outstanding Research in Science & Technology toka COSTECH), akileta michango ya nguvu kusimamia elimu bora na mchango katika tasnia ya uchimbaji madini hadi dunia ya Wasomi wa Kifaransa wakasimama na kumvika nishani ya Emperor Napoleon na kupewa ngazi ya Ordre des Palmes Académiques. Wengi tunamfahamu si tu kama Msomi bali mbunifu na mpigania haki za Mwafrika kufikia kuasisi na kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa kwanza wa Shirika la Kimataifa la Sayansi Afrika (ICSU) (Latest news: Regional Office for Africa — ICSU) Afrika ya kusini.
7. Tumemwona Zitto anaamka asubuhi na kukimbilia media na kutembeza karatasi ya kutafuta saini za kutosha eti kupiga kura ya kutokuwa na matumaini kwa Waziri Mkuu endapo Mawaziri (wahusika) hawatabadilishwa; akisha pata hizo saini hajawahi kurudi kwa Wabunge wala Wananchi kuwaeleza alichokuwa anakitafuta na kimepatikanaje sasa maana Mawaziri wapya tena wenye mashiko ndio hawa akina Muhongo hawataki na anawapiga vita bila sababu.
Ninyi mtaamua ni nani flip- floper na Mhadisi wa kutaka misifa (Political Stunt Engineer) kati ya Dr. Muhongo, Officier, Ordre des Palmes Academiques na Bwana Zitto, Leka Dutigite .
1.Muhongo anajulikana ni mwanachama wa CCM, Zitto ni CHADEMA (kwa utambulisho wa kadi na gwanda) na ni CCM (kwa maisha yake)
2. Muda mfupi, Muhongo alipoingia tu akaona uozo wa Muhando na Mafisadi huko TANESCO na akasema Mkurugenzi akae pembeni kupisha uchunguzi kamili; Zitto kakaa Bungeni muda wote na akiwa mwenyekiti wa POAC hajawahi kusema kuwa kuna migao ya umeme isiyo ya lazima wala kupiga kelele juu ya mateso na uhujumu unaofanywa na wenye majenereta dhidi ya TANESCO na Taifa letu. Na kusimamishwa kwa Muhando kunamkosesha usingizi Zitto hadi kesho!
3. Muhongo anasema Bodi mpya ya TPDC ifanye kazi yake barabara ikiwa ni pamoja na kupitia mikataba yote na kutoa mapendekezo yao tayari kwa hatua zinazopaswa kufuatwa kwa mujibu wa sheria. Zitto hataki anabaki kusema tu mikataba iwekwe wazi, wapi na bila kusema baada ya kuwekwa wazi nini kitafanyika.
4. Zitto anasema Bodi (tena mpya ) ya TPDC ni wale wale hivyo hawana moral authority kupitia mikataba hiyo; lakini hasemi Bunge (hilo hilo akiwemo yeye) la zamani hawana moral authority kupitia nyongeza za marekebisho ya Sheria ya Mafao waliyoyapitisha wao au mambo mengi tu ambayo wameyapitisha au kuyajadili na kuyasema karibu kila mwaka.
5. Zitto aliwahi sema aliingia Siasa kwa bahati mbaya, na akaueleza umma yuko njiani kuacha siasa aende kusoma. Hakuacha siasa tena badala yake tumemwona akifanya hata siasa chafu kiasi cha kuwachukuwa wenzake wa CHADEMA na kuwapeleka kwenye Leka Dutigite kwa kisingizio cha kuwanyanyua Wasanii kisha kuwacha njia panda waonekane kuwa wao wamemwandaa yeye kugombea Urais ili alete mtafaruku CHADEMA na alifikia hatua ya kusema hapa kuwa analiamini gazeti kuliko maneno ya wenzake akina Mh. Halima Mdee.
6. Tumemsikia Dkt. Muhongo kila mara akiueleza umma hapa Chuo Kikuu Mlimani na katika makongamano ya wasomi akizungumzia na kupigania kwa vitendo umuhimu wa elimu hasa tafiti, matumizi ya sayansi, teknolojia na ubunifu kwa nchi yetu na Bara la Afrika hadi ulimwengu ukamtambua akawa wa kwanza kupata tuzo ya Mwingereza, Prof. Robert Shackleton (the Robert Shackleton award), akifanya tafiti hadi Wasomi wa Kitanzania wakamkubali na kumpa tuzo ya Kitaifa ya Utafiti Bora (The Tanzanian National Award for Outstanding Research in Science & Technology toka COSTECH), akileta michango ya nguvu kusimamia elimu bora na mchango katika tasnia ya uchimbaji madini hadi dunia ya Wasomi wa Kifaransa wakasimama na kumvika nishani ya Emperor Napoleon na kupewa ngazi ya Ordre des Palmes Académiques. Wengi tunamfahamu si tu kama Msomi bali mbunifu na mpigania haki za Mwafrika kufikia kuasisi na kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa kwanza wa Shirika la Kimataifa la Sayansi Afrika (ICSU) (Latest news: Regional Office for Africa — ICSU) Afrika ya kusini.
7. Tumemwona Zitto anaamka asubuhi na kukimbilia media na kutembeza karatasi ya kutafuta saini za kutosha eti kupiga kura ya kutokuwa na matumaini kwa Waziri Mkuu endapo Mawaziri (wahusika) hawatabadilishwa; akisha pata hizo saini hajawahi kurudi kwa Wabunge wala Wananchi kuwaeleza alichokuwa anakitafuta na kimepatikanaje sasa maana Mawaziri wapya tena wenye mashiko ndio hawa akina Muhongo hawataki na anawapiga vita bila sababu.
Ninyi mtaamua ni nani flip- floper na Mhadisi wa kutaka misifa (Political Stunt Engineer) kati ya Dr. Muhongo, Officier, Ordre des Palmes Academiques na Bwana Zitto, Leka Dutigite .