Zitto ni Mzalendo wa kweli, Baada ya kumsikiliza leo, nimebaini haya...

sCOTLAND WILL NEVER LEAVE THE uk! mARK MY WORDS .... NA NIMESEMA HAYA LEO. iKIWA TOFAUTI i will send 500,000/- kwenye mfuko wowote ambao utautaka (NGO,curch ..etc)

Ninaweza kukueleza sababu ... but that will take long. Holla at me if you want us to "Discuss" Scotland.

oKAY MY APOLOGIES ...

This is an offer (subject to condition precedence
Kobello,
Kwa hili:
Rusha hiyo laki tano Tigo pesa tukawape NGO ya kina mama wajane "mwawode" pale mwananyamala, Nitakupa namba after the outcome of the referendum.
Sent from my iPhone using JamiiForums
This is an acceptance, hivyo hii sass ni agreement, ikisainiwa ni contract!
I will be a witness to this manna hizi betting za humu jf, kuna watu hawachelewi kuhamisha magoli!

No problem. Ila TIGO pesa,sidhani kama nitaweza kuitumia. Moneygram au Western Union ...?
Hii mode haina tatizo, mode yoyote tuu inaweza kutumika, muhimu ni subject mater tuu iwafikie walengwa.

Nitashauri uongeze hapo kidogo kwa kuichangia jf as a causative agent wa this deal, na pia ndio negotiation zilipofanyikia na ndio place of contract!, has to be paid some fees!.

Thanks.

Pasco
 
Mkuu kuna kitu gani hapo kilichokushinda kuelewa? Niliwauliza mambo gani sii ya Muungano ili nipate kujua wao wana yapi yaloachiwa kikatiba, sikujibiwa mkanizungusha weee japo nilikuwa kweli siyajui. Sasa nimetumia njia nyingine nipate kujua bado mnazunguka na majibu ya kihuni huni tu. Kila siku nipo hapa kujifunza na sio kubishana kila siku. nambieni mambo waloachiwa wao kutokuwa ya Muungano halafu ndio nitajua hayo mambo ili nami kesho nijenge hoja zangu. Mimi sio mwelewa wa kila kitu nataka kujifunza pia

NB: Naijua maana ya fiscal autonomy lakini sijui ni mambo gani yapo chini ya mamlaka ya Zanzibar kikatiba, kwani kosa?
Mkuu,

Fiscal autonomy Zanzibar wanayo. Hata serikali za mitaa zinayo. Monetary (policy) autonomy, Zanzibar haina kwa sababu ipo chini ya Muungano.
 
Nitashauri uongeze hapo kidogo kwa kuichangia jf as a causative agent wa this deal, na pia ndio negotiation zilipofanyikia na ndio place of contract!, has to be paid some fees!.

Thanks.

Pasco
Out of 500,000 or on top of 500,000?
 
Fiscal autonomy ya JMT inatgemea unaongelea kulinganisha na nini. Huwezi kuwa na fiscal autonomy ukiwa na mshirika mmoja mwenye fiscal autonomy seperate. Kwamba znz wana uwezo wa kuamua yao, halafu warudi Tanzania na kuamua ya Tanzania, bado tuna fiscal autonomy? May be as compared to Kenya au Uganda, siyo within our own system.
Kila serikali ina fiscal autonomy. Hata serikali ya kijiji.


Wazanzibar wanapolalamika (waziri wao) kuwa Mkukuta umewaacha pembeni hiyo ina maana gani.
Znz wanapotengewa fungu la mkukuta hiyo inaeleza nini. Kama hakukuwa na ugomvi, hayo yanatokeaje.
Fungu lipi la MKUKUTA? Unaongea vitu gani?

