Yesu si Mungu, Paulo ana kesi ya kujibu

Status
Not open for further replies.
sio kwamba haelewi maandiko,bali unamtaka ayaelewe unavyoelewa wewe na asihojihoji zaidi,
pia umetoa maelezo yako na unahisi maelezo yako ndio final,
sasa anakwambia lete ushahidi,hakubaliani na maelezo yako
Hakuna mahali nimemtaka akubaliane na mimi, mimi namueleza msingi wa imani ya kikristo ulipo, labda yeye aniambie anataka jibu gani!!.

Hili ni tatizo la kuuliza swali ukiwa na majibu yako kichwani.anataka ushahidi wa maandiko, akiletewa anasema bible haijashushwa hivyo haamini.
 
Hakuna mahali nimemtaka akubaliane na mimi, mimi namueleza msingi wa imani ya kikristo ulipo, labda yeye aniambie anataka jibu gani!!.

Hili ni tatizo la kuuliza swali ukiwa na majibu yako kichwani.anataka ushahidi wa maandiko, akiletewa anasema bible haijashushwa hivyo haamini.
sio wakristo wote wanaamini yesu ni mungu?,labda wawe wameanza kuamini mwezi uliopita
 
Wewe acha matumizi ya ubongo wa samaki,

Unashangaa Mungu kupigwa katika umbo la mwili!!!, na kudhihakiwa.unapotenda kinyume na matakwa yake sasa hivi, anakufanyaje ilhali anauwezo wa kukugeuza ngisi kwa tamko tu na ukaliwa????

Nyie watu hata upeo wenu una mashaka kidogo, unashindwaje kuona logic kwa jambo dogo kama hili????
Acha utoto wewe kama kweli yeye mungu mbona alivyokuwa msalabani akasema mungu wangu mungu wangu mbona umeniacha kama yeye ni mungu na huyu aliye kuwa anamlalamikia ni nani?nikuongeze kitu kingine mungu gani anakaa tumboni miez 9,anakula anakunywa a naenda haja dah .umeharibiwa akili na vitabu walivyotunga wajanja.lete hoja nikuelewa Acha kufikiri kwa ma kalio ww aafu unakuja hapa kutokwa povu we unaona umejiiibu Acha uk******laza
 
Acha utoto wewe kama kweli yeye mungu mbona alivyokuwa msalabani akasema mungu wangu mungu wangu mbona umeniacha kama yeye ni mungu na huyu aliye kuwa anamlalamikia ni nani?nikuongeze kitu kingine mungu gani anakaa tumboni miez 9,anakula anakunywa a naenda haja dah .umeharibiwa akili na vitabu walivyotunga wajanja.lete hoja nikuelewa Acha kufikiri kwa ma kalio ww aafu unakuja hapa kutokwa povu we unaona umejiiibu Acha uk******laza

Sikushangai hizi ni akili sampuli ya mohamed kabisa hizi.

Huu uzi uko posti ya ngapi, tuko tunafafanua haya maswali yako ya watoto wa sundayschool husomi uelewe, badala yake unakuja kuquote baba zako kihunihuni tu.

Haya rudi kaanze upya.
 
sio wakristo wote wanaamini yesu ni mungu?,labda wawe wameanza kuamini mwezi uliopita
Sasa kama ukristo kwake ni kuitwa john na kwenda kanisani!!!!, huyu hata ukikaa naye atakueleza nini cha maana, zaidi ya kukusifu kwa kuruhusiwa kuoa wake wengi?!!????
 
Nawaza tu
1. Kwa kuwa Yesu ni Mungu na Mungu huyo alizaliwa na bikira Maria basi nathubutu kusema bikira Maria ni mkubwa kuliko Yesu(Mungu) maana mtoto kwa mama atabaki kuwa mtoto tu. Hivyo utukufu wa juu kabisa ni wake Maria maana ndo aliyemzaa Mungu wenu.

2. Kwa mujibu wa maandiko yenu, Yesu alikufa na siku ya tatu akafufuka. Hiyo ina maana kuwa dunia ilikaa siku 3 bila Mungu. Je nani aliiongoza dunia kwa muda huo wa siku 3?

