Yussuf Makamba amwinda Reginald Mengi, yeye awataja mafisadi Papa rasmi!

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,020
Makamba amwinda Mengi



  • Ahoji safari za mikoani



Mwandishi Wetu Aprili 22, 2009

Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo


HUKU kukiwa na shinikizo la kutaka kumuondoa katika nafasi yake Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Yussuf Makamba, mwanasiasa huyo machachari, ametajwa sasa kumfuatilia Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni za IPP, Reginald Mengi.

Makamba ameelezwa kupendekeza ndani ya vikao vya chama hicho kuchunguzwa kwa uhusiano wa Mengi na wanasiasa waandamizi wa CCM wakiwamo wabunge, wengi wao wakiwa ni wale wanaofahamika kwa kuwa mstari wa mbele kupambana na ufisadi.

Habari za ndani ya vikao vya juu vya CCM vilivyofanyika Dar es Salaam mwishoni mwa wiki na baadaye mjini Dodoma, zinaeleza kwamba Makamba alitoa hoja hiyo katika vikao vya Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM na katika Kamati ya Maadili na Usalama ya chama hicho tawala.

Wakati Makamba akiwasilisha hoja hiyo, Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, alikuwa mmoja wa wageni wazito walioshiriki sherehe za miaka 75 ya kuzaliwa Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Mtera, John Malecela, mahali ambapo anaelezwa kusifia juhudi za wabunge wanaopinga ufisadi.

Miongoni mwa wabunge ambao Makamba anahisi wanaivuruga CCM wakiungwa mkono na Mengi ni pamoja na Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela, ambaye pamoja na kupongezwa na Kikwete kupata zawadi ya mwanamke shujaa, alikuwa mmoja wa washiriki wa sherehe ya kuzaliwa mumewe mwishoni mwa wiki, jijini Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine, Makamba anadaiwa kuhoji sababu ya Mengi kuingilia mambo ya CCM kwa kushirikiana na baadhi ya wanasiasa wa ndani ya chama hicho, hali ambayo Katibu Mkuu huyo wa CCM anaielezea ndani ya vikao kama inaashiria hatari kwa chama hicho siku za usoni.

Hatua ya Makamba kumgusa Mengi katika vikao rasmi vya chama, vimeelezwa kuwa sehemu ya mkakati maalumu wa kupunguza kasi kubwa ya mfanyabiashara huyo kuonekana akishirikiana na baadhi ya wabunge katika baadhi ya shughuli mbalimbali za kijamii, huku wakibainisha wazi kumuunga mkono Rais Kikwete.

Ingawa haijawekwa bayana lengo hasa la mapendekezo ya Makamba ni kuhoji pia hatua ya hivi karibuni ya Mengi kutoa misaada ya fedha kwa ajili ya kusaidia makundi mbalimbali ya kijamii kujiinua kiuchumi katika baadhi ya majimbo ya wabunge mbalimbali wa CCM bila kuyahusisha makao makuu ya chama hicho.

Mengi pia amekuwa mstari wa mbele katika vita ya ufisadi, vita ambayo inaungwa mkono na baadhi ya wabunge wa CCM akiwamo Anne Kilango - Malecela, ambaye hivi karibuni alitunukiwa Tuzo ya Mwanamke Jasiri na Serikali ya Marekani, kupitia ubalozi wake nchini.

Hata hivyo, habari zinaeleza kwamba hatua hiyo ya Makamba ni mkakati wa kujihami ama kulipiza kisasi kutoka kwa baadhi ya wanasiasa wakiwamo wabunge wanaopinga ufisadi ambao wamekuwa wakitaka kiongozi huyo kuondolewa katika nafasi yake kutokana na kushindwa kukisaidia chama hicho.

Tayari Makamba alitengwa katika kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Mbeya Vijijini, ambako CCM ilishinda baada ya kuelezwa kwamba kiongozi huyo wa CCM alikuwa chanzo cha chama hicho kushindwa katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Tarime.

Imefahamika kwamba sasa hata uchaguzi mdogo wa jimbo la Busanda, Makamba hatoshiriki kikamilifu, kukitolewa sababu kwamba ana majukumu mengi ya kitaifa na sababu nyingine za kiafya. CCM wanatarajiwa kumteua Lolesia Bukwimba, kuwania ubunge jimbo la Busanda.

Hayo yakiendelea, huko Mbeya, hali si shwari ndani ya chama hicho baada ya kuwapo mtafaruku miongono mwa viongozi wa CCM katika wilaya hiyo.

Katika moja ya matoleo yake, Raia Mwema ilikuwa na makala yenye kuelezea tahadhari iliyotolewa na wananchi wilayani Kyela kwa Rais Jakaya Kikwete kuhusu mwenendo wa kisiasa wilayani humo, sasa imedhihiri kwamba kilio cha wananchi wale kilikuwa ni cha kweli na kilipaswa kufanyiwa kazi na si kupuuzwa kama ilivyojidhihirisha.

Viongozi wa Chama cha Mapinduzi wilayani Kyela sasa wamefikia hatua inayoipeleka wilaya hiyo kwenye machafuko makubwa zaidi, kwani kitendo cha makatibu kata wanne wa Chama hicho kuwavamia viongozi wao wa Kamati ya Maadili ya Wilaya hiyo na kuwapiga wakitumia mateke na ngumi, kinazidi kuongeza chumvi kwenye kidonda.

Makatibu kata hao wanne wanaodaiwa kuwatwanga viongozi wao ni pamoja na Josephat Mwakajinga kutoka kata ya Kajunjumele, Grayson Mwaikambo wa kata ya Kyela mjini, Alex Mwaisombwa wa kata ya Lusungo na Ipyana Mwangunga ambaye ni Katibu Mwenezi wa kata ya Makwale

Hali ya kimazingira inaonyesha kuwa vurugu hizo zilimlenga zaidi Katibu wa Chama hicho wilayani Kyela, Maria Mwambanga ambaye kwa mujibu wa mjumbe mmoja wa Kamati ya Siasa ya Wilaya hiyo, inaelezwa kuwa wanataka kumuondoa kwa madai kuwa yuko upande wa Mbunge wa Jimbo hilo, Dk Harrison Mwakyembe.

Pamoja na madai hayo kuna taarifa vile vile kuwa Katibu huyo hatakiwi na baadhi ya viongozi wa chama hicho wilayani humo kwa madai kuwa hashindi ofisini na muda mwingi amekuwa akiutumia jijini Mbeya, hivyo kuunda genge la kumuondoa kwa nguvu.

Hata hivyo Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kyela, Japheth Mwakasumi anaelezea kushangazwa kwake na hatua ya makatibu kata hao kumvamia na kumpiga Mtendaji Mkuu wa Chama wilayani humo kwa madai yasiyo na kichwa wala miguu.

Dhamira yao wanataka mtu anayepokea mawazo yao, hapo ndipo ninaposhindwa kuwaelewa kwani si unayaleta kwenye vikao, ni wazi kuwa there is someone behind, maana miongoni mwa madai yao ni kwamba Katibu ni mtu wa Mbunge, kwa kweli siwaelewi, anaelezea kwa masikitiko Mwenyekiti huyo katika mahojiano maalumu na Raia Mwema.

Akizungumzia hali ya Katibu wake anasema sio nzuri na kwamba anaendelea na matibabu ikiwemo kupigwa picha.

Wee unafanya mchezo midume mizima inamshambulia mwanamke, hapana tumefika pabaya kama siasa zenyewe ndio hizi za majungu yasiyo na kichwa wala miguu halafu mnamshambulia mwamamke asiye na hatia, anazidi kushangaa Mwenyekiti huyo.

Aidha akizungumzia kinachoendelea ndani ya Chama hicho, Mwakasumi alisema kuwa Kamati ya Siasa ya Wilaya itaketi kesho Alhamis kulijadili suala hilo na kutoa maamuzi.

Hata hivyo, duru za ndani ya chama hicho wilayani humo zinabaisha kwamba vurugu hizo zilizosababisha Katibu huyo wa Wilaya kuumizwa vibaya, zinafadhiliwa na mmoja wa madiwani wilayani humo na kiongozi wa moja ya jumuiya za chama hicho mkoani Mbeya.

Ni wazi kwamba kwa taarifa hizo ni kwamba kuna kila dalili ya kuwepo kwa kambi mbili zenye mielekeo tofauti ya kisiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu mwakani.

Katika mahojiano na baadhi ya viongozi wa juu wa Chama hicho katika Wilaya ya Kyela pamoja na mkoani, wanazihusisha vurugu hizo moja kwa moja na harakati za kampeni za uchaguzi ujao mwakani na kwamba mbinu inayotumiwa na wafanya vurugu hao katika kukabiliana na Mbunge aliyepo haitofautiani na ile iliyotumika katika uchaguzi uliopita, kumtenganisha na uongozi wa juu wa chama hicho wilayani humo.

Katika mchakato wa kumpata mgombea ubunge wa Jimbo hilo kupitia CCM, viongozi wa juu wa wilaya wa Chama hicho hawakumtaka kabisa Mbunge wa sasa na badala yake waliegemea kwa Mbunge aliyekuwapo madarakani wakati ule, na hata Dk. Mwakyembe aliposhinda kwenye mchujo huo bado viongozi hao hawakumpa ushirikiano hivyo kutegemea zaidi nguvu ya wapiga kura ambako hadi sasa ndiko nguvu yake iliko.

Inaelezwa kuwa vurugu hizo za Jumamosi iliyopita zilitokea kwenye Kikao cha Kamati Maadili kilichoitishwa maalumu na kwa ajili ya kuwahoji baadhi ya makatibu kata, pamoja na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Wilaya hiyo, Visk Mahenge wanaotuhumiwa kuhusiana na vurugu zilizosababishwa na baadhi ya wajumbe wa Kikao cha Halmashauri Kuu ya Chama ya Wilaya hiyo Machi 31, mwaka huu.

Pamoja na tuhuma hiyo, Mwenyekiti wa Chama hicho Wilayani Kyela, Mwakasumi anaitaja tuhuma nyingine iliyokuwa wahojiwe makatibu hao ni kwa baadhi ya makatibu hao kudaiwa kuendesha kikao chenye mlengo wa kampeni za uchaguzi mwakani huku kikihusishwa na utoaji posho nje ya taratibu za chama hicho.

Wakizungumzia suala hilo la kampeni viongozi wa Chama hicho mkoani hapa walibaisha kuwa wanaelewa kuwepo kwa kampeni zinazoendelea chini kwa chini, lakini wakasisitiza haziwezi zikahalalishwa kuudharau uongozi uliopo madarakani kwani kwa kufanya hivyo ni kuruhusu vurugu na matumizi ya rushwa.

Mmoja wa viongozi wa chama hicho mkoani hapa alifikia hatua ya kusema, Kinachonisikitisha ni hatua ya baadhi ya viongozi waandamizi wa serikali kuchochea vurugu ndani ya chama wilayani Kyela, Katibu anatekeleza wajibu wake kwa kufuata kanuni na taratibu za chama zilizopo, hawezi kutoshirikiana na Mbunge wa jimbo la wilaya yake, hata kama mbunge ni kutoka chama cha upinzani bado angeshirikiana naye, ila tu asingeruhusiwa (mbunge wa upinzani) kuingia kwenye vikao vyetu vya chama, lengo ni maendeleo kwa wananchi na sio watu binafsi.

Moja ya matatizo yanayozikabili siasa za mkoa wa Mbeya ni kwa baadhi ya wanasiasa kuendelea kuishi katika ndoto za mtandao uliomwingiza madarakani Rais Jakaya Kikwete, wakiamini kwamba bado unazo nguvu zile zile za mwaka 2006 kurudi nyuma.

Pamoja Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya, Nawab Mulla kunukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari akielezea kuchukuliwa kwa hatua za nidhamu kwa waliosababisha vurugu hizo iwapo suala hilo litatuliwa nje ya mahakama, baadhi ya wanachama wameelezea kupingana naye katika hilo kwa maelezo kuwa Chama hicho siku hizi hakina uwezo huo wa kuwajibishana.

Wanautaja mgogoro ulioibuka kwenye kikao kimoja cha CCM Mkoa ambapo kiongozi mwanamke alitaka kumvalisha sidiria kiongozi mwenzake mwanaume kwa madai kwamba anaingilia mambo ya wanawake, lakini duru za kisiasa mkoani humo zikidai kuwa sababu hasa ni kutoungwa mkono kwenye kampeni zake kuwania uongozi wa juu wa chama hicho kwenye moja ya jumuiya zake.

Au ndio maana na Mengi leo kaamua kuwalipua mafisadi? Maana nasikia kwenye Press conference yake amewataja akina Rostam, Jeetu, Somaiya na Manji kuwa ndio mafisadi wakuu nchini

Invisible said:
Alichokiongea Mengi:

``Our country is currently facing a huge problem of corruption and is troubled by the fact that the people involved in acts of corruption do not what to be touched.
The resolve by our President, His Excellency Jakaya Mrisho Kikwete, to fight corruption and all other evils has shaken these people and they are now determined more than ever to combat all the people who are supporting the President in stopping further plunder of our country`s resources.

[ICODE]Tanzanians should know that people who are being accused of being corrupt in our country do not exceed ten, and out of the ten, five are being accused of being notoriously corrupt - corrupt sharks[/ICODE].

``These are: Rostam Aziz, Tanil Somaiya, Yusuf Manji, Jeethu Patel and Subash Patel.

These people are being accused of stealing billions of public money, and to make this worse, the billions have been transferred out of the country.

``These notoriously corrupt people are involved in almost all scandals that have happened in our country, including those concerning Richmond, EPA, Dowans, Army helicopters and vehicles, the Presidential Jet, Radar, NSSF, PSPF, National Lottery etc, etc.

``The great efforts of His Excellency the President to hasten economic development and better living for every Tanzanian are weakened by the horrendous theft of national resources.

A great majority of Tanzanians still face extreme poverty; they are unable to determine where the one meal a day is going to come from.

To make things worse, where a Tanzanian with better means provides assistance to lessen hardship within the society and to eradicate poverty, these people involved in corruption allege that such assistance has political agenda. They want Tanzanians to starve or die as a result of other problems.

``It seems that their aim now is to cause national havoc; it will not be surprising to learn that these people support what is behind DECI while Tanzanians remain chasing Pastors instead of asking themselves the real source of the havoc.

``These notoriously corrupt people are not only stealing our national resources; they are also stealing our precious time.

Instead of using our time for economic development we are using most of it to combat corruption.

``Our efforts have failed to even cause a dent; instead these corrupt people have been hardened in their determination.

They have established newspapers that are abusive and treat Tanzanians with contempt.

``They have created a scenario where the thief chases and attacks the person from whom he has stolen.

Even as Tanzanians continue to cry foul, the notoriously corrupt people continue to use their ill-obtained wealth to influence the granting of big contracts to them often in different names.

``Millions of Tanzanians are combating corruption, but there are a few who have come forward vehemently and are known by their names.

The notoriously corrupt people have been heard to say that they will annihilate these vehement combatants.

``The notoriously corrupt people should know that if the combatants are harmed in any way in this country or any other country, they will be answerable to the people of Tanzania.

``We Tanzanians must now ask ourselves - what gives these notoriously corrupt people the audacity to treat Tanzanians with contempt?

I would like to conclude by saying that all corrupt people and especially those who are being accused of notorious corruption must be dealt with conclusively, otherwise they will rock the stability of our nation. We must realise that we have now reached the stage when we must say enough is enough.

Mengi ataja mafisadi papa 2009-04-24

Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi, amewataja watu watano wanaotuhumiwa kuhusika na ufisadi mkubwa nchini na kuitaka serikali iwashughulikie haraka iwezekanavyo ili kuinusuru nchi kuyumbishwa nao. Watu hao, ambao Mengi alisema kwamba wanatuhumiwa kuwa ni mafisadi papa, ni pamoja na:

Mbunge wa Igunga na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CC-CCM) na Halmashauri Kuu ya Chama hicho (NEC-CCM) Taifa, Rostam .

Aliwataja wengine, kuwa ni wafanyabiashara, Tanil Somaiya, Yusuf Manji, Jeetu Patel na Subash Patel, ambao alisema wanatuhumiwa kuiba mabilioni ya wananchi na kuzihamishia nje ya nchi. `

Hawa wanatuhumiwa kuiba mabilioni ya fedha za wananchi, na baya zaidi fedha hizo zimehamishiwa nje ya nchi, alisema Mengi alipozungumza na waandishi wa habari katika Ofisi za IPP Limited, jijini Dar es Salaam jana na kuongeza: `…mafisadi wote na hasa wale wanaotuhumiwa kuwa mafisadi papa ni lazima washughulikiwe, la sivyo wataiyumbisha na kuitingisha nchi yetu.

Ni lazima Watanzania tuone kwamba sasa tumefika mahali pa kusema imetosha.`` Alisema watu hao ni kati ya watuhumiwa wasiozidi kumi wanaotuhumiwa kwa ufisadi mkubwa nchini na kuongeza kuwa wanahusishwa na karibu kila kashfa kubwa nchini, ikiwamo inayohusu kampuni hewa ya Richmond, ambayo ilitiliana saini na Shirika la Umeme nchini (Tanesco) mkataba tata wa kufua umeme wa dharura.

Kashfa nyingine, ambayo watu hao wanahusishwa nayo, alisema inahusu Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) kwenye Benki Kuu ya Tanzania (BoT), ambamo imethibitika kuchotwa Sh. bilioni 133 kwa njia za kifisadi na ile inayohusu kampuni ya Dowans Tanzania Limited, iliyorithi mkataba tata wa Richmond.

Nyingine, inahusu ununuzi wa helikopta na magari ya jeshi, ndege ya Rais, rada, Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mfuko wa Pensheni ya Watumishi wa Umma (PSPF), Bahati Nasibu ya Taifa na Mradi wa Makaa ya Mawe wa Mchuchuma. Alisema jitihada kubwa za Rais Jakaya Kikwete za kuleta maendeleo na maisha bora kwa kila Mtanzania, zimekuwa zikidhoofishwa na wizi mkubwa wa rasilimali za taifa, huku Watanzania wengi wakiandamwa na umaskini mkubwa, ikiwamo kutojua hata mlo mmoja kwa siku utatoka wapi. ``Chakusikitisha ni kwamba, pale Mtanzania mwema mwenye uwezo anaposaidia jamii kuondokana na umaskini, mafisadi wanapiga kelele kuwa misaada ya aina hiyo ina agenda.

Wanapinga, wanataka Watanzania wafe kwa njaa na matatizo mengine,` alisema Mengi. Alisema inavyoonekana, nia ya watu hao ni kutaka kuvuruga nchi na kwamba, si ajabu wakaunga mkono matatizo yanayotokana na kampuni ya Development Enterpreneurship Community (Deci) iliyokuwa ikichezesha mchezo wa upatu na Watanzania wakabaki wakifukuzana na wachungaji bila kujiuliza ni kina nani hasa wanachochea vurugu hizo. Mengi alisema ‘mafisadi papa, hawawaibii tu Watanzania rasilimali, bali wanawaibia pia muda.

Badala ya kutumia muda katika shughuli za maendeleo tunajikuta tukitumia muda mwingi kupambana nao, na hawatingishiki. Badala yake wanatumia fedha walizotuibia kuanzisha magazeti ya kujenga kiburi cha kutudharau, kututukana na kutunyanyasa. Inakuwa kesi ya mwizi kumkimbiza na kumpiga aliyeibiwa,` alisema Mengi. Alisema hata hivi sasa, mafisadi papa wanaendelea kutumia uwezo wao wa kiuchumi uliotokana na wizi wa rasilimali za nchi kushawishi na kupata miradi mikubwa mikubwa kwa kutumia majina tofauti tofauti, huku wakipuuza kabisa kelele za wananchi kuhusu ufisadi huo. Mengi alisema Watanzania wanaolia na ufisadi, ni mamilioni wakiongozwa na Rais Kikwete, lakini wapo wachache waliojitokeza na wanajulikana kwa majina.

Alisema zipo habari kwamba, wanaotuhumiwa kuwa mafisadi papa, wamedhamiria kuwatokomeza kabisa wanaopiga vita ufisadi wanaojulikana kwa majina. Kutokana na habari hizo, alisema: Mafisadi papa ni lazima wajue kwamba iwapo wapambanaji hao wa ufisadi watadhuriwa kwa njia yoyote hapa nchini au nje ya nchi, watawajibishwa na wananchi wa Tanzania. Aliongeza: ``Ni lazima Watanzania sasa tujiulize, hivi hawa mafisadi wanapata wapi

ujasiri wa majigambo, dharau na nguvu za kututukana na kutunyanyasa?`

` Awali, Mengi alisema nia njema ya Rais Kikwete ya kupambana na mafisadi na aina zote za uovu zimewashtua mafisadi na sasa wamecharuka na wanapambana na watu wote wanaomsaidia kupambana nao kuwazuia wasiendelee kuitafuna nchi. Rostam amekuwa akituhumiwa kuwa mmoja wa wamiliki wa kampuni ya Kagoda Agriculture Limited, inayodaiwa kuchota Sh. bilioni 40 kwenye EPA, tuhuma ambazo amekuwa akizikanusha. Shubash Patel anakabiliwa na sakata la kuchukua ardhi ya wanakijiji kwa njia za hila eneo ambalo kuna madini ya chuma, katika eneo la Mchuchuma, Iringa.

Tanil Somaiya anatajwa kuwa ni mshirika kwa mtuhumiwa wa ununuzi wa rada, Shailesh Prapji Vithlani ambaye tayari ana kesi katika mahakama ya Kisutu alikoshitakiwa bila kuwepo nchini. Katika sakata la rada, serikali ililizwa kiasi kikubwa cha fedha huku zaidi ya Dola milioni 12 zikiingia katika mifuko ya waliofanikisha ununuzi huo. Somaiya na Vithlani walikuwa wanamiliki kampuni nchini iliyohusika na kashfa hiyo.

Jeetu Patel kwa sasa ana kesi za EPA katika mahakama ya Kisutu zikihusu kampuni zake tano tofauti ambazo zilihusika kuchota mabilioni ya fedha kati ya Sh bilioni 133 zilizochotwa kifisadi.

SOURCE: Nipashe



Videos:



 
Makamba is a disgrace, of feeble mind, senile, and now like an unimaginative comedian out of jokes, is shooting himself in the foot, continuously, repeatedly.

His only salvation is the personal relationship he has with that other loser,Kikwete.

It is only a matter of time before they are both exposed for the corrupt failures that they truly are.
 
Au ndio maana na Mengi leo kaamua kuwalipua mafisadi? Maana nasikia kwenye Press conference yake amewataja akina Rostam, Jeetu, Somaiya na Manji kuwa ndio mafisadi wakuu nchini
 
Au ndio maana na Mengi leo kaamua kuwalipua mafisadi? Maana nasikia kwenye Press conference yake amewataja akina Rostam, Jeetu, Somaiya na Manji kuwa ndio mafisadi wakuu nchini

MN hebu malizia kuhusu hiyo press conference, alizungumzia nini hasa?
 
Huu ndio mwanzo wa mwisho wa ccm, mpaka sasa katibu mkuu ajuhi aanzie wapi, kwa kilango, kwa mwakyembe kwa sitta, kwa shelukindo na pia ana kazi ya kuhakikisha ni kikwete pake yake ndio anasimama kwa uraisi bila kuwa na upinzani wa maana.

Kwa kweli hii kazi ni ngumu sana kwa makamba hipo juu ya uwezo wake
 
MN hebu malizia kuhusu hiyo press conference, alizungumzia nini hasa?

Ndio, alikuwa na press conference ofisini kwake leo na ametoa statement ya kurasa mbili, nashangaa kuwa hili halijafika humu hadi saa hizi!

Katika statement yake amesema kuwa mafisadi wakubwa wanaoimaliza Tanzania hawazidi kumi. Na yeye akaamua kuwataja watano ambao amewaita 'mafisadi papa' - Rostam Aziz, Tonil Somaiya, Yusuf Manji, Subash Patel na Jeetu Patel.

Amesema hawa wanatuhumiwa kuiba mabilioni ya wananchi na mbaya zaidi fesha hizo wamezihamishia nje ya nchi.

Amesema wanaotuhumiwa kuwa 'mafisadi papa' wanahusishwa na kashfa kubwa zikiwemo Richmond, EPA, Dowans, helikopta na magari ya jeshi, ndege ya rais, rada, NSSF, NSPF, bahati nasibu ya taifa, mradi wa Mchuchuma na kadhalika.

Amesena jitihada kubwa za JK kuleta maisha bora kwa wananchi zinkwamishwa na hawa.

Amesena kuna uwezekano kuwa mabwana hawa naahusika pia na suala la DECI na si ajabu wakaunga mkono matatizo yanayotokana na DECI na watanzania wabaki wakifukuzana na wachungaji bila kujiuliza ni kina nai hasa wanachochea vurugu hizi.

kwa ufupi nawasilisha
 
Au ndio maana na Mengi leo kaamua kuwalipua mafisadi? Maana nasikia kwenye Press conference yake amewataja akina Rostam, Jeetu, Somaiya na Manji kuwa ndio mafisadi wakuu nchini
Hii list ya G4 we acha tu... Kawataja directly mkuu?

I see, basi kasheshe ipo!
 
Mhhhh.. hapa ngoma ina anza kunoga, ila inachanganya kwakweli.. Mengi ana nguvu gani? ama Mkulu kampa shavu amwage kuku tu kwenye mtama? wacha tusibili mwaya tutaona na kusikia mengi mwaka huu.
 
Mengi ana hasira nao tangu akose Kilimanjaro hotel oooh hataki hata kuwasikia hao mtandao na mafisadi...
 
..sasa CCM na Kikwete wamefadhiliwa na hao mafisadi kwa muda mrefu sana. mahusiano ya Rostam na Kikwete ya kuvuruga siasa za CCM na Tanzania kwa kutumia pesa na vyombo vya habari ni ya zaidi ya miaka 10.

..huu ufisadi ukiufuatilia[money trail] kwa jinsi ambavyo wenzetu wa magharibi wanaufuatilia unaweza kufikia conclusion kwamba CCM na Jakaya Kikwete walikiuka sheria za Jamhuri ktk harakati zao za kutafuta madaraka.

..CCM na Raisi Kikwete wanapaswa kuueleza umma kwamba katika uhai wa chama chao wamepokea fedha kiasi gani toka kwa mafisadi waliotajwa na wengine wanaohisiwa kwa ufisadi.

