JOHN MADIBA
JF-Expert Member
- Jan 30, 2011
- 251
- 155
SPIKA wa Bunge, Anne Makinda, alimwongezea Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, muda wa kuwasilisha utetezi wake dhidi ya Baraza la Mawaziri, lakini mbunge huyo aliwasilisha utetezi wake jana alasiri.
Asubuhi ya jana Makinda alisema amemwongezea muda hadi Jumatatu ijayo, ili athibitishe tuhuma zake kwamba Baraza la Mawaziri lilishawishiwa kubadili msimamo na kubariki azimio la kuongeza muda wa uhai kwa Shirika Hodhi la Mali za Mashirika ya Umma (CHC) kwa miaka mitatu kinyume cha mapendekezo ya Bunge.
Kwa mujibu wa Makinda, wakati akitoa taarifa jana bungeni, Zitto alikuwa amemwomba Spika amsaidie kupata nyaraka kutoka Baraza la Mawaziri na Wizara ya Fedha na Uchumi ambazo zinahusu mjadala wa CHC zitakazomsaidia katika utetezi wake.
Uamuzi huo ulitolewa jana bungeni na Spika Makinda, wakati akitoa taarifa hiyo mara baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali na majibu.
Waheshimiwa wabunge, kwa mujibu wa sheria, nyaraka za Baraza la Mawaziri ni siri; na hili liliwahi kuelezwa na Spika wa Bunge aliyepita Julai 2008 alipokuwa akizungumzia suala la TICS. Hivyo, ofisi yangu haiwezi kumsaidia Zitto kupata nyaraka hizo, ila namwongezea muda hadi Jumatatu Julai 4 mwaka huu, awe amewasilisha utetezi wake, alisema Spika Makinda.
Hata hivyo, taarifa zilizolifikia gazeti hili jana alasiri na kuthibitishwa na Zitto mwenyewe zinaeleza kuwa mbunge huyo ambaye pia ni Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni aliwasilisha utetezi wake, ukiwa na viambatanisho vyote muhimu.
Ingawa Zitto hakuwa tayari kueleza kwa undani aina ya vielelezo alivyowasilisha katika utetezi wake, habari ambazo gazeti hili lilizipata zinaeleza kwamba katika moja ya viambatanisho vyake, mbunge huyo amewasilisha vivuli vya waraka wa Baraza la Mawaziri.
Zitto aliibua hoja hiyo wiki iliyopita wakati akichangia Azimio hilo la CHC, lililowasilishwa bungeni na Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo, hivyo kuwalazimu mawaziri watatu; William Lukuvi (Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge), Waziri Mustafa Mkulo na Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), George Mkuchika, kusimama kila wakati kujibu hoja zake.
Akichangia hoja hiyo, Zitto alisema azimio hilo limegeuzwa tofauti na ilivyokuwa na kusisitiza kuwa hali hiyo imetokana na ushawishi (lobbyist) ambao baraza la mawaziri lilipewa, hivyo aliwataka wabunge kutoyakubali maamuzi hayo akisema yataigharimu nchi.
Nawaombeni sana waheshimiwa wabunge fumbeni macho muangalie suala hili kwa kutokubali maamuzi haya ya Baraza la Mawaziri, maamuzi haya yanatokana na lobbyist, naamini Baraza la Mawaziri halikuwa well advised (halikushauriwa vema), alisema Zitto na kumfanya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kusimama na kuomba mwongozo wa Spika akimtaka Zitto kuthibitisha kauli yake.
Katika mwongozo huo, Mkuchika alisema Zitto amewadhalilisha kwa kulituhumu Baraza la Mawaziri kurubuniwa na watu kupindisha maamuzi hayo ya Bunge, hivyo kumtaka aombe radhi lakini pamoja na hatua hiyo Zitto alisema ana uhakika na anachokisema.
Hatua hiyo ilimfanya pia Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, kukazia kauli ya Waziri Mkuchika na kumtaka Zitto kuthibitisha kauli yake lakini pamoja na kauli hiyo ya Lukuvi Zitto alisimama na kusema kuwa maamuzi ya Baraza la Mawaziri yanatokana na matokeo ya ushawishi kwa baraza hilo na kuitaka serikali kupeleka pendekezo la awali la CHC lililotolewa na Waziri wa Fedha na kuongeza kwamba, Na tusiruhusu baraza la mawaziri kuendeshwa na malobbyist.
Baada ya Zitto kueleza hayo, Lukuvi naye alisimama na kusema anafahamu kuwa Zitto ana uchungu na anakerwa na hali hiyo na kumsisitiza kuthibitisha kauli yake lakini baadaye Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA), alisimama na kusema, Kwa kuwa Zitto amekwisha kutoa taarifa hiyo na kujibiwa na serikali, mwisho wake humrudia mwenyewe (Zitto) ili alihitimishe.