Mafuta na gesi inawaathiri wapi hadi waje kujadili Dodoma.
Tanzania inaagiza mafuta na kodi za customs zipo chini ya serikali kuu. Foreign currency movement kwenye kuagiza petroleum, Bulk importation under EWURA ime- include Zanzibar, levy ya vitu kama kerosene na Argas, zina-include customs (under union) ... etc, etc...
Bandari za Tanganyika zinawagusa wapi kimaisha hadi waje kujadili Dodoma
Explosive Act, 1963, Ufanisi wa Bandari unaimarisha external trade na popote pale fedha ya kigeni inapotumika lazima Benki kuu iwe involved. Bandari ni mpaka, usalama wake upo chini ya muungano.

TBS, NECTA, wizara ya afya,elimu,kilimo, miundo mbinu n.k. zinawaathiri vipi hadi waje kulala Dodoma
Wanakuja kujadili kwa sababu zipi, na zinawagusa vipi.
TBS-Industrial lincencing , jambo la muungano.
NECTA - Mbona ina uwezo wa kufuta matokeo Zanzibar??

Pili, kinachochukiza kuhusu watalii ni kuwa wanakuja kutetea masilahi na fiscal autonomy ya zanzibar.
Wanalipwa na JMT ambayo wao hawana mchango( Ben Ndulu, katibu mkuu fedha JMT na SMZ)
Hapa inakuwaje mkuu, hebu tueleze, wao wametumwa na znz, vipi ''Mtanzania bara'' awagharamie.
Wana uhalali upi wa kujadili ya 'Tanzania bara'' to be polically correct, na tunawezaje kuwaweka pembeni wakati tunajadili yetu

Tatu, wanakuja kujadili bandari kwa mfano, ili iweje.
Kumbuka wao wana kila kitu chao kinachohusu bandari kuanzia bajeti, uwakilishia, sheria n.k.
Huku Tanganyika wanakuja kujadili nini?
Kila mbunge anaangalia maslahi ya jimbo lake.
 
Mchambuzi
Hebu fanya ustaarab mpatie Kobello data anazohitaji kwa mtafiti kama wewe hizi in data ndogo sana. Wapambe wanataka kukuokoa wanadai uzi uondolewe, yaani unashindwa hata na Mrisho Gambo (huwa anatupa data), kamanda fanya kweli, Mkuu Pasco naomba uulinde huu uzi ili tuache kurudiarudia maneno acha tupate hitimisho
 
Last edited by a moderator:
Kobello;10626357]Sasa hapo nikujibu vipi?
Hakuna Tanganyika. Once ukikubali hilo, tunaweza kujadiliana kihoja zaidi na siyo kiimani. Ni sawa na kujadili fizikia wakati mtu mwingine analeta mambo ya Mungu. Hakuna Tanganyika, hivyo mambo ya muungano yanakabiliwa na serikali ya muungano, na mambo yasiyo ya muungano yanakabiliwa na serikali hiyohiyo ya muungano.
Nguruvi3: Unaweza vipi ku-address malalamiko ya znz kuwa Tanganyika imevaa koti la Tanzania.
Mambo yasiyo ya muungano ni yapi ikiwa umeshasema hkuna Tanganyika kuna Tanzania.
Sasa kama ipo Tanzania hayo yasiyo ya muungano ni ya eneo gani tusilo lijua.
Hili swali umekimbia, kwa maana ya kuwa huna jibu.

Nimesoma majibu yako hapo chini, nisingependa ujibu kwasababu hujui unaongelea nini.
Kama huwezi ku-address lalamiko namba moja la wazanzibar kuhusu Tanganyika kuvaa koti kama ilivyo katika nukuu, I can say with certain unaandika tu,hukumbuki unaandika nini.

Nimekusamehe usijibu kabisa, wanajamvi watasoma na kuamua vichwani mwao
Kobello;10628883]Kila serikali ina fiscal autonomy. Hata serikali ya kijiji.
Ok, hiyo ya ''Tanzania bara'' unayosema ambayo ipo ndani ya muungano, fiscal autonomy yake ipo wapi na kwa kutumia nini na njia zipi.
Fungu lipi la MKUKUTA? Unaongea vitu gani?
Kwani mkukuta ni maneno tu!
Tanzania inaagiza mafuta na kodi za customs zipo chini ya serikali kuu.

Foreign currency movement kwenye kuagiza petroleum, Bulk importation under EWURA ime- include Zanzibar, levy ya vitu kama kerosene na Argas, zina-include customs (under union) ... etc, etc...
Sijui unafaulu vipi mitihani kama huelewi swali.

Swali ni hili, hao watalii kutoka zanzibar wanapokuja Dodoma kujadili gesi na mafuta ya Mtwara n.k. wakati wao wameshaondoa katika muungano, hayo ya Tanganyika yanawagusa vipi kimaisha kama ulivyosema?

Hakuna mahali nimezungumzia kuagiza mafuta! Nadhani unakwepa hoja, teh teh teh, ujanja uliozeeka kweli kweli.
Kama huna jibu unasepa tu kama ulivyokimbia maswali mengine, teh teh, mkuu wewe unaishi Marekani bwana!
Explosive Act, 1963, Ufanisi wa Bandari unaimarisha external trade na popote pale fedha ya kigeni inapotumika lazima Benki kuu iwe involved. Bandari ni mpaka, usalama wake upo chini ya muungano.
Kama bandari ni usalama, na nakubaliana nawe 100%, Zanzibar wameondoa katika mambo ya muungano. Wanazo bandari zao.

Huo usalama ni wa Tanganyika peke yake? Kama ni wa Tanzania, iweje wazanzibar waondoe katika muungano na bado tubaki tukiwa na Tanzania.

Kama ni mpaka, mpaka upi tena maana kuna miwili, wa Tanzania na znz.
Mkuu unaona jinsi hoja zinavyokuchanganya. Wewe ni wa majuu mkuu, watu wana set bar too high juu yako!
TBS-Industrial lincencing , jambo la muungano.
Wazanzibar wana ZBS ambayo ina standard zake. Hizi za TBS ni za muungano, sasa sijui muungano ni Tanganyika. Tufungue macho mkuu, upo kwa Obama.
NECTA - Mbona ina uwezo wa kufuta matokeo Zanzibar??
Ndio maana ninasema wewe upo oudated.
NECTA haina uwezo wa kufuta matokeo. Hayo yalitokea siku za nyuma.

Sasa hivi wana baraza lao la mitihani na si NECTA.

Wanafunzi wao hawatahiniwi na NECTA, mkuu hizi ni very basic information, sasa kama huzijui unaongelea muungano gani?

Nadhani std yako ni ya juu sana labda uongelee Scotaland maana mambo ya tz huna ufahamu hata wa bahati mbaya.
 
NECTA haina uwezo wa kufuta matokeo. Hayo yalitokea siku za nyuma.

Sasa hivi wana baraza lao la mitihani na si NECTA.

Wanafunzi wao hawatahiniwi na NECTA, mkuu hizi ni very basic information, sasa kama huzijui unaongelea muungano gani?

Nadhani std yako ni ya juu sana labda uongelee Scotaland maana mambo ya tz huna ufahamu hata wa bahati mbaya.
May be cos you seem to be too shallow.
Kwa kuanza hebu nipe jina la hiyo "NECTA" ya Zanzibar.

Lazima nitakurudia .... tuanz na hilo kwanza
 
did you get the message? I don't have time to review my post; if you didn`t get my point please let me know I will clarify; honestly did you consider VETA?? Getting some education will make you achieve something positive in your life. I am doing good not because my father was rich or was some kind of fisadi; not at all; he was just mkulima who valued education; I am wiling to share with you my story so at least you can change your life. We live in different world don't ever expect that government will make you live good; you need to work your ways around; I am showing you the way please follow and in case you find hardship in box me. Don`t waste your time neither CCM nor UKAWA will change your life they all sing the same song different tune; kamanda focus in well being of you and your family. And next time when you correct me please drop a line English.
I am not ready to share any of you nasty and stupid stories about you hopeless life. After all, you are among the hoodlums who loiter in American streets pretending to have achieved economically while not.
 
