Zitambue tofauti za ubebaji maiti na majeruhi na tafsiri yake kiroho

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,634
697,928
Je, umeshashuhudia maiti ikitolewa kwenye kitanda cha hospital na kupelekwa mochwari?

Je, umeshashuhudia maiti akisafirishwa?

Je, umeshashuhudia maiti akitolewa eneo la ajali ama akipelekwa kuzikwa?

Na je umeshashuhudia ubebaji wa majeruhi ama mgonjwa toka eneo la ajali ama hapo anapogonjeka? Au hospital akihamishwa chumba au kitanda!?

Ubebaji wa maiti ni wa kutanguliza kichwa mbele! Tafsiri yake ni kwamba huyu haamki tena... Yaani hatanyanyuka asimame na miguu yake tena. Huyo hiyo ndio hitimisho la safari yake hapa duniani kuelekea kwenye mwendelezo wa maisha mengine nje ya uhai wa kimwili. Kumbeba kinyume kwa kumtanguliza miguu mbele ni kumzuia mchakato wake kuelekea kuzimu. Hapo ni kuleta ukinzani wa nguvu mbili kiroho la lolote linaweza kutokea!

Ubebaji wa majeruhi ni miguu mbele kichwa nyuma! Tafsiri yake kiroho ni kwamba huyu bado anapumua na ana nafasi ya kusimama tena atakapojaaliwa kupona! Kumtanguliza kichwa mbele majeruhi ni kumchulia kifo na lolote linaweza kutokea hata kama majeraha yake hayakuwa makubwa! Hapa kwa wabebaji hakuna shida ila kama ndugu wakawaona na wanafahamu hili, inaweza kuwaletea shida wabebaji

Kama maisha yasivyo na rivasi kuanzia kuzaliwa mpaka kifo ndio hivyo hivyo kifo kisivyo na rivasi kwenye mwili uliokwisha kutengana na roho. Kwenda tofauti na huo mtiririko wa kiasili ni sawa na kwenda kinyume na roho, ukiilazimisha irudi ambako haparudiki. Na roho huwa haipangiwi hivyo itakachoweza kufanya ni kutoa adhabu

Kuna baadhi ya vifo vya majeruhi ni kutokana na matendo ya kwenda kinyume na asili ya kiroho... Kuna vituko na matukio kwenye misiba pia ni kutokana na, kukiuka ama kwenda kinyume na kanuni za mfu na roho iliyoachana na mwili.

Si kila kitu ni laana
Si kila kitu ni maagano
Si kila kitu ni ushirikina
Vingine ni makosa ya kawaida kwa kujua ama kwa kutojua
 
Ubebaji wa maiti ni wa kutanguliza kichwa mbele! Tafsiri yake ni kwamba huyu haamki tena... Yaani hatanyanyuka asimame na miguu yake tena....
1666091217719.png


Wanalijua hilo kweli au walipewa tu mwili waubebe
 
Mshana Jr huwa nafuatilia nyuzi zako ila hii umeipa heading kubwa halafu maelezo ni very shallow.... Natumaini utaijaziia au kuipa mwendelezo hii maada.

Nawasilisha
Nadhani ni kweli ni kama vile kuna kitu kinahitaji kuongezewa
 

View attachment 2391020
Kifo cha malkia taratibu zake ni tofauti kabisa na taratibu za taratibu za vifo vingine.. Baadhi ni hizi hapa
. Mmojawapo wa viongozi wa kiroho baada ya kifo humtangazia marehemu ukuhani wa nguvu za siri na kumtakia maziko ya kawaida kama dada katika Kristo
. Kuna nyuki kwenye viunga vya vya kasri la malikia hujulishwa kifo cha malikia kwa kuwekewa vitambaa vya rangi fulani kama sikosei ni nyeupe au nyekundu
. Kuchinja mbuzi wa kafara
. Kwenye jeneza,sehemu ya crown ni shada la maua, sehemu ya msalaba ni crown yenye msalama na fimbo ya malkia, msalaba huja miguuni.. Tafsiri ya msalaba ni kifo na kufufuka kama Kristo..
 
Huko ulaya majeruhi na wagonjwa mahututi wanabebwa tuu wakiangalia mbele huku ndg Zao wakiwa wamezunguka kitanda wakisaidia kusuma kitanda hicho
Ndio maana kuna 'haunted houses' nyingi sana na maroho na mapepo kila mahali
 
Naongeza kidogo maiti sharti itoke na kuingia ndani kupitia mlango wa mbele ya nyumba. Kama uwewahi kupewa tenda ya ujenzi wa matuary kuna mlango mmoja wa kuingia na kutoka maiti. Pia jokofu lazima kichwa kiwe mbele huku unakovutia au kusukumia maiti.

Maiti haitolewi mlango wa nyuma ni mwiko. Ilikoingilia maiti ndiko itakakotokea.
Mortuary ya hospital ya wilaya ni nilipo ni tofauti milango ipo miwili, wa kuingia na kutokea mwingine usidanganye

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom