Just Distinctions
JF-Expert Member
- May 5, 2016
- 2,781
- 5,440
na ukiwekewa umeme ni unit ngapi unapewa kama kianzio? maana mi nimepewa 10 tu
Hakuna cha siku 60 au siku 100 nimelipia kuunganishiwa umeme nguzo moja tu tangu october 2016 hadi sasa ni usumbufu tu bora hela yangu ningenunua solar
HATUA YA KWANZA
MAOMBI YA MWANZO
Je mteja anaweza kuchukua fomu ofisi yeyote ya tanesco?
Mteja anaweza kuchukua fomu ya maombi ya umeme katika ofisi yeyote ya shirika bila kujali kuwa eneo hilo linahudumiwa na ofisi husika. Ila atapaswa kurudisha ofisi ya maeneo ambayo makazi yake yapo ili kurahisisha kufanyiwa vipimo (service line survey)
JE KUNA GHARAMA ZOZOTE KATIKA UCHUKUAJI WA FOMU?
Fomu za maombi ya umeme zinatolewa bure kabisa kwa wateja wote.
VITU MUHIMU VYA KUZINGATIA WAKATI WA KUCHUKUA FOMU
1. Hakikisha umeme umefika maeneo yako na kama ni mradi uwe umekamilika.
2. Hakikisha mtandao wa nyaya ndani ya nyumba yako (wiring) umefanyika kupitia mkandarasi aliyesajiliwa.
3. Kitambulisho kinachomtambulisha muombaji wa umeme mfano leseni ya udereva, hati ya kusafiria, kitambulisho cha kazi (hii inasaidia shirika kumtambua mteja husika)
4. Kwa mwombaji wa mita ya ziada (meter separation) jina litakalotumika ni la mwenye nyumba kama linavyosomeka katika mita ya awali. Vinginevyo mteja atapaswa kutumia uthibitisho wa ruhusa ya mwenyenyumba kama atakuwa ni mpangaji. Lazima mteja aje na namba ya mita (kama zipo zaidi ya moja aje nazo zote) ili kuhakiki kama kuna yenye deni.
5. Kwa waombaji wanaomba kwa ajili ya ofisi, makapuni au taasisi za serikali au binafsi anapaswa kuja na leseni ya biashara, tin namba, udhibitisho wa usajili wa kampuni. Au udhibitisho wa ofisi ya serikali husika.
6. Kwa wapangaji wa nyumba za taasisi au makampuni waje na barua za waliopangisha zinazoonyesha kuwe wenye nyumba hizo wameridhia mita husika iwe na jina la mpangaji husika.
7. Shirika linapenda kuwaomba wamiliki wa nyumba kupenda kufika ofisi zetu wenyewe ili kuzuia udanganyifu ambao umekuwa ukifanywa na baadhi ya watu wasiokuwa waaminifu
HATUA YA PILI KUWEKA MCHORO, PICHA NA KUINGIA MAKUBALIANO YA KUFUNGIWA UMEME NAKUREJESHA FOMU
Endapo mteja atakidhi vigezo na masharti ya hatua ya mwanzo na kupatiwa fomu ya maombi ya mwanzo anatakiwa afanye yafuatayo
1. Kuisoma fomu kwa umakini mkubwa na kukubailiana na vigezo namba moja mpaka kumi na mbili. Mteja akijiridhisha kuwa amekubaliana na masharti yote ataweka sahihi sehemu husika (ukurasa wa pili wa fomu ya maombi ya umeme)
2. Kumpatia mkandarasi aliyesajiliwa ili achore mchoro wa mtandao wa nyaya (wiring diagram) wa nyumba husika pamoja na kugonga muhuri. (gharama ni makubaliano baina ya mteja na mkandarasi husika), wakandarasi wanapatikana kwenye ofisi zao maeneo mbalimbali, orodha ya waliosajiliwa pia inapatikana kwenye ofisi za tanesco. Mteja anapaswa kupewa orodha na kuchagua mkandarasi anayemtaka yeye.