I am not ready to share any of you nasty and stupid stories about you hopeless life. After all, you are among the hoodlums who loiter in American streets pretending to have achieved economically while not.

Kamanda don't be naive; calm down! I work my way up; I have nothing to pretend , what do I get if I do?? NOTHING! wow! I am impressed at least you showed me something; lets get back to basic did you go to Chang'ombe VETA?? I am waiting, my offer still open; don't worry about me; I live better than you; no question about that; what I do is trying to open the way so somehow you can live your dream; again don't be ashamed God told me something about you; you need help follow the lead!
 
Nguruvi3
Kamanda Usiharibu mjadala mwache Mchambuzi alete data zake kaa pembeni kidogo hii zenu ni mbinu mnazozitumia kurudia maneno ni kupindisha hoja ili kukwepesha ukweli Kobello anasubiri za Mchambuzi kama unazo data zilizoombwa na Kobello usisite mpe mtafiti wa UNESCO azipitie ili atoe majibu muafaka
 
Last edited by a moderator:
Kamanda don't be naive; calm down! I work my way up; I have nothing to pretend , what do I get if I do?? NOTHING! wow! I am impressed at least you showed me something; lets get back to basic did you go to Chang'ombe VETA?? I am waiting, my offer still open; don't worry about me; I live better than you; no question about that; what I do is trying to open the way so somehow you can live your dream; again don't be ashamed God told me something about you; you need help follow the lead!
You are good for nothing! please distance yourself from this discussion as it is above your little brain.
 
You are good for nothing! please distance yourself from this discussion as it is above your little brain.

Believe me; there is nothing above me on this forum; I can read; research and analyse; I am competent the only thing troubling me is vilaza like you that why I am encouraging you to go to VETA probably when you come back you will be in different level!
 
Mchambuzi
Hebu fanya ustaarab mpatie Kobello data anazohitaji kwa mtafiti kama wewe hizi in data ndogo sana. Wapambe wanataka kukuokoa wanadai uzi uondolewe, yaani unashindwa hata na Mrisho Gambo (huwa anatupa data), kamanda fanya kweli, Mkuu Pasco naomba uulinde huu uzi ili tuache kurudiarudia maneno acha tupate hitimisho

Data za gharama za serikali Mbili sio? Kama ni hizo, Zipo njiani, lakini sio kwenye Uzi huu, nakuja na Uzi mpya; I need a few days; I am working on the data, Tayari theoretical framework,variables, na units of analysis Zimekaa sawa; Uzi huu sio wa kukurupuka, sio Uzi wa kisiasa, vuta Subira, unaiva jikoni;

Tutaona mtatokea wapi;

Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Kobello,
Katika majibu yako kwa Mkandara hapo juu Kwamba Zanzibar has fiscal autonomy, nakubaliana na wewe; nadhani umekiri Hilo sio kwa kubahatisha Bali kwa kuelewa maana ya fiscal autonomy, tofauti na mkandara ambae Amekwepa kufafanua uelewa wake juu ya fiscal autonomy; kwa maana nyingine anakataa Kwamba Zanzibar haina fiscal autonomy, akiulizwa afafanue, anaanza Kupiga chenga;

Lakini Katika majibu ya hoja yako kwa Nguruvi3 hapo juu, umesema Kama hata serikali ya kijiji Ina fiscal autonomy, do you mind to elaborate zaidi juu ya Hili tukuelewe vyema zaidi?


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Hivi Zitto hana kitu cha thamani kinachoweza mwinua zaidi ya kujisifia mwenyewe ,kwa kumezesha watu uozo wake?
 
Kobello,

Huko juu tulikubaliana Kwamba MKUZA sio suala la muungano kwani Katika mkataba wa muungano, suala la kupunguza umaskini halipo. Ukahitimisha Kwamba kwahiyo serikali ya Zanzibar Ina Haki ya kuwa na MKUZA nje ya muungano. Kwa maana hii, umekubali au umehalalisha yaliyomo kwenye mkataba wa muungano, Jambo ambalo Huko nyuma ulikuwa unasua sua. Hilo moja.

Pili, unapingana na hoja yetu juu ya uwepo wa rasimu ya mafichoni ya CCM, Huku umma ukiona wazi Kwamba kinachojadiliwa Dodoma sio Kile walichopendekeza kwa tume ya warioba. Chini ya serikali Mbili zinazoboreshwa na Sitta, CCM na wapambe wao pale Dodoma, kupitia rasimu Yao ya mafichoni, wameongeza mambo Mapya kuwa ya muungano, mambo ambayo awali hayakuwepo, lakini pia Kinyume mapendekezo ndani ya rasimu tume ya katiba; mambo Mapya ya muungano kwa Mujibu wa rasimu ya CCM ya mafichoni sasa ni pamoja na serikali za Mitaa (kumbuka Ulisema hata znZ wanazo Kama suala nje ya muungano!), ardhi, uvuvi, ufugaji n.k; yote haya hayapaswi kuwa sehemu ya muungano kwa Mujibu wa mkataba wa muungano ambao ulioutumia hapo juu Kama sehemu ya utetezi wako wa Hoja zako; lakini hata kwa Mujibu wa katiba ya JMT [1977], masuala haya hayatajwi kuwa ni ya muungano. Swali langu kwako:

•Kwanini Hali hii inajitokeza na kwanini turuhusu Hali hii Wakati ni wazi Kwamba serikali ya muungano haihusiki na serikali za Mitaa, ardhi, uvuvi na ufugaji upande wa Zanzibar?

Tatu, Unatetea Mfumo wa sasa wa serikali Mbili, lakini hapo hapo unakiri Kwamba suala la poverty Alleviation ni suala la nchi washirika, sio suala la muungano. Tungependa utueleze, je:

•Masuala ambaya ni nje ya yale ya muungano, Kama Hil la maendeleo ya kiuchumi (economic development) yatasimamiwa na serikali gani chini ya Mfumo wenu wa serikali Mbili zilizoboreshwa?

Chini ya Mfumo wa serikali Mbili, haiwezekani kuundwa Chombo kitakachosimamia mambo yasiyo ya muungano; tumeshaona majanga ya tume ya pamoja ya fedha ambayo imekwama kwa sababu fiscal autonomy ya mshirika mwingine wa muungano (Tanganyika) haijatenganishwa na fiscal autonomy ya muungano/Tanzania, licha ya TRA kusaidia tume Katika uchambuzi na kutofautisha Mapato ya muungano, Tanganyika na Zanzibar.

Katika muundo wa serikali Mbili zilizoboreshwa, kila suala ambalo halihusiani na Zanzibar litabakia kuwa ni Jambo la muungano. Hii kwa sababu katiba ya JMT [1977] Inasema wazi Kwamba "serikali ya muungano Ina mamlaka ya kusimamia mambo ya muungano na mambo yasiyokuwa ya muungano kwa upande wa Tanzania bara aka Tanganyika. Kwa maana hii, chini ya Mfumo wenu wa serikali Mbili zilizoboreshwa, serikali ya muungano itaendelea kushughulika na maendeleo ya uchumi, Kilimo, afya, maji, nishati, madini, ujenzi, uchukuzi, maliasili na utalii, mambo ambayo ni ya Tanzania bara (Tanganyika) lakini kwa kofia ya muungano. Upo hapo?

Hata Kama "CCM" itaamua Kama ilivyopanga kuruhusu Zanzibar kukopa nje kwa ajili ya kusimamia shughuli zake za maendeleo, chini ya serikali Mbili zilizoboreshwa, utekelezaji wake bado utaleta matatizo mengi sana ikiwa ni pamoja na mtanganyika kuzidi kukamuliwa kodi zake kumtumikia mzanzibari with nothing in return.

Nne, Tunaelezwa Kwamba ulipaji kodi ni "uzalendo". Swali linalofuata ni je:

• kwanini mwananchi wa ruvuma kulipa kodi za kumbeba mzanzibari iwe ni kitendo cha uzalendo kwa "Tanzania" Wakati mwananchi wa Zanzibar, kodi anayolipa ni uzalendo kwa "Zanzibar" pekee?

•huu muungano mliodhamiria wa kujenga muungano wenye uzalendo kwa mataifa mawili ya Zanzibar na Tanzania?

Mapato yote ya ZRA na Yale ya TRA kwa upande wa Zanzibar hayavuki Bahari, lakini ya mkazi wa ruvuma - Yale yote ya TRA pamoja na local government authorities (suala ambalo sio la muungano) Kama vile ushuru wa manispaa ya songea, haya yanawekwa kwenye kapu moja la hazina chini ya saada mkuya na kina mwigulu, na kuvushwa Bahari kwenda Zanzibar with nothing in return, zaidi ya hoja za kisiasa Kwamba huo Ndio utaifa wa "Tanzania" tunaojivunia.

Wakuu wangu, inawezekana ulipaji kodi ukawa ni uzalendo lakini walipa kodi wa Tanganyika wana Haki ya kujua kodi zao zinatumikaje na kwa faida gani. Kwa mfano, Mapato makubwa kuliko yote ya kodi ni Corporate income and personal income tax, tumeshajadili hili, hasa Kwamba wanaolipa kodi hizi ni watanganyika by over 95%. Kwa Bahati Mbaya sana, wale wanaokatwa PAYE kwa mfano, hukatwa moja kwa moja kwa serikali kuu/muungano, (sio Tanganyika Kama vile PAYE ya Zanzibar inavyoenda kwa Zanzibar peke yake). Watanganyika hawa Hawana jinsi ya kukwepa wajibu huu ambao kwa kweli ni wa lazima kuliko hiyari. Je:

•sio Haki kwa walipa kodi hawa wa Tanganyika Kuhoji uhalali wa matumizi ya fedha zao?

Kwa kawaida, hawa walipa kodi - wakulima, wafanyakazi, wafanyabiashara, na wengine, legitimacy ya serikali Yao huwa ni tu pale wanapoona faida ya matumizi ya jasho Lao. Hatuwezi kukaa Hapa na kufurahia tu matumizi ya fedha hizi za walipa kodi bila ya kujadili faida kwa walipa kodi hawa. Huu Ndio msingi wa Kuhoji:

•kwanini mlipa kodi wa tanganyika ambebe mwananchi wa nchi Jirani unconditionally?

Kodi ni jasho mtu, kodi ni Mapato halali ya mtu, kodi ni Haki ya mtu Kama vile ilivyokuwa Haki nyingine yoyote inayoainishwa kikatiba.

•Haki hizi kwa mzanzibari Zipo kikatiba, za mtanganyika je?

Kitendo cha kumdai mtanganyika ni lazima kiende sawa na Maelezo juu ya nini kinapatikana ili mlipa kodi Huyu aweze kukubali kupunguziwa Haki yake (jasho on the pay check)- Mapato yake kukatwa. Nje ya hapo, muungano wa serikali Mbili ni dhuluma na ni mzigo kwa mtanganyika, hata mkiziboresha namna gani.

Cc Mag3, Jasusi, JokaKuu, MJINI CHAI, Dingswayo, Nguruvi3, Mkandara, chama, MwanaDiwani, Gamba la Nyoka, zomba, ZeMarcopolo, Mwigulu Nchemba, Bongolander, Mtanganyika



Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Believe me; there is nothing above me on this forum; I can read; research and analyse; I am competent the only thing troubling me is vilaza like you that why I am encouraging you to go to VETA probably when you come back you will be in different level!

Basi acha majigambo, na acha kushambulia watoa hoja, badala yake jadili hoja iliyopo Mbele yako, lakini Kama unatuona sisi vilaza, au mada hizi Zipo chini ya kiwango, si uondoke tu kwenye mjadala mkuu;


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom