Yote haya ni matokeo ya upinzani dhaifu...?

Fortilo

JF-Expert Member
Apr 10, 2012
4,722
14,248
katika historia ya tanzania, upinzani umemark miaka ishirini hivi tangu uanzishwe rasmi., tofauti na matarajio ya wengi, kwamba angalau vitendo vya rushwa, matumizi mabaya au yasiyo ya lazima ya pesa za walipa kodi, kutoaminiana miongoni mwa jamii, uzembe wa kutoa huduma za msingi kwa jamii, tatizo la ajira, yote hayo yamekuwa yakiongezeka, hil halina ubishi.

Sasa wadadisi wa mambo hata wananchi wa kawaida wamepoteza imani kubwa na upinzani kwa mising ifuatayo;

mosi, baadhi ya viongozi wa upinzani kungangania madaraka, na kugombea nafasi za juu wao wenyewe tu..

pili, baadhi ya viongoz wa upinzani kujihusisha na vitendo vya rushwa hasa wabunge, na pengine kuzitetea hasa wale wanaohusishwa nazo moja kwa moja, mf. nishati na madini, na wakat mwingine kuwakatisha tamaa wapambanj hawa hawa kukubali kuendesha magari ya kifahari wakati wao wenyewe wanayapinga majukwaani kwa nini wasikatae vitendo hivi kama sio mawakili wa siasa uchwara na siasa njaa zinazoitafuna nchi yetu kila uchao?

MWENYE MACHO HAAMBIWI TAZAMA.
 
Upinzani hawana dola! hawakusanyi kodi! kazi yao ni kushauri na kutoa sera mbadala na kuwaamsha watu.kusema ukweli bila upinzani hasa wa CDM kuanzia 2005 hii nchi ingekuwa imeshauzwa kitambo.

Sema tuna rais Dhaifu! Serikali legelege! na upuuzi wa bunge under majority ya wapenda posho,rushwa,wanaolala hovyo kutoka chama tawala cha CCM.
 
Like father like son!Suluhisho la matatizo yetu ni katiba iliokali na straight foward juu ya mambo ya msingi kama muundo/mfumo wa serikali, matumizi ya rasilimali za umma na uwajibikaji.Wala sio nanni kakaa Magogoni.Nikikumbuka wakati Kikwete anachaguliwa 2005 TULIKUA NA MATUMAINI SANA.Angalia miaka kumi sasa, tuko wapi??????
Anayonia ya dhati kabisa ila mfumo alioukuta kuubadili bsio rahisi, sisi wananchi tuubadili kupitia KATIBA MPYA.
Wapinzani njaa tu, watatupigisha MARK TIME na hatuna muda wakupoteza tena INATOSHA 50yrs, mchawi ni katiba.
 
Inawezekana una hoja ya msingi, ila hukuweza kuijenga vizuri. Huwezi kuulaumu upinzani ndani ya nchi hii kwasababu tu ya udhaifu na uovu wa serikali!
 
katika historia ya tanzania, upinzani umemark miaka ishirini hivi tangu uanzishwe rasmi., tofauti na matarajio ya wengi, kwamba angalau vitendo vya rushwa, matumizi mabaya au yasiyo ya lazima ya pesa za walipa kodi, kutoaminiana miongoni mwa jamii, uzembe wa kutoa huduma za msingi kwa jamii, tatizo la ajira, yote hayo yamekuwa yakiongezeka, hil halina ubishi.

Sasa wadadisi wa mambo hata wananchi wa kawaida wamepoteza imani kubwa na upinzani kwa mising ifuatayo;

mosi, baadhi ya viongozi wa upinzani kungangania madaraka, na kugombea nafasi za juu wao wenyewe tu..

pili, baadhi ya viongoz wa upinzani kujihusisha na vitendo vya rushwa hasa wabunge, na pengine kuzitetea hasa wale wanaohusishwa nazo moja kwa moja, mf. nishati na madini, na wakat mwingine kuwakatisha tamaa wapambanj hawa hawa kukubali kuendesha magari ya kifahari wakati wao wenyewe wanayapinga majukwaani kwa nini wasikatae vitendo hivi kama sio mawakili wa siasa uchwara na siasa njaa zinazoitafuna nchi yetu kila uchao?

MWENYE MACHO HAAMBIWI TAZAMA.

Pole sana, mada yako umeijenga katika msingi wa tope!
 
katika historia ya tanzania, upinzani umemark miaka ishirini hivi tangu uanzishwe rasmi., tofauti na matarajio ya wengi, kwamba angalau vitendo vya rushwa, matumizi mabaya au yasiyo ya lazima ya pesa za walipa kodi, kutoaminiana miongoni mwa jamii, uzembe wa kutoa huduma za msingi kwa jamii, tatizo la ajira, yote hayo yamekuwa yakiongezeka, hil halina ubishi.

Sasa wadadisi wa mambo hata wananchi wa kawaida wamepoteza imani kubwa na upinzani kwa mising ifuatayo;

mosi, baadhi ya viongozi wa upinzani kungangania madaraka, na kugombea nafasi za juu wao wenyewe tu..

pili, baadhi ya viongoz wa upinzani kujihusisha na vitendo vya rushwa hasa wabunge, na pengine kuzitetea hasa wale wanaohusishwa nazo moja kwa moja, mf. nishati na madini, na wakat mwingine kuwakatisha tamaa wapambanj hawa hawa kukubali kuendesha magari ya kifahari wakati wao wenyewe wanayapinga majukwaani kwa nini wasikatae vitendo hivi kama sio mawakili wa siasa uchwara na siasa njaa zinazoitafuna nchi yetu kila uchao?

MWENYE MACHO HAAMBIWI TAZAMA.
ni kweli kabisa muwasilishaji nakuunga mkono asilimia mia kwa mia lakini awali naomba nikuulizwe haya:-
1. hv uchaguzi wa ndani unaondelea wa CCM tumeshudia rushwa iliyokithiri mpaka rais akikiri uwepo wa Rushwa hapo utasemaje?

2. Hv wale mawaziri wawili kutoka wizara moja waliolumbana kisa naibu katolewa out na kampuni ya CCCC ni wanatoka upinzani?
 
Hivi tuhuma za rushwa uchaguzi BAVICHA zilikuwa ni sehemu ya kiwanda cha uongo au bado babu anafanya upembuzi yakinifu?
Tusilikia mengi na vielelezo kubainishwa hatimae kombe limefunikwa na mwana wa haramu amepatikana si kupita tena.
 
Mi nadhani matokeo unayaona ni kutokana UJINGA wa watanzania walio wengi baadhi yao wakilewa fedha za ufisadi. Hata humu jamvini wamejaa wakitetea ufisadi na watawala wasiojali maslahi ya Taifa letu.
 
Watu wanabeza bure tu sasa. Iwapo hapo juu si hoja ni kipi sasa cha kujadilika hapa JF?! Jamani, mbona tunatanguliza kebehi kwa kila tusichokubaliana nacho? Mheshimiwa saana hapo juu kaleta hoja ya kwamba - iwapo upinzani unamiaka 20 sasa tangu urudi, ni kipi kimeufanya bado uonekane 'dhaifu' machoni pa wengine... na tumjibu kwa hoja basi ili kuelewesha jamii kwa ujumla. Ahsanteni.
 
Back
Top Bottom