Anfaal
JF-Expert Member
- Jan 19, 2010
- 1,154
- 113
vyombo vya habari hivi karibuni vimekunukuu ukishauri kuwa, Tanesco iachane na uzalishaji wa umeme na suala hilo wapewe makampuni ya umma ambayo kwa mujibu wako unaamini yanauwezo wa kufanya hivyo (gazeti la Tanzania Daima).
Nina hakika katika hili ulimaanisha mifuko ya pensheni maana haya ndiyo yamekuwa kimbilio la kila uwekezaji na ndio hasa yanayoonekana kuwa yana faida licha ya ukweli kwamba uwepo wao hutegemea fedha za wananchi.
Lakini utofauti wangu na wewe umelenga katika maeneo makuu mawili. Mosi, unashau kuwa ufanisi wa mashirika ya umma ni wa kutia mashaka km ilivyo tanesco kwahiyo kinachofanyika ni kuhamisha matatizo kutoka shirika moja kwenda jingine na si kutatua kabisa. Pia km utakumbuka ni hivi karibuni suala la usimamizi wa mifuko hii ndio lilijadiliwa na mifuko hii bado inaonekana inaloop holes nyingi saana za kifisadi, hivi kushauri uwekezaji ufanyike na mifuko hii, huamini kuwa ni sawa na kuidhinisha michango ya wafanyakazi itafunwe yote licha ya kuwa tayari michwa inaitafuna?
Pili, kuhimiza uwekezaji wa kutumia sekta za umma ni kuupuza uwepo wa sekta binafsi ambazo zenyewe huheshimika zaidi katika kusimamia biashara na ujenzi wa uchumi. Hivi kushauri huko ulikosema, huoni kuwa ni muendelezo wa unfair play kwenye sekta za biashara kwa kuzibana kabisa sekta binafsi ambazo ndio injini za maendeleo?
Nina hakika katika hili ulimaanisha mifuko ya pensheni maana haya ndiyo yamekuwa kimbilio la kila uwekezaji na ndio hasa yanayoonekana kuwa yana faida licha ya ukweli kwamba uwepo wao hutegemea fedha za wananchi.
Lakini utofauti wangu na wewe umelenga katika maeneo makuu mawili. Mosi, unashau kuwa ufanisi wa mashirika ya umma ni wa kutia mashaka km ilivyo tanesco kwahiyo kinachofanyika ni kuhamisha matatizo kutoka shirika moja kwenda jingine na si kutatua kabisa. Pia km utakumbuka ni hivi karibuni suala la usimamizi wa mifuko hii ndio lilijadiliwa na mifuko hii bado inaonekana inaloop holes nyingi saana za kifisadi, hivi kushauri uwekezaji ufanyike na mifuko hii, huamini kuwa ni sawa na kuidhinisha michango ya wafanyakazi itafunwe yote licha ya kuwa tayari michwa inaitafuna?
Pili, kuhimiza uwekezaji wa kutumia sekta za umma ni kuupuza uwepo wa sekta binafsi ambazo zenyewe huheshimika zaidi katika kusimamia biashara na ujenzi wa uchumi. Hivi kushauri huko ulikosema, huoni kuwa ni muendelezo wa unfair play kwenye sekta za biashara kwa kuzibana kabisa sekta binafsi ambazo ndio injini za maendeleo?