4. Ninavyofaham uwezo wa Mungu hauna limit, ana uwezo wa kujua ya jana ,leo na kesho, hivyo Yesu(kama kweli ni Mungu) kabla ya ujio wake duniani alishaona kitakachomtokea. Kwani alikubali kuja kudhalilika? Kwanini aliionesha dunia kuna watu wana uwezo zaidi yake (waliomtesa msalabani) ilhali ye ni Mungu muweza wa yote.

3. Kama kweli yeye Yesu ni Mungu kwanini alikuja dunian? Kwanini alishindwa kuuumba kiumbe chenye uwezo wa kufanya hiyo kazi iliyomleta yeye duniani? Haoni kuwa kitendo cha yeye kuja duniani na kuteswa kama viumbe wengine dhaifu kimechangia kupunguza imaani kwa baadhi ya watu (mfano Mimi siamini kabisa Mungu muweza wa yote anaweza kuteswa na kiumbe alichokiumba mwenyewe)
Maswali ni mengi lkn acha niishie hapa
 
Ulitaka auite ufalme wake dogo au bro????
Haya bwana na mungu wenu anayeuchapa usingizi hadi wanafunzi wanataka wafe baharini sasa sijui wakati mungu amelala nani alikuwa anaongoza ulimwengu, halafu Waisrael Noma sana yani hawamtaki mungu wao wanamtaka barabaaaa.
 
Haya bwana na mungu wenu anayeuchapa usingizi hadi wanafunzi wanataka wafe baharini sasa sijui wakati mungu amelala nani alikuwa anaongoza ulimwengu, halafu Waisrael Noma sana yani hawamtaki mungu wao wanamtaka barabaaaa.
Wewe mwenyewe unamkana sjui unamtaka nani????
 
View attachment 406746

"Lakini sasa mnatafuta kuniua mimi, MTU ambaye nimewaambia iliyo kweli, niliyoisikia kwa Mungu. Ibrahimu hakufanya hivyo."

Yohana 8:40

Katika andiko hilo YESU kwa kinywa chake yeye mwenyewe amejiita kuwa ni "MTU". Kama kuna mtu ana ushahidi wowote katika biblia YESU akijiita MUNGU, basi nami hapo nitaamini kuwa YESU Mungu.

Hata hivyo, mnaweza kusema pia, kuwa YESU alikuwa Mungu na Pia alikuwa mtu. Hata hivyo tukitazama sifa mbalimbali za mungu kama zilivyo tajwa au ainishwa na biblia, utaona hata kiduchu YESU hana sifa hizo.

Mathalani.

"Mungu si mtu, aseme uongo; Wala si mwanadamu, ajute; Iwapo amesema, hatalitenda? Iwapo amenena, hatalifikiliza.."

Hesabu 23:19

Tumeona katika Yohana 8:40 Yesu akijiita Mtu, na hapa katika hesabu tunaambiwa Mungu si mtu, sasa wewe unayemuita Yesu Mungu umepata wapi?

NANI KAFUNDISHA YESU NI MUNGU?

"tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu; "

Tito 2:13

Hayo maneno katika kitabu cha Tito, kimsingi ni barua ya kimisionari aliyo andika Paulo kwa watu wa Tito, kama tuonavyo katika barua hiyo, pamoja na mambo mengine Paulo anawaambia watu wa Tito kuwa Yesu ni Mungu Mkuu, maneno haya ya Paulo yanakwenda kinyume kabisa na maneno ga Yesu mwenyewe aliyo yasema katika Yohana 8:40 lakini kinyume kabisa na mafundisho ya kinabii kutoka katika kitabu cha Hesabu 23:19.

YESU ANASEMAJE KUHUSU PAULO?

Awali ya yote Paulo hakuwahi kuwa mwanafunzi wa Yesu na hakuwahi kumuona Yesu Kristo. Yesu kabla hajapaa kwenda mbinguni aliwahi kusema maneno haya.

"Maneno hayo nimewaambia, msije mkachukizwa. Watawatenga na masinagogi; naam, saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada. Na hayo watawatenda kwa sababu hawakumjua Baba wala mimi"

Yohana 16:1-3

Hapa Yesu anatabiri kuwa wanafunzi wake watakuja kuuliwa, anatabiri wakristo na wafuasi wa kanisa lake watakuja kuuliwa, na akasisitiza huyo atajaye wauwa wanafunzi wake hamjui yeye wala Baba(Mungu)

Nani huyo aliyeua wanafunzi wa Yesu? Jawabu ni Sauli ambaye ni Paulo.

"Lakini Sauli, akizidi kutisha na kuwaza kuwaua wanafunzi wa Bwana, akamwendea Kuhani Mkuu, akataka ampe barua za kuenda Dameski zilizoandikwa kwa masinagogi, ili akiona watu wa Njia hii, waume kwa wake, awafunge na kuwaleta Yerusalemu."

Matendo 9:1-3

Kwa hivyo Mtu aliyetajwa na Yesu katika injili ya Yohana 16:1-3 kuwa atawaua wanafunzi wa Yesu si mwingine Paulo, na katika kitabu cha matendo tunaoneshwa ukatili wa Paulo kwa wanafunzi wa Yesu. Hata hivyo, Bwana Yesu anaendelea na utabiri wake juu ya Paulo katika aya hii.

"Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo"

Yohana 8:44

Katika aya hiyo Bwana Yesu anasema huyo Paulo si kwamba ni muuaji tu, lakini pia mtu muongo sana. Na uongo mkubwa alio ufanya Paulo ni pale aliposema kakutana na Yesu na kisha akajifanya kipofu.

"Hata alipokuwa akisafiri, ikawa anakaribia Dameski; ghafula ikamwangaza kote kote nuru kutoka mbinguni. Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Sauli, Sauli, mbona waniudhi? Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe. Lakini simama, uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda"

Matendo 9:3-7

Baaada ya Paulo kuwaua sana wanafunzi wa Yesu na kuwatesa sana ili waache mafunzo ya Yesu, lakini wanafunzi wa Yesu waligoma na walikataa katakata kuachana na mafunzo Yasu. Pia naomba mjue, mafunzo ya Yesu yalikuwa mwiba kwa serikali(Dola ya Rumi) na Paulo alikuwa anatumiwa na serikali katika kuhakikisha wanafunzi wa Yesu wanaachana na ukristo/uyaudi.

Pamoja na juhudi hizo za Paulo lakini alishindwa, hivyo njia aliyo amua kuitumia si nyingine bali ni kujiunga na wanafunzi wa kristo. Na ili aaminike ndipo hapo alipotengeneza stori ya kumuona Yesu na maagizo ya upofu, lakini kubwa zaidi alimnunua Anania ili msaidie kufanikisha lengo lake. Kwa kumtumia Anania na kwa kudanganya kwake kuwa kamuona Yesu, wanafunzi wa Yesu walimkubali.

Na hapo ndipo Paulo alipoanza kuyachakua mafunzo ya Yesu, na ndio maana ukristo wa sasa si ule alio ufundisha Yesu.

YESU NA MFARISAYO.

"Ewe FARISAYO KIPOFU, safisha kwanza ndani ya kikombe, ili nje yake nayo ipate kuwa safi. Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mmefanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, nayo kwa nje yaonekana kuwa mazuri, bali ndani yamejaa mifupa ya wafu, na uchafu wote."

Mathayo 26:23

Paulo msomi mkubwa alikuwa Farisayo, lakini Yesu alisema nini juu mafarisayo? Kama tulivyo ona, Yesu anawaona mafarisayo kama vipofu, lakini kubwa katika andiko hili Yesu anamtabiri pia Paulo na maigizo yake ya upofu.

"Paulo alipotambua ya kuwa sehemu moja ni Masadukayo, na sehemu ya pili ni Mafarisayo, akapaza sauti yake katika ile baraza, Ndugu zangu, mimi ni Farisayo mwana wa Farisayo; mimi ninahukumiwa kwa ajili ya tumaini la ufufuo wa wafu"

Matendo 23:6

Kwanza Paulo amekiri kwa kinywa chake kuwa yeye ni farisayo. Lakini hiyo haitoshi Paulo alijitia upofu aso kuwa nao.

"Sauli akainuka katika nchi, na macho yake yalipofumbuka, hakuona kitu; wakamshika mkono wakamleta mpaka Dameski. Akawa siku tatu haoni; hali, wala hanywi."

Matendo 9:8-9

Katika aya hizi tunaona kuwa Paulo amekiri kuwa Farisayo lakini pia tunaona Paul yuko katika maigizo ya upofu. Yote haya mawili yanakamilisha unabii wa Yesu pale aliposema

"Ewe farisayo kipofu.."

Mathayo 26:23

Katika aya hizo inatajwa sifa kuu au tabia kubwa ya Mafarisayo, na ambayo imethibiti(ilitimia) kwa Paulo. Sifa hiyo si nyingine bali UNAFIKI.

Paulo alikuwa mnafiki, yaani alijifanya muumini wa mafundisho Yesu ili mradi apate kuwapotosha wanafunzi wa Yesu, na hili kwakweli kafanikiwa sababu hakuna hata kanisa moja ambalo linafuata mafunzo ya asili ya Yesu. Kila kanisa lina kituko chake.

MWISHO.

Kwa kifupi huku nikizingatia maelezo yangu yote ya huko juu, kuwa YESU SI MUNGU, lakini hakumaanishi kuwa hakuna wanao muita au wanao amini Yesu Mungu. La kuzingatia kama tukiambiwa kauli ipi ya kushika kati ya YESU mwenyewe na ya Paulo kwa vyovyote vile tunatakiwa kushika kauli ya Yesu.

Kauli zote za Paulo ambazo hazipingani na za Yesu, kauli hizo tutazifuata, lakini kauli yoyote ya Paulo inayo pingana na Yesu, kauli ya Paulo itapuuzwa na kuanguka, alafu watu wote wanatakiwa wafuate kauli ya Yesu.

Hakuna kauli ya Yesu anayo alijiita Mungu, lakini zipo nyingi akijiita Mtu au mwana wa adamu. Na siku zote alijitafautisha na Mungu. Yesu anakata mzizi wa fitina katika andiko hili.

"Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma"
Yohana 17:3

Nasema YESU SI MUNGU, na Paulo ana kesi ya kujibu kwa kudanganya ulimwengu, na kwa kuharibu mafundisho ya Yesu na kubwa zaidi kwa kuwatesa na kuwaua wanafunzi wa Yesu na wafuasi wake.

Katika kuendeleza urongo wa Paulo, watu wameambukizwa urongo, sasa wanatusambazia picha na sanamu za wacheza sinema na kisha wanataka tuziheshimu kama Yesu, kweli watu wanaangamia kwa kukosa maarifa.

TUJADILI!

Dotto Rangimoto Chamchua(Njano5)
Call/whatspp 0622845394 Morogoro.

Ee Mwenyezi Mungu, Mungu wa Ibrahim na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo uwape neema yako wale wasiokufahamu, wakufahamu, wakukiri na wakutumikie ili waokoke. Wale wenye kiburi uwalegeze mioyo yao ili warudi kwako na wasipotee na waliolegea katika IMANI uwape nguvu ya kukutumikia kwa uaminifu. Amen.
 
Sikushangai hizi ni akili sampuli ya mohamed kabisa hizi.

Huu uzi uko posti ya ngapi, tuko tunafafanua haya maswali yako ya watoto wa sundayschool husomi uelewe, badala yake unakuja kuquote baba zako kihunihuni tu.

Haya rudi kaanze upya.
anyway ngoja nikuache kama ulivyo coz akili chache haiwezi ongoza akili nyingi ok my in law gooday
 
Kabla hatujamsaidia huyu mwenye mada mwenye mashaka. Tumuulize Mungu ninani kwanza.
 
Alivyokua duniani Yesu alijivua uungu. Ndo mana akawa anamtegemea Mungu baba!
Angekua Mungu akati yuko duniani hasingezaliwa, hasingesikia njaa, hasingeweza jaribiwa na hasingekufa. Yesu alichukua ubinadamu ili aishi duniani.
Unaonesha jinsi gani ulivyokosa akili ya kutafakari. Yaani umesema kwamba yesu alivyokuwa duniani alikuwa anamtegemea mungu baba. Jibu lako tu linaoonesha kuwa kumbe kuna mwingine zaidi ya yesu alikuwa ndio kila kitu na ndio Mungu huyo. Kwani una miungu mingapi wewe? Maana kuja kwa yesu duniani nilijua utasema kuwa alijitegemea mwenyewe kwavile alijivua uungu. Kumbe ana mtegemea baba. Sasa hapo mkuu ni baba na sio yesu. Je yesu ni nani? Haaa ni mtumishi tu wa Mungu.

Matendo 3:13

Mungu wa Ibrahimu na wa Isaka na wa Yakobo, Mungu wa baba zetu, amemtukuza mtumishi wake Yesu, ambaye ninyi mlimsaliti na kumkana mbele ya Pilato, alipokuwa ametoa hukumu yake afunguliwe

Matendo 3:26

Mungu, akiisha kumfufua mtumishi wake Yesu, alimtuma kwenu ninyi kwanza, ili kuwabarikia kwa kumwepusha kila mmoja wenu na maovu yake
 
Ok kwa maana hiyo haya yote yazingekinzana na maisha ya Yesu, moja kwa moja ungekubari kwamba ni Mungu?????.

Sasa sisi tulioambiwa kwamba atachukua mwili aje kukaa kwetu akiwa na mwili wa kibinaadamu(unaielewa point yetu sasa????),kwamba mwili wa kibinaadamu una sifa zisizobadirika.ili Mungu mwenyewe asikinzane na sifa zake kwamba, hachoki, haumwi njaa, hafi, haonekani.ilibidi auvue utukufu wake mbinguni na kuuvaa mwili wenye mapungufu hayo.

Swali ni je, kama alikufa siku tatu akiwa kaburini mamlaka na nguvu vilikuwa chini ya nani, maana Mungu hafi na akifa sio Mungu, (SWALI HILI MSINGI WAKE NI KWAMBA, UNAYEULIZA SWALI HILI TAYARI UMEKADIRIA UKOMO WA UWEZO WA MUNGU) kwamba mungu kuna mambo hawezi kufanya yako juu ya uwezo wake.lakini jibu ni rahisi, uliokufa ni mwili sio Utukufu wake, na kudhihirisha kwamba utukufu wake uliishi bado mauti hayakuwa na mamlaka na mwili ule ukachukuliwa tena.

Mpaka hapo?????


Asili ya imani ya mungu-mtu na desturi zake


Kulingana na mafundisho ya Biblia tukufu, asili ya imani ya mungu-mtu imetokana na watu wa mataifa, yaani wapagani ambao wengi wao ndio ambao hawakubahatika kufikiwa na ujumbe wa Mungu-Yehovah kupitia msururu wa Manabii wake ambao kwa idadi kubwa aliwatuma kwa wana wa Israeli.

Kwa hali hiyo, ni wazi kuwa watu hawa (wa mataifa au wapagani) walikuwa mbali kabisa na Mungu-Yehovah kwa kutomjua na kwa hiyo wakaangukia katika imani potofu ya kuamini miungu bandia yenye desturi za kujigeuza kuwa mfano wa wanadamu.

Uthibitisho wa hayo tunaupata katika maandiko ya Biblia tukufu yafuatayo:


"Na huko Listra palikuwa na mtu mmoja, dhaifu wa miguu, kiwete tangu tumboni mwa mamake, ambaye hajaenda kabisa. Mtu huyo alimsikia Paulo alipokuwa akinena, ambaye akamkazia macho na kuona kuwa ana imani ya kuponywa, akasema kwa sauti kuu, simama kwa miguu yako sawa sawa. Akasimama upesi akaenda. Na makutano walipoona aliyoyafanya Paulo wakapaza sauti zao, wakisema kwa Kilikaonia, miungu wametushukia kwa mifano ya wanadamu. Wakamwita Barnaba, Zeu na Paulo, Herme, kwa sababu ndiye aliyekuwa mnenaji. Kuhani wa Zeu ambaye hekalu lake lilikuwa mbele ya mji, akaleta ng'ombe na taji za maua hata malangoni, akitaka kutoa dhabihu pamoja na makutano". (Matendo ya Mitume 14:8-13)


Tunachoelezwa na maandiko hayo ya Biblia Tukufu hapo juu ni kwamba, Bwana Paulo na mwenzie Barnaba walipofika Listra (huko kwa watu wa mataifa au wapagani) waliwakuta wenyeji wa huko tayari walikuwa na dini yao yenye miungu iliyokuwa na tabia ya kujigeuza kuwa wanadamu.

Miungu hiyo ambayo tayari ilikuwa na majina yao kama hayo ya Zeu na Herme, walikuta pia tayari imewekewa taratibu za dini, ikiwemo hiyo ya kuwa na mahekalu.

Aidha, waliikuta dini yao hiyo tayari imewekewa pia utaratibu wake wa ibada wanazoifanyia miungu yao hiyo; kama hiyo ya kuitolea miungu hiyo dhabihu kwa kuichinjia wanyama na kadhalika.

Maelezo hayo ya Biblia vile vile yanaonyesha pia kuwa kwa kuathiriwa na imani yao hiyo ya miungu-watu, watu hao (wa mataifa au wapagani) walipokuwa wakimwona mtu afanyaye maajabu, basi humwita mtu huyo kuwa ni mungu kwa majina ya miungu yao hiyo (akina Zeu na Herme) kama walivyowaita hapo kina Paulo na mwenzie Barnaba kwa kuona jinsi walivyomfanyia maajabu kiwete.

Kwa kuwa waliamini kuwa miungu yao ndio ifanyayo hivyo.

Kwa ujumla basi, hiyo ndiyo hali halisi aliyoikuta Bwana Paulo na mwenzie Barnaba kwa watu wa mataifa yaani wapagani.

Kwa shuhuda hiyo ya Biblia, tunaona wazi kuwa asili ya imani ya mungu-mtu mwenye desturi ya kujigeuza mwanadamu inatokana na watu wa mataifa, yaani wapagani.
 
mkorinto:

Sifa kuu za miungu-watu wa wapagani


Kwa mujibu wa Bwana Paulo (kama tutakavyokuja kuona hapo baadae) miungu-watu hii (kama hiyo ya akina Zeu na Herme) ilikuwa na sifa kuu zifuatazo:

Kuzaliwa na mwanamke

Kuwa na sifa zote za mwanadamu (kama vile kula, kunywa, kulala, kwenda choo, kuchoka na kadhalika).

Kujibadilisha-badilisha (wakati fulani inakuwa miungu na wakati mwingine inakuwa wanadamu).
Kufa na Kufufuka.

Kwa wanaotaka kupata taarifa zaidi kuhusu sifa hizi za miungu-watu kama zilivyoelezwa na Bwana Paulo, wasome taarifa zaidi kutoka "Encyclopaedia Brittanica" chini ya maneno Zeus na Hermes (Jupiter na Mercury).
 
mkorinto:



Dini ya Kikristo na imani ya mungu-mtu


Awali kabisa tumeona maandiko ya Biblia tukufu yakielezea jinsi Bwana Paulo na mwenzie Barnaba walivyokwenda kwa watu wa mataifa, yaani wapagani na kuwakuta watu hao tayari wanayo dini yao yenye miungu iliyokuwa na tabia ya kujigeuza kuwa wanadamu.

Sambamba na dini hiyo (ya wapagani), Biblia pia inafundisha kuwa miaka miwili baada ya Nabii Isa au Yesu (a.s.) kuondoka, Bwana Paulo naye alileta duniani dini mpya ya mungu-mtu (kama tutakavyokuja kuona hapo baadae) mwenye desturi naye ya kujigeuza kuwa mfano wa wanadamu.

Dini hiyo aliyoianzisha Paulo aliita "Ukristo". (Tazama Biblia ya Wakatoliki, Imprimatur Mihayo, 1967 Tabora Uk. 1025).

Pamoja na shuhuda hiyo, pia kulingana na mafundisho yake (kama tutakavyokuja kuona kwa kirefu zaidi hapo baadae), ukiondoa majina yao, mungu huyo aliyekuja kumhubiri Paulo, kimsingi hakutofautiana kabisa na miungu hiyo ya wapagani.

Na kwa ujumla basi, ibada nyingi kama si zote za dini ya mungu wake huyo (ya Ukristo) kimsingi zinalingana sawa na zile ibada za watu wa mataifa (wapagani).
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom