Zanzibar bila ya Tanganyika Inawezekana

Mwiba

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
7,607
1,744
Ukweli ni lazima usemwe ,Zanzibar bila ya Tanganyika inawezekana sana ,kuendelea kuwa na Muungano usioeleweka ni kujizidisha kuangamia katika dimbwi la umasikini , Mimi kama Mtanzania ningelipenda Muungano huu uliopo ujadiliwe upya na ikiwezekana ,tugawane mbao. Je wewe unasemaje ?
 
Ukweli ni lazima usemwe ,Zanzibar bila ya Tanganyika inawezekana sana ,kuendelea kuwa na Muungano usioeleweka ni kujizidisha kuangamia katika dimbwi la umasikini , Mimi kama Mtanzania ningelipenda Muungano huu uliopo ujadiliwe upya na ikiwezekana ,tugawane mbao. Je wewe unasemaje ?
Mkuu usiwe na wasi wasi juu ya hilo.Sasa hivi Tanganyika kichwa cha mwenda wazimu, nyie fanyeni vitu vyenu.
 
Tusubiri tuone nini kitatokea baada ya uchaguzi wa mwaka huu maana tumekwishaanza kupata taarifa za kuwa na serikali tatu kama mambo yakienda kama watu walivyopanga.Natamani sana kuiona serikali ya TANGANYIKA
 
Tusubiri tuone nini kitatokea baada ya uchaguzi wa mwaka huu maana tumekwishaanza kupata taarifa za kuwa na serikali tatu kama mambo yakienda kama watu walivyopanga.Natamani sana kuiona serikali ya TANGANYIKA

Naweza kusema kwamba wewe ni mtu wa kwanza kutumia neno tamani,kwa kweli huo ni ukweli wa ndani kabisa kuliko wale wengine wanaoonyesha kuweka kisasi iwapo watu watagawana mbao.

Kwa upande wangu Tanganyika bila ya Zanzibar ni vita vya wenyewe kwa wenyewe ,mtanganyika kumuuwa mtanganyika .
 
Naweza kusema kwamba wewe ni mtu wa kwanza kutumia neno tamani,kwa kweli huo ni ukweli wa ndani kabisa kuliko wale wengine wanaoonyesha kuweka kisasi iwapo watu watagawana mbao.

Kwa upande wangu Tanganyika bila ya Zanzibar ni vita vya wenyewe kwa wenyewe ,mtanganyika kumuuwa mtanganyika .

Bwana wewe ondoka kwa amani yako, ukiungana na Oman haya, na Comoro sawa miungano hii isiyo na tija imetudumaza miaka karibu 50.
 
Natamani kuiona Tanganyika na Watanganyika. Natamani nimsikie mtu akijiita mimi ni MTanganyika kama WaZanzibari. Hakuna cha MTanzania kuna MTANGANYIKA NA MZANZIBARI waZenj wanaufurahia uzanzibar wao, kwanini waTANGANYIKA hamuutaki utaifa wenu mnang'ang'ania uTanzania? Furahieni uTanganyika wenu bwana! Akah.
 
Mwiba said:
Kwa upande wangu Tanganyika bila ya Zanzibar ni vita vya wenyewe kwa wenyewe ,mtanganyika kumuuwa mtanganyika .

Mwiba,

..tayari wa-Tanganyika wanauana wenyewe kwa wenyewe. Hujafuatilia habari za Tarime, mauaji ya vikongwe na albino kanda ya Ziwa?

..Zenj haina influence yoyote ile kwa Tanganyika. kuna wa-Tanganyika kibao ambao hawana hata habari kwamba kuna muungano na nchi inaitwa Zenj. hiyo ndiyo sababu kubwa ya kutokusikia wananchi wakipiga kelele za kupinga muungano.

..kwa maoni yangu, serikali tatu itakuwa ni gharama zisizokuwa na lazima kwa wa-Tanganyika. fedha za kuendesha serikali hiyo, bunge lake, etc etc zinaweza kutusaidia kuboresha mambo mengine mengi ya msingi.
 
Mwiba,
Mkuu wangu mapenzi yako hayawezi badilisha mipango ya CUF na CCM.. Maadam wamefikia Muafaka inabidi kwanza kuua CCM Zanzibar na baraza la Mapinduzi kabla hujafikiria Zanzibar bila Bara..Na muhimu zaidi elewa kwamba Maalim Seif anajua fika kwamba pasipo Bara Zanzibar (Unguja) hawamuhitaji!
 
zanzibar bila muungano ni

uunguja na upemba ?

uzanzibari na uzanzibara?

mwarabu na mmatumbi ?

mzanzibari halisi na wakuja ?


tuwe realistic

huwezi jua thamani ya kitu hadi kikutoke
 
zanzibar bila muungano ni

uunguja na upemba ?

uzanzibari na uzanzibara?

mwarabu na mmatumbi ?

mzanzibari halisi na wakuja ?


tuwe realistic

huwezi jua thamani ya kitu hadi kikutoke
Mtu wa Pwani,
Sikujua kuna wakati unasemaga kitu cha maana.
 
Kila siku maneno yale yale na thread zile zile na kusema kweli inachosha. Bwana Mwiba Muungano hautavunjwa na WanaJF. DO yourself a favor na kawa fuate wenyewe nguvu za kufanya hilo ulitakalo. Go already and leave damn. Mumekuwa sasa kama mgeni ambae kila saaa ana sema jamani naondoka lakini kuondoka haondoki. Mgeni una subiria ubembelezwe ubaki? Mlango ule pale na mizigo yako hii hapa tutaonana kesho.
 
Mwiba,

..wagombea wa Uraisi wa Zanzibar wametamka kwamba watadumisha muungano.

..hizi chuki dhidi ya wa-Tanganyika ni jambo ambalo wanasiasa wa Zenj wanatumia kupata kura.
 
Ofcourse itawezekana kama wazanzibar wataacha uvivu, wachape kazi sio kukaa na kutegemea misaada toka arabuni.
Itawezekana kama ubaguzi kati ya Mpemba na Muunguja utaisha(in my opinion wapemba ni wachapa kazi zaidi)
Itawezekana kama mtagundua kuwa walio nyuma yenu mjitenge ni wachache wanaopenda madaraka.
Itawezekana kama mtawapeleka wanenu shule na vyuo sio skuli na madrasa tu.
Itawezekana kama mtaacha kujihisi nyie ni waarabu (nakumbuka kuitwa mwafrika niipokuwa hotel moja zanzibar)
Itawezekana kama mtaacha porojo za kupiga mahesabu ya kuishi kama brunei wakati hata kodi hamlipi.
Na mwisho Mungu awasaidie mpate mafuta kwenye eneo lenu maana karafuu sio dili tena.
 
Ukweli ni lazima usemwe ,Zanzibar bila ya Tanganyika inawezekana sana ,kuendelea kuwa na Muungano usioeleweka ni kujizidisha kuangamia katika dimbwi la umasikini , Mimi kama Mtanzania ningelipenda Muungano huu uliopo ujadiliwe upya na ikiwezekana ,tugawane mbao. Je wewe unasemaje ?

Wazanzibari wanatapatapa kwa sababu dhahabu, Tanzanite, almasi, nk wanavisikia kwenye bomba tu! Ndio maana wanajivunia mafuta ambayo mpaka sasa bado ni kitendawili! Hata hivyo mabadiliko ya 10 ya Katiba ya Zanzibar, 1984 inaongeza kipengele cha Tume ya Pamoja ya Fedha ya Jamhuri ya Muungano (kifungu cha 64 cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba hiyo ambayo yamebadilisha Ibara ya 124 (2)) ambapo Zanzibar itakuwa inamegewa 4.5% ya mapato ya Muungano, kwa hiyo watakuwa wanafaidika na tanzanite, almasi, dhahabu, nk kiaina!
 
Wazanzibari wanatapatapa kwa sababu dhahabu, Tanzanite, almasi, nk wanavisikia kwenye bomba tu! Ndio maana wanajivunia mafuta ambayo mpaka sasa bado ni kitendawili! Hata hivyo mabadiliko ya 10 ya Katiba ya Zanzibar, 1984 inaongeza kipengele cha Tume ya Pamoja ya Fedha ya Jamhuri ya Muungano (kifungu cha 64 cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba hiyo ambayo yamebadilisha Ibara ya 124 (2)) ambapo Zanzibar itakuwa inamegewa 4.5% ya mapato ya Muungano, kwa hiyo watakuwa wanafaidika na tanzanite, almasi, dhahabu, nk kiaina!
kabla ya kuwambia waZanzibari kuhusu hizo Tanzanite,almasi nk...wewe kama mTangayika umefaidika nazo kitu gani? umefika Mtwara ? nenda kawambie kama Tanganyika ina Tanzanite na almasi.... naona wako masikini kuliko kule Zanzibar...
 
muungano ni suala ambalo karibu ya wazanzibari na watanganyika wengi wenye kufikir kwa kutumia kichwa wanajua umuhimu wake


na pande zote wanakiri kuwa yapo mapungufu, tofauti niionayo:-

kila mtu anavyoangalia hayo mapungufu,

kila upande unaona wao wanaonewa na wenzao wanapendelewa

wanahisi ss hatunufaiki ila wale wananufaika

wanatofautiana jinsi ya kuondosha hizo tofauti, kila upande una mawazo yake juu ya jinsi gani ya kutatua hayo mapungufu


nn cha kufanya ?


mm nnaona kwa sasa ni kuwafahamisha wananchi kuhusu huu muungano, kwa nn tuliungana, wapi tumekwama, faida zipi zilitarajiwa na kwa nn hazipatikani.


hatua

baada ya hapo watushirikishe wananchi kwenye ngazi mbali mbali: wasomi wa sheria, wasomi wa uchumi, NGO's, wananchi wa kawaida na asasi nyenginezo wauzungumze muungano na kuuchambua na kutoa suluhisho ambalo litasaidia kuondoa tatizo


hapa pana hitaji uongozi jasiri ambao utakuwa tayari kuyasimamia haya, ila ukipatikana na ukakubali lolote lile hata ikisemwa waaasisi walikuwa wapumbavu ktk hili na lile tukubali na pale wanapostahiki tukubali


hata hivyo baada ya hapo matatizo yatatokea lkn tubuni utaratibu wa kuyashughulikia ikibidi
 
waachane wa znzbr wajitenge! alafu tubaki pembeni tukiwaangalia wakianza kubaguana wenyewe kwa wenyewe .. ! waachane wajiunge na OIC "kwani itawanufaisha kushinda muungano na tanganyika" kila mwaka kuna vijana wa tanzania wanaopelekwa uturuki kusoma fani mbalimbali bahati mbaya wadhamini wanachukuwa wa znzbr wengi kushinda watu wa bara, na hawakubali post graduate untill nchi iwe katika OIC!.. kama tunawapenda wa znzbr tuwaache! na mafuta yao "ndoto za alinacha" je wale wapemba waliojaa TEMEKE VIPI watarudi kwao?!! muungano ukifa? vijana wengi wa ki znzbr wanakimbilia bara wakisema znz hakuna cha kufanya. hakuna pesa, hakuna kazi.. ! lakini wanasiasa wao hawalioni hili...
 
kabla ya kuwambia waZanzibari kuhusu hizo Tanzanite,almasi nk...wewe kama mTangayika umefaidika nazo kitu gani? umefika Mtwara ? nenda kawambie kama Tanganyika ina Tanzanite na almasi.... naona wako masikini kuliko kule Zanzibar...

swali zuri!
 
Back
Top Bottom