3. Mteja atapaswa kuweka picha moja ya mwombaji wa umeme
4. Kisha mteja atarudisha fomu hiyo iliyokamilika ofisi ya eneo ambalo makazi yake yako (inayomudumia)
HATUA YA TATU- KUFANYIWA VIPIMO (SURVEY)
Mara baada ya mteja kurejesha fomu iliyojazwa kikamilifu, mteja atapangiwa tarehe ya kufanyiwa vipimo (survey). Mafundi watafika kwenye nyumba au sehemu inayoombewa umeme ili kutathimini gharama atakazolipia mteja kwa kuzingatia umbali wa eneo ilipo miundombinu ya umeme kama nguzo na transfoma na uwezo wa umeme huo kuunganisha kwa wateja wapya.
HATUA YA NNE: - KUPATIWA MAKADIRIO YA GHARAMA KIASI GANI ALIPE ILI AFUNGIWA UMEME
Mara baada ya kufanyiwa tathimini mteja anaweza kupatiwa makadirio ya gharama ya kiasi gani alipe ili kufungiwa umeme. Makadirio haya huweza kutumwa kwa njia ya nukushi, ujumbe mfupi wa meneno, barua pepe au mteja kufika ofisini na kuchukua barua. Viwango vya muda wa kutoa makadirio kama inavyoonekana kwenye jedwali hapo chini:
MAELEZO
Muda wa makadirio
Kama miundombinu iliyopo itatumika (ndani ya mita 30 kutoka kwenye nguzo iliyokaribu)
Ndani ya siku 7 za kazi
Ujenzi wa njia ya nyongeza unahitajika (mita 30- 100)
Ndani ya siku 10 za kazi
Kama mfumo mpya wa usambazaji unahitajika kujegwa au mfumo wa umeme mkubwa unahitajika kuongezwa kwa ajili ya kiwanda au biashara kubwa (kama hakuna mfumo wa kumuunganishia mwombaji) (zaidi ya mita 100)
Ndani ya siku 14 za kazi
HATUA YA TANO: - KUFANYA MALIPO
Mteja atafika ofisi ya tanesco ili kupatiwa namba ya kumbukumbu (reference number) itakayomuwezesha kufanya malipo bank, mteja atafanya malipo na atapatiwa stakabadhi ya malipo bank (risiti kwa njia ya ujumbe mfupi- sms) (kwa sasa ni bank ya nmb tu), wateja wanahimizwa kufanya malipo yote bank na si kwa mtu mwingine yeyote. Malipo yote yatakayofanyika nje ya mfumo uliwekwa hayatambulika na tanesco. Mteja akishafanya malipo bank husika hatatakiwa kurudi tena tanesco bali tanesco watakuwa na taarifa zake zote na kinachofuata ni kumfungia umeme.
HATUA YA SITA:-KUUNGANISHIWA UMEME
Mara baada ya mteja kufanya malipo viwango vya muda wa kumfungia umeme vitakuwa kama ilivyoonyeshwa kwenye jedwali hapo chini.
MAELEZO
Muda wa kufungiwa
Kama miundombinu iliyopo itatumika (ndani ya mita 30 kutoka kwenye nguzo iliyokaribu)
Ndani ya siku 30 za kazi
Ujenzi wa njia ya nyongeza itahitajika
(mita 30- 100)
Ndani ya siku 60 za kazi
KAMA MFUMO MPYA WA USAMBAZAJI UNAHITAJIKA KUJEGWA AU MFUMO WA UMEME MKUBWA UNAHITAJIKA KUONGEZWA KWA AJILI YA KIWANDA AU BIASHARA KUBWA (KAMA HAKUNA MFUMO WA KUMUUNGANISHIA MWOMBAJI) (ZAIDI YA MITA 100)
Ndani ya siku 90 za kazi
KWA MAULIZO WASILIANA NASI
Kituo cha huduma kwa wateja: - 0768985100/0222194400
Barua pepe: customer.Service@tanesco.Co.Tz
Facebook: www.Facebook.Com/tanesco yetu
Twitter: - www.Twitter.Com/tanesco yetu
Tovuti; www.Tanesco.Co.Tz
Na ile naona wanaandika volt 380 ina maana ni below au na resistsnce Mohms kwa single na three phase huwa ni nagapi?1. Kuhusu meter ngapi hapo huwezi kusema mpaka surveyor afike site na kuangalia mazingira yalivyokaa na namna gani ata design ili uweze kupata huo umeme
2. Cut out inafungwa baada ya meter kabla ya umeme kuingia kwenye main switch ambayo itakuwa na Circuit Breaker. Kuweka Cut Out sio lazima ila ukiweka ni sawa.
3. Kuhusu umeme wa single phase au three phase inatagemea na load yako. Load inamaanisha mahitaji yako ya umeme. Mfano unatumia taa ngapi, fridge ngapi, labda una pump ya maji, una cooker, una tv ngapi, una ac ngapi.
Hapo contractor wako wa umeme anataefanya wiring ya nyumba yako ndio ata calculate load yako na akipata total KW unazohitaji ndio ita determine unahitaji single au three phase..
Hivyo hakuna kusema eti umeme wa single au wa three phase ndio mzuri hapana. Aina ya phase unayowekewa inatokana na load yako. Mara nyingi ukiwa na load kuanzia 14kW kwenda juu hiyo ni three phase ina maana kushuka chini ni single phase.
Na huwezi kuwekewa three phase ukiwa na load ndogo kwakuwa umeme wa three phase una Volts kuanzia 400 wakati single phase ni 220- 200 Volts.
Hivyo basi ukiwekewa umeme wa Volts 400 wakati una load ndogo inaweza kupelekea vitu vyako kua overloaded na kuungua na ukiwekewe umeme wa volts 210 wakati load yako ni kubwa basi usishangae ukiwasha ac haziwaki mara cooker haliwaki maana umeme unakuwa mdogo. Asante
hapo kwa kuangalia mita za aina gani ?Cut-out ni kifaa cha umeme ambacho kina unganisha cable ya umeme ya tanesco na wiring ya mteja. Yaani hapa ndipo pale umeme wa tanesco unakutana na wiring system ya mteja inapoanzia.
Kazi yake ni kuhakikisha kuwa kuwa umeme unahitaji mteja unapita salama kwenda kwenye nyumba yako.
Inaunganishwa direct kwenye umeme unaokuja kwako mteja na ina kitu kinaitwa ‘main fuse’. Hii husaidia kuhakikisha kiwango sahihi cha umeme kinaingia kwenye nyumba yako.
Kama umeme ukiwa mwingi unataka kuingia kwenye nyumba yako hiyo main fuse inafanya isolation ili umeme huo usiingie kwenye nyumba ili vitu visiungue na hapo inafanya kuzuia umeme usiingie kwako kwa kiwango kikubwa kwa ku trip na umeme kukata kwemye jengo kukiwa na overload ya voltage.
saaaaaafiiiiiiiiiiiiiiii nimeelewaMimi ni mwananchi wa kawaida tu kama wewe na kweli nina uzoefu na masuala ya Tanesco.
Kuna tabia ya sisi watanzania wengu kutopenda kusoma au kuomba kueleweshwa mambo. Ukifanya application ya maombi ya umeme ile form unayopewa ina maelezo yakutosha na kuna kipengele kinaeleza kuwa "material yote kuanzia kwenye nguzo mpaka kwenyr meter vitabaki kuwa mali ya Tanesco"
Kwanini mali ya Tanesco!?
Jibu: Tanesco wanatoa huduma ya umeme na hawauzi meter wala nguzo wala nyaya, wao wanasambaza huduma ya umeme na wewe unacholipia ni gharama kwaajili ya kupatiwa huduma ya umeme na sio gharama kwaajili yakuuziwa nguzo au meter.
Kwa mantiki hiyo basi kama uli sign ule mkataba ina maana ulisoma na kuridhia yaliyoandikwa na hivyo hupasi kupinga pale utakapoambiwa kuwa huwezi kuhamisha hiyo meter kwakuwa sio mali yako na huko unapoenda kama utahitaji umeme lazima ufanye maombi upya na kulipia gharama kama kawaida.
Kuhusu kupungua kwa gharama ni katika ku upgrade tu kutoka labda single phase kuenda three phase katika nyumba hiyo hiyo. Mfano una meter ya single phase lakini matumizi yako yameongezeka na hiyo haikidhi load uliyonayo basi utafanya maombi ya kuomba umeme na contractor wako atachora mchoro wa wiring na kuonyesha vifaa vilivyopo na total load kisha baada ya taratibu zote ile gharama ya three phase service line itachukuliwa kisha itatolewa ile uliyolipia mwanzo (single phase)
Mfano kama ulilipia 500 kupata single phase na gharama ya three phase ni 2000 basi watafanya 2000-500 na utalipia 1500
ThanksHATUA YA KWANZA
MAOMBI YA MWANZO
Je mteja anaweza kuchukua fomu ofisi yeyote ya tanesco?
Mteja anaweza kuchukua fomu ya maombi ya umeme katika ofisi yeyote ya shirika bila kujali kuwa eneo hilo linahudumiwa na ofisi husika. Ila atapaswa kurudisha ofisi ya maeneo ambayo makazi yake yapo ili kurahisisha kufanyiwa vipimo (service line survey)
JE KUNA GHARAMA ZOZOTE KATIKA UCHUKUAJI WA FOMU?
Fomu za maombi ya umeme zinatolewa bure kabisa kwa wateja wote.
VITU MUHIMU VYA KUZINGATIA WAKATI WA KUCHUKUA FOMU
1. Hakikisha umeme umefika maeneo yako na kama ni mradi uwe umekamilika.
2. Hakikisha mtandao wa nyaya ndani ya nyumba yako (wiring) umefanyika kupitia mkandarasi aliyesajiliwa.
3. Kitambulisho kinachomtambulisha muombaji wa umeme mfano leseni ya udereva, hati ya kusafiria, kitambulisho cha kazi (hii inasaidia shirika kumtambua mteja husika)
4. Kwa mwombaji wa mita ya ziada (meter separation) jina litakalotumika ni la mwenye nyumba kama linavyosomeka katika mita ya awali. Vinginevyo mteja atapaswa kutumia uthibitisho wa ruhusa ya mwenyenyumba kama atakuwa ni mpangaji. Lazima mteja aje na namba ya mita (kama zipo zaidi ya moja aje nazo zote) ili kuhakiki kama kuna yenye deni.
5. Kwa waombaji wanaomba kwa ajili ya ofisi, makapuni au taasisi za serikali au binafsi anapaswa kuja na leseni ya biashara, tin namba, udhibitisho wa usajili wa kampuni. Au udhibitisho wa ofisi ya serikali husika.
6. Kwa wapangaji wa nyumba za taasisi au makampuni waje na barua za waliopangisha zinazoonyesha kuwe wenye nyumba hizo wameridhia mita husika iwe na jina la mpangaji husika.
7. Shirika linapenda kuwaomba wamiliki wa nyumba kupenda kufika ofisi zetu wenyewe ili kuzuia udanganyifu ambao umekuwa ukifanywa na baadhi ya watu wasiokuwa waaminifu
HATUA YA PILI KUWEKA MCHORO, PICHA NA KUINGIA MAKUBALIANO YA KUFUNGIWA UMEME NAKUREJESHA FOMU
Endapo mteja atakidhi vigezo na masharti ya hatua ya mwanzo na kupatiwa fomu ya maombi ya mwanzo anatakiwa afanye yafuatayo
1. Kuisoma fomu kwa umakini mkubwa na kukubailiana na vigezo namba moja mpaka kumi na mbili. Mteja akijiridhisha kuwa amekubaliana na masharti yote ataweka sahihi sehemu husika (ukurasa wa pili wa fomu ya maombi ya umeme)
2. Kumpatia mkandarasi aliyesajiliwa ili achore mchoro wa mtandao wa nyaya (wiring diagram) wa nyumba husika pamoja na kugonga muhuri. (gharama ni makubaliano baina ya mteja na mkandarasi husika), wakandarasi wanapatikana kwenye ofisi zao maeneo mbalimbali, orodha ya waliosajiliwa pia inapatikana kwenye ofisi za tanesco. Mteja anapaswa kupewa orodha na kuchagua mkandarasi anayemtaka yeye.
3. Mteja atapaswa kuweka picha moja ya mwombaji wa umeme
4. Kisha mteja atarudisha fomu hiyo iliyokamilika ofisi ya eneo ambalo makazi yake yako (inayomudumia)
HATUA YA TATU- KUFANYIWA VIPIMO (SURVEY)
Mara baada ya mteja kurejesha fomu iliyojazwa kikamilifu, mteja atapangiwa tarehe ya kufanyiwa vipimo (survey). Mafundi watafika kwenye nyumba au sehemu inayoombewa umeme ili kutathimini gharama atakazolipia mteja kwa kuzingatia umbali wa eneo ilipo miundombinu ya umeme kama nguzo na transfoma na uwezo wa umeme huo kuunganisha kwa wateja wapya.
HATUA YA NNE: - KUPATIWA MAKADIRIO YA GHARAMA KIASI GANI ALIPE ILI AFUNGIWA UMEME
Mara baada ya kufanyiwa tathimini mteja anaweza kupatiwa makadirio ya gharama ya kiasi gani alipe ili kufungiwa umeme. Makadirio haya huweza kutumwa kwa njia ya nukushi, ujumbe mfupi wa meneno, barua pepe au mteja kufika ofisini na kuchukua barua. Viwango vya muda wa kutoa makadirio kama inavyoonekana kwenye jedwali hapo chini:
MAELEZO
Muda wa makadirio
Kama miundombinu iliyopo itatumika (ndani ya mita 30 kutoka kwenye nguzo iliyokaribu)
Ndani ya siku 7 za kazi
Ujenzi wa njia ya nyongeza unahitajika (mita 30- 100)
Ndani ya siku 10 za kazi
Kama mfumo mpya wa usambazaji unahitajika kujegwa au mfumo wa umeme mkubwa unahitajika kuongezwa kwa ajili ya kiwanda au biashara kubwa (kama hakuna mfumo wa kumuunganishia mwombaji) (zaidi ya mita 100)
Ndani ya siku 14 za kazi
HATUA YA TANO: - KUFANYA MALIPO
Mteja atafika ofisi ya tanesco ili kupatiwa namba ya kumbukumbu (reference number) itakayomuwezesha kufanya malipo bank, mteja atafanya malipo na atapatiwa stakabadhi ya malipo bank (risiti kwa njia ya ujumbe mfupi- sms) (kwa sasa ni bank ya nmb tu), wateja wanahimizwa kufanya malipo yote bank na si kwa mtu mwingine yeyote. Malipo yote yatakayofanyika nje ya mfumo uliwekwa hayatambulika na tanesco. Mteja akishafanya malipo bank husika hatatakiwa kurudi tena tanesco bali tanesco watakuwa na taarifa zake zote na kinachofuata ni kumfungia umeme.
HATUA YA SITA:-KUUNGANISHIWA UMEME
Mara baada ya mteja kufanya malipo viwango vya muda wa kumfungia umeme vitakuwa kama ilivyoonyeshwa kwenye jedwali hapo chini.
MAELEZO
Muda wa kufungiwa
Kama miundombinu iliyopo itatumika (ndani ya mita 30 kutoka kwenye nguzo iliyokaribu)
Ndani ya siku 30 za kazi
Ujenzi wa njia ya nyongeza itahitajika
(mita 30- 100)
Ndani ya siku 60 za kazi
KAMA MFUMO MPYA WA USAMBAZAJI UNAHITAJIKA KUJEGWA AU MFUMO WA UMEME MKUBWA UNAHITAJIKA KUONGEZWA KWA AJILI YA KIWANDA AU BIASHARA KUBWA (KAMA HAKUNA MFUMO WA KUMUUNGANISHIA MWOMBAJI) (ZAIDI YA MITA 100)
Ndani ya siku 90 za kazi
KWA MAULIZO WASILIANA NASI
Kituo cha huduma kwa wateja: - 0768985100/0222194400
Barua pepe: customer.Service@tanesco.Co.Tz
Facebook: www.Facebook.Com/tanesco yetu
Twitter: - www.Twitter.Com/tanesco yetu
Tovuti; www.Tanesco.Co.Tz
Ndugu mpendwa mteja wetu kwa heshima kubwa kabisa tunaomba uambue kuwa TANESCO kupitia usimamizi mzuri wa serikali yetu imefanya kazi kubwa sana haswa kwenye uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme.utakuwa shahidi kuwa leo vijiji vingi na maeneo mengi ya mijini yafurahia umeme. Shirika linaendelea kusambaza umeme kwa awamu mbalimbali hivyo uvumilivu wako na taarifa sahihi za eneo lako na namba yako ya simu itatusaidia kukupatia ufafanuziTanesco ifutwe haina faida inajiendesha KIBWANYENYE sana! Dar kuna sehemu umeme haujafika vipi kuhusu NAMINYWIRI? Vipi Kuhusu NAMTUMBO? Vipi Kuhusu NYAMISATI,vp kuhusu NAMANYERE,NKASI? Vipi Kuhusu KAZURAMIMBA?
View attachment 1030837
View attachment 1030846
View attachment 1030847
Maeneo yote hayo uliyotaja umeme upo ni baadhi ya maeneo machacha haujafika hivyo ni vema kutuunga mkono badala ya kuona hatujafanya chochoteNdugu mpendwa mteja wetu kwa heshima kubwa kabisa tunaomba uambue kuwa TANESCO kupitia usimamizi mzuri wa serikali yetu imefanya kazi kubwa sana haswa kwenye uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme.utakuwa shahidi kuwa leo vijiji vingi na maeneo mengi ya mijini yafurahia umeme. Shirika linaendelea kusambaza umeme kwa awamu mbalimbali hivyo uvumilivu wako na taarifa sahihi za eneo lako na namba yako ya simu itatusaidia kukupatia ufafanuzi
Sent using Jamii Forums mobile app
Niliomba umeme mwaka 2016 mpaka sasa haujafika,nilijaribu kufatilia nikaambiwa baadhi ya wafanyakazi wasio waaminifu wa TANESCO wamekula fedha ya mradi karibia milioni mia 5,kwasasa nimefunga solar tu,nguzo zipo tu zimeachwa kama mapambo ila kwenye vikao vya kwenu huko huwa wanasema TAYARI TUSHAPATA Umeme wakati Fedha 500m watu wamekula!! Tushaandika Barua kwenda kwa Waziri kuelezea huo WIZI tunasubiri majibu.Ndugu mpendwa mteja wetu kwa heshima kubwa kabisa tunaomba uambue kuwa TANESCO kupitia usimamizi mzuri wa serikali yetu imefanya kazi kubwa sana haswa kwenye uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme.utakuwa shahidi kuwa leo vijiji vingi na maeneo mengi ya mijini yafurahia umeme. Shirika linaendelea kusambaza umeme kwa awamu mbalimbali hivyo uvumilivu wako na taarifa sahihi za eneo lako na namba yako ya simu itatusaidia kukupatia ufafanuzi
Sent using Jamii Forums mobile app