sinza pazuri
JF-Expert Member
- Aug 16, 2014
- 2,525
- 7,377
Mudathir wakati yupo Azam FC alikuwa mwishoni wa mkataba wake akaenda kuzungumza na uongozi wa Azam kuhusu kuingia mkataba mpya na akataka kuongezewa mshahara.
Viongozi wa Azam FC na tajiri wao Yusuf Bakhresa wakamwambia sawa ila nenda tunajadili kisha tutakupigia simu. Baada ya muda akiwa kwao Zanzibar anaona taarifa imetolewa kuwa ameachwa.
Muda akaamua kukigeukia kilimo mpaka alipotafutwa na genius Injinia Hersi aende akakipige Yanga.
Kwa hiyo ushangiliaji wa Mudathir ni kwamba ameamua kuwapigia simu yeye mwenyewe mpaka wapokee. Wasipopokea tumekwisha.