BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,015
Kuna tetesi kuwa ZZK katumwa na Mkuu wa Kaya..., Nimekuwa nikijiuliza, ni kweli mkuu wa kaya alikuwa hana taarifa za huu ubadhirifu wa mabilioni uliofanywa na aliowateua au ndo tunafanyiwa maigizo tu sisi makabwela?
Kwani Kikwete na Zitto wanashare Urais wa Tanzania mpaka Msanii amtume Zitto amfanyie kazi ambazo Kikwete alistahili kuzifanya? Huyu jamaa kama kiongozi wa nchi anatia aibu sana. Tuliandika hapa kwamba magamba wamtafute mgombea mwingine katika uchaguzi wa 2010 lakini kuna watu wakampigia debe la nguvu akiwemo Malecela na kudai kwamba Magamba wana utamaduni wao wa kuachiana Kiongozi akae madarakani kwa awamu mbili (miaka 10) hivyo kusingekuwa na mgombea mwingine yeyote toka magamba zaidi ya Kikwete. Pamoja na kuvurunda sana katika awamu yake ya kwanza bado magamba wakampitisha kama mgombea wao, sasa wamevuna walichopanda wanahaha huku na kule katika kutaka kuwahadaa Watanzania baada ya kuona kifo chao kinakuja kwa kasi ya kutisha. Kigumu chama cha magamba!!!! Kigumu!!!