Zanzibar ni sawa na Kigoma, asema Shamsa Vuai Nahodha

Nikupateje

JF-Expert Member
Dec 22, 2009
1,334
988
Kuifananisha Zanzibar na mkoa wowote wa Tanzania Bara imekuwa ni dhana ikikataliwa hasa na wazanzibar. Tunakumbuka Julai 2008, Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliingia matatani aliposema Zanzibar siyo nchi.

Leo tena Bungeni kumeibuka hoja hiyo. Mheshimiwa Zitto Kabwe aliuliza swali zuri tu, swali alilomuuliza Waziri Shamsa Vuai Nahodha. Swali lenyewe ni kwamba siku haijawahi kutokea tangu tujitawale Mkuu wa Majeshi (Chief of Defence forces/TPDF) akatoka Zanzibar. Wakuu wote wamekuwa wakitoka Bara.

Swali likaendelea kuuliza je, Waziri anaweza kutamka kuwa sasa inawezekana akapendekezwa mkuu kutoka Zanzibar?

Kila mmoja hata mimi nikajawa na shauku kujua jibu la swali hili. Binafsi nilijisiki vizuri mbele ya TV yangu kwanza nikijua kwamba swali linajibiwa na mzanzibar na aliyewahi kuwa Waziri Kiongozi wa Serikali ya Zanzibar.

Kwa kweli alijibu vizuri kwa kusema kuna wanzanzibar kadhaa kwenye ngazi za juu ya jeshi letu (TPDF) katika ngazi ya Brigedier-General na wengine. Hivyo upo uwezekano japo hawezi kutamka rasmi kama itakuwa hivyo. Hadi hapo kwa hakika swali likawa limeisha.

Lakini Nahodha akaongezea kauli nyingine ambayo sidhani kama alipima matokeo yake. Akasema hata hivyo na yeye kama Nahodha anajua historia ya CHADEMA ambako hajawahi kusikia Mwenyekiti wa CHADEMA akitokea mkoa wa KIGOMA. Bunge zima likabaki linacheka. Kwani muuliza swali aliyekuwa anajibiwa ni Zitto kabwe na anatokea Kigoma.

Athari za jibu hili ni nini? Zitto aliipa Zanzibar uzito unaostahili katika uwiano wa mambo ya muungano. Kwa namna moja Zitto anaonyesha kwamba kuna usawa wa eneo wa iliyokuwa Tanganyika na usawa kwa eneo la Zanzibar. Hivi viwili ndivyo vinavyobidi kulinganishwa.

Sasa, Nahodha anapojibu swali kwa kulinganisha Zanzibar na Kigoma basi hii ni hoja yake na wala haikuwa mlinganisho wa Zitto Kabwe.

Maadam mlinganisho huu umetajwa na mzanzibar basi wazanzibar waache kulalamika wanapolinganishwa Zanzibar yote kama mkoa wowote wa bara. Maana ni ukweli kwamba Zanzibar inaingia zaidi ya mara tatu kwenye mkoa wa Mwanza kieneo na population.

Binafsi ninamshukuru sana mzanzibar huyu Shamsa Vuai Nahodha kwa ulinganisho huu, maana ingekuwa leo amesema mbara yaani m-tanganyika sijui upepo ungekuwaje mle bungeni na siajabu dakika hii ingekuwa ni mfululizo wa kuomba miongozo kwa spika kwa kitendo cha kuilinganisha Zanzibar na mkoa.

Shukurani sana Shamsa Vuai Nahodha.
 
duh,kweli waziri.alitaka kumanisha nini sasa,maana swali liko linajieleza na suala la muungano ni la nchi nzima na wala siochama cha siasa.kweli waziri zaifu amejaa mipasho,au komba anatoa training ya mipasho kwa magamba???
kweli raisi zaifu hawezi kuteua waziri mahili.
 
Zitto anauliza swali kama hilo ili iweje? Kwani jeshini watu wanapewa madaraka kwa kutumia taratibu gani? Nahodha amejibu vizuri sana.
 
Hongera mkuu, naona umejitahidi kuweka maneno kwenye mdomo wa Nahodha!
 
Zitto anauliza swali kama hilo ili iweje? Kwani jeshini watu wanapewa madaraka kwa kutumia taratibu gani? Nahodha amejibu vizuri sana.

Sidhani kama umesikiliza kipindi chote cha bunge leo. Swali unalouliza Serikali wamejitahidi kujibu kama dhana yako katika sehemu mbalimbali za nchi hii lakini serikali imefika mahala imeona jibu kama lako halina msingi na wabunge wauliza maswali wana hoja.

Imetajwa mifano mingi kama vile kusini ambako wamelalamika hawaoni wanajeshi wakiajiriwa kwa wingi huko japo iliahidiwa mambo yatakuwa sawa. Waziri amekubali kwamba wabunge waonapo kasoro wazitaarifu mara moja.

Na hata katika majibu ya Nahodha kwa Zitto hakujikita kwenye hoja kama ya kwako. Zitto kapewa majibu sahihi isipokuwa alichofanya Nahodha ni kile waswahili wanachoita kuchamba kwingi mwisho unashika na mavi badala ya kujisafisha.

Una haki ya kutoa maoni lakini sijui yamejikita katika msingi gani wakati hata unaodhani unawatetea ni wazi hawaoni msaada wa utetezikatika hoja yako.
 
Hongera mkuu, naona umejitahidi kuweka maneno kwenye mdomo wa Nahodha!

Kwani mimi ndiye niliyempanua mdomo ili atamke neno KIGOMA au CHADEMA ambavyo havikuwa msingi wa swali?

Nahodha abebe mzigo wa kauli yake ambayo imerekodiwa kwenye hansard.
 
Nazidi kuamini kwamba CHADEMA inaogopeka sana kwenye korido za ccm/cuf na serikali
 
Kwani mimi ndiye niliyempanua mdomo ili atamke neno KIGOMA au CHADEMA ambavyo havikuwa msingi wa swali?

Nahodha abebe mzigo wa kauli yake ambayo imerekodiwa kwenye hansard.

Kwahiyo Nahodha kasema Zanzibar ni sawa na Kigoma na imerekodiwa kwenye hansard? au ni ushabiki wako tu wa kuhusishanisha visivyokuwepo?
 
Saafi Sheikh Nahodha, Zanzibar ni sawa na Hong Kong kwa China, Special Administrative Region
 
Zitto anauliza swali kama hilo ili iweje? Kwani jeshini watu wanapewa madaraka kwa kutumia taratibu gani? Nahodha amejibu vizuri sana.

Watu wanaopewa madaraka jeshini ni wale wanaotimiza vigezo vilivyo wekwa.ndio maana zito akauliza swali hilo akiamini kuwa hata zanzibar watu hawo wapo lakini hawajapewa hiyo nafasi tangu uhuru.kitendo cha waziri kushindwa kujibu swali moja kwa moja mpaka akazungukia kigoma ni kuwafanya wazanzibar wenzake hawana uwezo huwo wamezidiwa hata na watu wa kigoma.
 
Hao akina Nahodha ndio wasaliti wenyewe wa Wazanzibari. Idiot.
 
Watu wanaopewa madaraka jeshini ni wale wanaotimiza vigezo vilivyo wekwa.ndio maana zito akauliza swali hilo akiamini kuwa hata zanzibar watu hawo wapo lakini hawajapewa hiyo nafasi tangu uhuru.kitendo cha waziri kushindwa kujibu swali moja kwa moja mpaka akazungukia kigoma ni kuwafanya wazanzibar wenzake hawana uwezo huwo wamezidiwa hata na watu wa kigoma.

Said Abdallah Natepe alikuwa upande gani wa Tanzania na alipewa majukumu ya aina gani? Halafu hujajibu hoja ya utaratibu upi unatumiwa kumpata kiongozi wa majeshi yetu maana kama kuna wanajeshi 10 walio na sifa za kupata hiko cheo, lazima atakayepewa ni mmoja tu. Kwanini apate yeye ndio nataka kujua. Haya mambo ya kugawana madaraka kama njugu yameanza kufanya hili Taifa liende mrama kwa kukosa maarifa na kuwajibika.
 
Said Abdallah Natepe alikuwa upande gani wa Tanzania na alipewa majukumu ya aina gani? Halafu hujajibu hoja ya utaratibu upi unatumiwa kumpata kiongozi wa majeshi yetu maana kama kuna wanajeshi 10 walio na sifa za kupata hiko cheo, lazima atakayepewa ni mmoja tu. Kwanini apate yeye ndio nataka kujua. Haya mambo ya kugawana madaraka kama njugu yameanza kufanya hili Taifa liende mrama kwa kukosa maarifa na kuwajibika.
Upande aliokuwepo na majukumu yake alitakiwa ajibu waziri km alivyoulizwa na mh zitto.mkuu wa majeshi anateuliwa na amiri mkuu wa majeshi kwa kuzingatia utalaam wa kijeshi alionao mteuliwa.

Hata katika hao 10 kwa mjibu wa majibu ya waziri mzenji hajawahi kuwa miongoni mwao ili awezekuteuliwa tangu uhuru ili nchi isiende mrama ndio maana waziri kawaona wa kgm kuwa na uwezo kuliko wazenji.
 
Inasikitisha, bunge limejaa vijembe badala ya hoja za msingi. Ni vyema hawa waheshimiwa wakarudisha posho zetu kwani hatukuwapeleka bungeni kwenda kupashana, wakitaka kupashana waingie studio au mitaani.
 
swali la Zitto ni la kinafiki sehemu nyeti kama ya mkuu wa majeshi uwezi kuteua kwa kuangalia Uzanzibar au Utanganyika maasi ya mwaka 64 yalitufundisha mengi mkuu wa majeshi mbali na kuwa na sifa za kijeshi pia anahitajika kuwa mtu anayeungwa mkono na watu wa chini yake kumbuka hao watu wanashika silaha ukiteua mtu kwa uwiano wanaweza kutumia zana hizo hizo kuonyesha hisia zao tunataka watu wateuliwe kwa uwezo na vigezo vya sehemu husika
 
nikionacho mimi toka kwenye majibu ya Nahodha ni kuwa ndani ya CCM wengi wao wanaona njia pekee ya kukizuia CDM kujijenga ni kukizushia habari za ukabila na umaeneo. kwake Nahodha alichokuwa anajaribu kukiwakilisha ni kuwa CDM wao ni watu wa kaskazini tu watakaoshika uenyekiti wake na si toka sehemu nyinginezo. kwa vile hii sio mara ya kwanza kwa viongozi waandamizi wa CCM kuleta hoja za ukabila/udini/u-mikoa dhidi ya CDM, bila shaka yoyote hii ndo hoja yao pekee dhidi ya CDM, ambayo wanajua inaweza kufanya kazi. nyinginezo zimeshindwa....no wonder wanakosa usingizi
 
Kuifananisha Zanzibar na mkoa wowote wa Tanzania Bara imekuwa ni dhana ikikataliwa hasa na wazanzibar. Tunakumbuka Julai 2008, Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliingia matatani aliposema Zanzibar siyo nchi.

Leo tena Bungeni kumeibuka hoja hiyo. Mheshimiwa Zitto Kabwe aliuliza swali zuri tu, swali alilomuuliza Waziri Shamsa Vuai Nahodha. Swali lenyewe ni kwamba siku haijawahi kutokea tangu tujitawale Mkuu wa Majeshi (Chief of Defence forces/TPDF) akatoka Zanzibar. Wakuu wote wamekuwa wakitoka Bara.

Swali likaendelea kuuliza je, Waziri anaweza kutamka kuwa sasa inawezekana akapendekezwa mkuu kutoka Zanzibar?

Kila mmoja hata mimi nikajawa na shauku kujua jibu la swali hili. Binafsi nilijisiki vizuri mbele ya TV yangu kwanza nikijua kwamba swali linajibiwa na mzanzibar na aliyewahi kuwa Waziri Kiongozi wa Serikali ya Zanzibar.

Kwa kweli alijibu vizuri kwa kusema kuna wanzanzibar kadhaa kwenye ngazi za juu ya jeshi letu (TPDF) katika ngazi ya Brigedier-General na wengine. Hivyo upo uwezekano japo hawezi kutamka rasmi kama itakuwa hivyo. Hadi hapo kwa hakika swali likawa limeisha.

Lakini Nahodha akaongezea kauli nyingine ambayo sidhani kama alipima matokeo yake. Akasema hata hivyo na yeye kama Nahodha anajua historia ya CHADEMA ambako hajawahi kusikia Mwenyekiti wa CHADEMA akitokea mkoa wa KIGOMA. Bunge zima likabaki linacheka. Kwani muuliza swali aliyekuwa anajibiwa ni Zitto kabwe na anatokea Kigoma.

Athari za jibu hili ni nini? Zitto aliipa Zanzibar uzito unaostahili katika uwiano wa mambo ya muungano. Kwa namna moja Zitto anaonyesha kwamba kuna usawa wa eneo wa iliyokuwa Tanganyika na usawa kwa eneo la Zanzibar. Hivi viwili ndivyo vinavyobidi kulinganishwa.

Sasa, Nahodha anapojibu swali kwa kulinganisha Zanzibar na Kigoma basi hii ni hoja yake na wala haikuwa mlinganisho wa Zitto Kabwe.

Maadam mlinganisho huu umetajwa na mzanzibar basi wazanzibar waache kulalamika wanapolinganishwa Zanzibar yote kama mkoa wowote wa bara. Maana ni ukweli kwamba Zanzibar inaingia zaidi ya mara tatu kwenye mkoa wa Mwanza kieneo na population.

Binafsi ninamshukuru sana mzanzibar huyu Shamsa Vuai Nahodha kwa ulinganisho huu, maana ingekuwa leo amesema mbara yaani m-tanganyika sijui upepo ungekuwaje mle bungeni na siajabu dakika hii ingekuwa ni mfululizo wa kuomba miongozo kwa spika kwa kitendo cha kuilinganisha Zanzibar na mkoa.

Shukurani sana Shamsa Vuai Nahodha.

Waziri Nahodha kafanya kosa la kiufundi kwa mzaha huo wa kitoto na litamgharimu kisiasa kwa sababu mzaha huo maana yake anakiri kwamba Zanzibar sio nchi ni mkoa mmojawapo tena mdogo tu katika jamhuri ya Tanzania unaoitwa kigoma. wazanzibari hawapendi nchi yao kuchukuliwa kama mkoa wa tanzania!! mizaha mizaha katika mambo ya msingi ni hatari sana!! sasa asubiri kishindo cha uamsho! alitakiwa apime athari ya mzaha wake kabla ya kutamka. pole Nahodha.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom