OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,235
- 103,869
KUNA wakati huwa hatupendi ukweli. Tunapenda kudanganyana kwa sababu tu ya ushabiki. Ni kama hili la Simba na Yanga kimataifa.
Nimeona tambo za Yanga katika michuano ya Kombe la Shirikisho. Wanatamba kuwa watafanya vizuri na kufika mbali.
Wanatamba kuwa wao ni bora kuliko timu yoyote nchini kwa sasa. Ni kweli. Matokeo ya Ligi ya ndani yanaonyesha hilo. Ni wazi kuwa Yanga iko katika kilele cha ubora wao.
Tangu msimu uliopita mpaka sasa wamepoteza mechi moja tu ya ligi. Ni rekodi bora sana. Hakuna timu nchini imewahi kufanya hivyo.
Yanga imekuwa vyema sana ndani na nje ya uwanja. Haipotezi mechi kizembe. Ni ngumu kutabiri inapoteza mchezo lini. Inapendeza sana.
Lakini ukweli ni kwamba pamoja na uimara ilionao Yanga sasa bado ina mengi ya kujifunza katika michuano ya kimataifa.
Huku kwenye mechi za CAF, Simba ina dunia yake. Imejenga ufalme ambao hautikisiki kirahisi.
Ilianza ikiwa hovyo lakini imekwenda ikiimarika siku hadi siku. Sasa wamekuwa wababe hasa wakiwa nyumbani.
Baada ya miaka 15 bila kuingia hatua ya makundi kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, miaka hii mitano iliyopita imebadilisha kila kitu.
Ilionekana kama imebahatisha ilipofuzu robo fainali mwaka 2019. Ni kweli haikuwa na timu imara sana kama sasa. Lakini ilikuwa na hesabu kali.
Pamoja na kufungwa 5-0 na AS Vita pale Kinshasa. Ikapigwa tena kipigo kama hicho na Al Ahly pale Cairo. Bado Simba iliweza kupenya. Iliweka hesabu kali na mipango ya kushinda nyumbani.
Leo hii Simba ni kati ya Timu 10 bora Afrika. Unajua Simba Sc inaelekea wapi. Kituo kinachofuata ni kunyakua kombe la kulitua juu ya mlima Kilimanjaro-Visit Tanzania. Kuna baadhi huleta dhihaka kwamba Simba imechukua kombe gani Afrika?!! Ni kweli hajachukua lakini ni nani anayeweza kutoka 1 ghafla akafika 10 bila kupita 2 na 3? Kwa hiyo Yanga wanayo ya kujifunza zaidi ya mengi ambayo mpaka sasa wamejifunza.
Kwanza kabisa wameingia kwenye kuendesha timu kiuwekezaji kama ilivyofanya Simba Sc na Mo Dewji. Hatimaye GSM amewekeza Yanga na matunda yameanza kuonekana. Pili wamekuwa na msukumo wa kuhakikisha wanatumia vizuri uwanja wa nyumbani kupata matokeo. Hii ndiyo ile Simba wanaita Kwa Mkapa hatoki mtu.
Leo hii katika point 46.5 za Tanzania CAF Simba ina point 39 na Yanga ina 10 pekee. Nasema izidishe bidii kujifunza ili kuvuna point nyingi zaidi na kufika viwango vya Simba Sc. Ikazane kwa sababu wote walikuwa ligi ya mabigwa Afrika lakini Simba anakuwa mkiwa bila mdogo wake Yanga ambaye hatimaye amedondokea Kombe la Shirikisho.
My Take
Wivu wa maendeleo ni jambo jema, ila wivu wa chuki ni dhambi itakufa kifo kibaya
Nimeona tambo za Yanga katika michuano ya Kombe la Shirikisho. Wanatamba kuwa watafanya vizuri na kufika mbali.
Wanatamba kuwa wao ni bora kuliko timu yoyote nchini kwa sasa. Ni kweli. Matokeo ya Ligi ya ndani yanaonyesha hilo. Ni wazi kuwa Yanga iko katika kilele cha ubora wao.
Tangu msimu uliopita mpaka sasa wamepoteza mechi moja tu ya ligi. Ni rekodi bora sana. Hakuna timu nchini imewahi kufanya hivyo.
Yanga imekuwa vyema sana ndani na nje ya uwanja. Haipotezi mechi kizembe. Ni ngumu kutabiri inapoteza mchezo lini. Inapendeza sana.
Lakini ukweli ni kwamba pamoja na uimara ilionao Yanga sasa bado ina mengi ya kujifunza katika michuano ya kimataifa.
Huku kwenye mechi za CAF, Simba ina dunia yake. Imejenga ufalme ambao hautikisiki kirahisi.
Ilianza ikiwa hovyo lakini imekwenda ikiimarika siku hadi siku. Sasa wamekuwa wababe hasa wakiwa nyumbani.
Baada ya miaka 15 bila kuingia hatua ya makundi kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, miaka hii mitano iliyopita imebadilisha kila kitu.
Ilionekana kama imebahatisha ilipofuzu robo fainali mwaka 2019. Ni kweli haikuwa na timu imara sana kama sasa. Lakini ilikuwa na hesabu kali.
Pamoja na kufungwa 5-0 na AS Vita pale Kinshasa. Ikapigwa tena kipigo kama hicho na Al Ahly pale Cairo. Bado Simba iliweza kupenya. Iliweka hesabu kali na mipango ya kushinda nyumbani.
Leo hii Simba ni kati ya Timu 10 bora Afrika. Unajua Simba Sc inaelekea wapi. Kituo kinachofuata ni kunyakua kombe la kulitua juu ya mlima Kilimanjaro-Visit Tanzania. Kuna baadhi huleta dhihaka kwamba Simba imechukua kombe gani Afrika?!! Ni kweli hajachukua lakini ni nani anayeweza kutoka 1 ghafla akafika 10 bila kupita 2 na 3? Kwa hiyo Yanga wanayo ya kujifunza zaidi ya mengi ambayo mpaka sasa wamejifunza.
Kwanza kabisa wameingia kwenye kuendesha timu kiuwekezaji kama ilivyofanya Simba Sc na Mo Dewji. Hatimaye GSM amewekeza Yanga na matunda yameanza kuonekana. Pili wamekuwa na msukumo wa kuhakikisha wanatumia vizuri uwanja wa nyumbani kupata matokeo. Hii ndiyo ile Simba wanaita Kwa Mkapa hatoki mtu.
Leo hii katika point 46.5 za Tanzania CAF Simba ina point 39 na Yanga ina 10 pekee. Nasema izidishe bidii kujifunza ili kuvuna point nyingi zaidi na kufika viwango vya Simba Sc. Ikazane kwa sababu wote walikuwa ligi ya mabigwa Afrika lakini Simba anakuwa mkiwa bila mdogo wake Yanga ambaye hatimaye amedondokea Kombe la Shirikisho.
My Take
Wivu wa maendeleo ni jambo jema, ila wivu wa chuki ni dhambi itakufa kifo kibaya