Katika mapendekezo yake Zitto alisema ndani ya Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma na hata katika Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali, walikubaliana kwamba CHC wapewe muda wa kutosha kukamilisha kazi na majukumu yao halafu baada ya hapo ndipo Waziri Mkulo apeleke bungeni Azimio hilo na si kuwapa kipindi cha mpito cha miaka mitatu kama alivyowasilisha azimio hilo jana.
Alisema kuwa chombo hicho kinaangalia mali za umma na mashirika, hivyo kutaka kukiua na kupeleka majukumu haya kwa Msajili wa Hazina ambaye uwezo wake wa kulinda mali za umma ni mdogo sana, ni kutaka kuiba mali za Watanzania.
Alisema azimio la serikali la kuipa CHC kukamilisha majukumu yake limelenga katika kuwasaidia wafanyabiashara walioiba mali za umma ikiwa ni pamoja na kukopa mabilioni ya fedha kutoka iliyokuwa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), ambao kesi zao zipo mahakamani, kupata ahueni kwa vile hatua hiyo itapoteza ushahidi.
Pamoja na Zitto, hoja hiyo iliungwa mkono na Mbunge wa Mwibara, Alphaxard Lugola (CCM), Mbunge wa Kalenga, Dk. William Mgimwa (CCM) na Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed (CUF), waliokomelea msumari wa mwisho katika kupinga hoja hiyo.
Kutokana na hatua hiyo, Spika Anne Makinda, alihitimisha mgongano huo na kumpa siku saba Zitto (hadi Juni 29) kuthibitisha kauli yake hiyo.
Hatua hiyo ilimfanya Waziri Mkulo kulazimika kurekebisha azimio hilo na kusema kwa mujibu wa kifungu cha 5(1) cha sheria ya benki, Bunge linaazimia kuongeza muda wa uhai wa Shirika la CHC kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia Julai mosi hadi Juni 30, 2014 ili kutoa fursa kwa shirika hilo hodhi la mali za mashirika kukamilisha taratibu za kiutendaji na kisheria na baada ya hapo serikali itafanya tathmini ya shirika hilo la CHC na kupeleka taarifa bungeni ili kuona namna litakavyoshughulikiwa.
Awali akiwasilisha hoja ya msingi, Waziri Mkulo ililiomba Bunge kupitisha Azimio hilo ili CHC iweze kuongezewa kipindi cha mpito cha miaka mitatu imalize majukumu yake na baadaye majukumu yake yahamishiwe Ofisi ya Msajili wa Hazina.
Asubuhi ya jana Makinda alisema amemwongezea muda hadi Jumatatu ijayo, ili athibitishe tuhuma zake kwamba Baraza la Mawaziri lilishawishiwa kubadili msimamo na kubariki azimio la kuongeza muda wa uhai kwa Shirika Hodhi la Mali za Mashirika ya Umma (CHC) kwa miaka mitatu kinyume cha mapendekezo ya Bunge.
Kwa mujibu wa Makinda, wakati akitoa taarifa jana bungeni, Zitto alikuwa amemwomba Spika amsaidie kupata nyaraka kutoka Baraza la Mawaziri na Wizara ya Fedha na Uchumi ambazo zinahusu mjadala wa CHC zitakazomsaidia katika utetezi wake.
Uamuzi huo ulitolewa jana bungeni na Spika Makinda, wakati akitoa taarifa hiyo mara baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali na majibu.
Waheshimiwa wabunge, kwa mujibu wa sheria, nyaraka za Baraza la Mawaziri ni siri; na hili liliwahi kuelezwa na Spika wa Bunge aliyepita Julai 2008 alipokuwa akizungumzia suala la TICS. Hivyo, ofisi yangu haiwezi kumsaidia Zitto kupata nyaraka hizo, ila namwongezea muda hadi Jumatatu Julai 4 mwaka huu, awe amewasilisha utetezi wake, alisema Spika Makinda.
Hata hivyo, taarifa zilizolifikia gazeti hili jana alasiri na kuthibitishwa na Zitto mwenyewe zinaeleza kuwa mbunge huyo ambaye pia ni Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni aliwasilisha utetezi wake, ukiwa na viambatanisho vyote muhimu.
Ingawa Zitto hakuwa tayari kueleza kwa undani aina ya vielelezo alivyowasilisha katika utetezi wake, habari ambazo gazeti hili lilizipata zinaeleza kwamba katika moja ya viambatanisho vyake, mbunge huyo amewasilisha vivuli vya waraka wa Baraza la Mawaziri.
Zitto aliibua hoja hiyo wiki iliyopita wakati akichangia Azimio hilo la CHC, lililowasilishwa bungeni na Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo, hivyo kuwalazimu mawaziri watatu; William Lukuvi (Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge), Waziri Mustafa Mkulo na Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), George Mkuchika, kusimama kila wakati kujibu hoja zake.
Akichangia hoja hiyo, Zitto alisema azimio hilo limegeuzwa tofauti na ilivyokuwa na kusisitiza kuwa hali hiyo imetokana na ushawishi (lobbyist) ambao baraza la mawaziri lilipewa, hivyo aliwataka wabunge kutoyakubali maamuzi hayo akisema yataigharimu nchi.
Nawaombeni sana waheshimiwa wabunge fumbeni macho muangalie suala hili kwa kutokubali maamuzi haya ya Baraza la Mawaziri, maamuzi haya yanatokana na lobbyist, naamini Baraza la Mawaziri halikuwa well advised (halikushauriwa vema), alisema Zitto na kumfanya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kusimama na kuomba mwongozo wa Spika akimtaka Zitto kuthibitisha kauli yake.
Katika mwongozo huo, Mkuchika alisema Zitto amewadhalilisha kwa kulituhumu Baraza la Mawaziri kurubuniwa na watu kupindisha maamuzi hayo ya Bunge, hivyo kumtaka aombe radhi lakini pamoja na hatua hiyo Zitto alisema ana uhakika na anachokisema.
Hatua hiyo ilimfanya pia Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, kukazia kauli ya Waziri Mkuchika na kumtaka Zitto kuthibitisha kauli yake lakini pamoja na kauli hiyo ya Lukuvi Zitto alisimama na kusema kuwa maamuzi ya Baraza la Mawaziri yanatokana na matokeo ya ushawishi kwa baraza hilo na kuitaka serikali kupeleka pendekezo la awali la CHC lililotolewa na Waziri wa Fedha na kuongeza kwamba, Na tusiruhusu baraza la mawaziri kuendeshwa na malobbyist.
Baada ya Zitto kueleza hayo, Lukuvi naye alisimama na kusema anafahamu kuwa Zitto ana uchungu na anakerwa na hali hiyo na kumsisitiza kuthibitisha kauli yake lakini baadaye Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA), alisimama na kusema, Kwa kuwa Zitto amekwisha kutoa taarifa hiyo na kujibiwa na serikali, mwisho wake humrudia mwenyewe (Zitto) ili alihitimishe.
Katika mapendekezo yake Zitto alisema ndani ya Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma na hata katika Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali, walikubaliana kwamba CHC wapewe muda wa kutosha kukamilisha kazi na majukumu yao halafu baada ya hapo ndipo Waziri Mkulo apeleke bungeni Azimio hilo na si kuwapa kipindi cha mpito cha miaka mitatu kama alivyowasilisha azimio hilo jana.
Alisema kuwa chombo hicho kinaangalia mali za umma na mashirika, hivyo kutaka kukiua na kupeleka majukumu haya kwa Msajili wa Hazina ambaye uwezo wake wa kulinda mali za umma ni mdogo sana, ni kutaka kuiba mali za Watanzania.
Alisema azimio la serikali la kuipa CHC kukamilisha majukumu yake limelenga katika kuwasaidia wafanyabiashara walioiba mali za umma ikiwa ni pamoja na kukopa mabilioni ya fedha kutoka iliyokuwa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), ambao kesi zao zipo mahakamani, kupata ahueni kwa vile hatua hiyo itapoteza ushahidi.
Pamoja na Zitto, hoja hiyo iliungwa mkono na Mbunge wa Mwibara, Alphaxard Lugola (CCM), Mbunge wa Kalenga, Dk. William Mgimwa (CCM) na Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed (CUF), waliokomelea msumari wa mwisho katika kupinga hoja hiyo.
Kutokana na hatua hiyo, Spika Anne Makinda, alihitimisha mgongano huo na kumpa siku saba Zitto (hadi Juni 29) kuthibitisha kauli yake hiyo.
Hatua hiyo ilimfanya Waziri Mkulo kulazimika kurekebisha azimio hilo na kusema kwa mujibu wa kifungu cha 5(1) cha sheria ya benki, Bunge linaazimia kuongeza muda wa uhai wa Shirika la CHC kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia Julai mosi hadi Juni 30, 2014 ili kutoa fursa kwa shirika hilo hodhi la mali za mashirika kukamilisha taratibu za kiutendaji na kisheria na baada ya hapo serikali itafanya tathmini ya shirika hilo la CHC na kupeleka taarifa bungeni ili kuona namna litakavyoshughulikiwa.
Awali akiwasilisha hoja ya msingi, Waziri Mkulo ililiomba Bunge kupitisha Azimio hilo ili CHC iweze kuongezewa kipindi cha mpito cha miaka mitatu imalize majukumu yake na baadaye majukumu yake yahamishiwe Ofisi ya Msajili wa Hazina.