..nakumbuka Barack Obama alirudisha fedha alizochangiwa na yule rafiki yake mtuhumiwa wa ufisadi. ingekuwa vizuri kama Raisi Kikwete na CCM watarudisha fedha zote walizochangiwa na hawa mafisadi. huo ndio uungwana.
 
Kazi kweli kweli;mzee kaamua....yumo manji;PATEL FAMILLY.RICHMOND NK///
 
Mama Mia sikiliza hiyo habari ikifika muda halafu utupostie hapa atakaowataja!..Tupate kujua na sie
 
Mama Mia sikiliza hiyo habari ikifika muda halafu utupostie hapa atakaowataja!..Tupate kujua na sie

no p bellinda jacob..ntakupostia kwanza hongera kwa kujiita jina kamili
 
[B said:
no p bellinda jacob..ntakupostia kwanza hongera kwa kujiita jina kamili[/B]

Asante sana Mama Mia!..Naamini unaupenda huo wimbo na movie yake(abba)..

Saa mbili na nusu imepita au bado ni anatoa introduction?!
 
Mfanyabiashara maarufu Reginald Mengi ajitoa mhanga kwa mafisadi

Boniface Meena na Mkinga Mkinga

MFANYABIASHARA maarufu nchini, Reginald Mengi jana aliamua kujitoa muhanga alipotangaza majina ya wafanyabiashara watano wenye asili ya Kiasia ambao anadai kuwa ni mafisadi papa wanaoiba mabilioni ya fedha za wananchi na kutaka wachukuliwe hatua kwa madai kuwa wataiyumbisha na kuitingisha nchi.

Kati ya wafanyabiashara waliotajwa na Mengi, wawili wamefunguliwa mashtaka ya tuhuma za wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), wengine wakiwa wameshatajwa kwenye kashfa mbalimbali, zikiwemo za zabuni ya utoaji umeme wa dharura ya Richmond Development na uuzwaji wa jengo la Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Mengi, ambaye anamiliki kampuni ya IPP yenye kampuni mbalimbali zikiwemo za habari na vinywaji, alitaja wafanyabiashara hao watano akisema kuwa ndio papa kwa ufisadi lakini akasema idadi ya mafisadi wanaofilisi nchi hawazidi 10.

"Wanaotuhumiwa kuwa mafisadi papa wanahusishwa na karibu kila kashfa kubwa hapa nchini zikiwepo kashfa za Richmond, EPA, Dowans, helikopta na magari ya jeshi, ndege ya rais, rada, NSSF, Bahati Nasibu ya Taifa, mradi wa makaa ya mawe wa Mchuchuma na kadhalika," alidai Mengi katika mkutano wake na waandishi wa habari alioufanya kwenye ofisi yake jijini Dar es salaam.

Kati ya wafanyabiashara hao watano ambao Mengi alidai ni mapapa wa ufisadi, wamo Rostam Aziz, Yusuf Manji na Jayantkumar Chandubhai Patel (Jeetu Patel), ambao Mwananchi ilipata nafasi ya kuzungumza nao kuhusu tuhuma hizo za Mengi.

Hata hivyo, Mengi hakuwa tayari kutoa vielelezo kuthibitisha madai yake, lakini akasema iwapo watamshtaki mahakamani na wafanye hivyo kwa kuwa huko ndiko haki inakopatikana.

Mengi alirusha tuhuma nyingi kwa watu hao ambao alidai kuwa wamecharuka baada ya Rais Jakaya Kikwete kuamua kupambana nao na hivyo wameamua kupambana na yeyote anayemsaidia mkuu huyo wa nchi katika vita hiyo.

"Jitihada kubwa za Mhe. Rais za kuleta maendeleo na maisha bora kwa kila Mtanzania zinazoofishwa na wizi mkubwa wa rasilimali za taifa. Bado Watanzania wengi wanaandamwa na umaskini mkubwa; hawajui hata mlo mmoja kwa siku utatoka wapi," alidai Mengi ambaye pia alitoa taarifa ya maandishi aliyoisaini.

"Cha kusikitisha ni kuwa pale Mtanzania mwema mwenye uwezo anaposaidia jamii kuondokana na umasikini, mafisadi wanapiga kelele kuwa misaada ya aina hiyo ina agenda. Wanapinga kwa kuwa wanataka Watanzania wafe na njaa na matatizo mengine."

Mengi alikwenda mbali zaidi na kudai mafisadi anaowatuhumu wanaweza wakaunga mkono matatizo yanayotokana na Deci, taasisi inayoendesha mchezo wa kuchangisha fedha na kulipa maradufu na Watanzania kubakia "wakifukuzana na wachungaji bila ya kujiuliza ni kina nani hasa wanachochea vurugu".

Wakiongea na Mwananchi, watu hao wanaotuhumiwa kwa ufisadi hawakutaka kujibu kwa kirefu na badala yake walimtuhumu mwenyekiti huyo mtendaji wa IPP kuwa ana wivu, fitina chuki na ambaye ameshindwa kuendesha nyumba na biashara zake, huku mwingine akieleza kuwa anatumia haki yake ya kidemokrasia ya kutoa maoni yake.

"Mengi... (si mstaarabu)," alisema Manji ambaye anamiliki kampuni ya Quality Group. "Nyumba yake imemshinda na biashara zake zimemshinda ndio maana anazungumza ujinga."

Rostam Aziz, ambaye ni mbunge wa Igunga anayejishughulisha na biashara mbalimbali za miradi mikubwa ya ujenzi, uchimbaji na habari, alimuelezea Mengi kama mtu ambaye analingana kwa umri na baba yake mzazi na hivyo hawezi kubishana naye.

Lakini akasema: "Mengi amejaa chuki, wivu na fitina. Sina cha kumsaidia isipokuwa kumuombea Mungu ili amsaidie kwa kumpuuzia hayo maana ni adhabu kwa nafsi yake mwenyewe. Kwa malezi niliyopata, siwezi kubishana na mzee."

Jeetu Patel naye alisema haoni busara kujibizana na Mengi na kwamba alichofanya mwenyekiti huyo wa Chama cha Wafanyabiashara Wenye Viwanda (CTI) ni kutumia haki yake ya kidemokrasia ya uhuru wa kuongea.

“Hayo ni matatizo yake," alisema Patel, ambaye anakabiliwa na kesi ya tuhuma za wizi wa fedha za EPA. "Amewaita waandishi kuzungumza nao... sikumsikia lakini ninachoweza kusema ni kwamba anatumia uhuru wake wa kujieleza.

“Binafsi sijui chochote kuhusu hizo tuhuma za Mengi dhidi yangu, ila anayo haki ya kusema chochote. Nina mambo mengi ya kufanya hivyo sioni kama itanisaidia kwenye biashara zangu za kila siku kuanza majibizano na Mengi.”

Katika mkutano wake na waandishi wa habari, Mengi alidai kuwa watu hao aliowataja si tu kwamba wanaiba rasilimali za Tanzania, bali pia wanaiba muda wa Watanzania.

"Badala ya kutumia muda katika shughuli za maendeleo, tunajikuta tukitumia muda mwingi kupambana nao na hawatingishiki," alidai Mengi. "Badala yake wanatumia fedha walizotuibia kuanzisha magazeti ya kujenga kiburi cha kutudharau, kututukana na kutunyanyasa. Inakuwa kesi ya mwizi kumkimbiza na kumpiga aliyeibiwa.

"Hata sasa hivi, mafisadi papa wanaendelea kutumia uwezo wao wa kiuchumi uliotokana na wizi wa rasilimali za nchi yetu kushawishi na kupata miradi mikubwa mikubwa kwa kutumia majina tofauti tofauti huku wakipuuza kabisa kelele za wananchi kuhusu ufisadi wao.

Alisema ni muhimu wananchi wakajiuliza hawa mafisadi wanapata wapi ujasiri wa majigambo, dharau na nguvu za kutukana na kunyanyasa watu.

Alisema mafisadi papa ni lazima wajue kwamba iwapo wapambanaji wa ufisadi watapata madhara kwa njia yoyote hapa nchini au nje ya nchi, wananchi wa Tanzania watawawajibisha.

"Ni lazima Watanzania wote tuone kwamba sasa tumefika mahali pa kusema imetosha," alidai Mengi.


***************************************************
Je, hii Press Conference ni majibu ya kile kilichojadiliwa kwenye kikao cha Sekretariati ya CC?

Tayari watuhumiwa 3 wameonyesha kugwaya kwenda mahakamani, what is the appropriate next move?

Maana naona hii ya kuwataja peke yake haitoshi na kwa kuwa hawawezi kwenda mahakamani mambo yanaishia kwenye magazeti na TV tu na mwisho wa siku hawa mafisadi wanaendelea kudunda mtaani. Kwa wataalam wa sheria, hivi hakuna uwezekano wa raia wa kawaida kuwashitaki hawa watu akiwatuhumu kwamba ni mafisadi? Ama ndo mpaka mtu apate kibali cha Feleshi ambaye amekuwa akiandaa mashitaka mepesi yasiyo na nguvu sana?
 
Back
Top Bottom