bryan2
JF-Expert Member
- Jun 8, 2016
- 3,323
- 4,667
Nani asiyejua kutetema? Japo mimi Simba ila wakati mwingine najificha hata kichakani ili niteteme jamaa zangu wa Simba wasinione.
Twende kwenye mada, kwa hesabu zile za darasa la nje Yanga ndiyo timu yenye kuwa na bahati ya kupata straika hatari kutoka nje ya nchi.
Anzia tu mzee wa kutetema Fistoni Kalala Mayele beki na makipa wa timu pinzani hawana hamu na huyu kiumbe.
Donald Dompo Ngoma
Mzimbabwe huyu naye alikuwa chuma haswa beki zimeteswa.
Bonifasi Ambani
Jamaa wa Ruto tu hapo naye alikuwa straika mmoja hatari, kapanda hewani akiona nyavu anaanza kulia, japo sika hakika ila nasikia mwamba baada ya kuibuka mfungaji bora na kuwanyima wenzake mpunga wakaanza kumbania kumpa pasi.
Didier Kavumbagu
Kijana toka Bujumbura/Burundi aliwika sana, beki na makipa walikua wakilala wanamwota.
Hamis Tambwe
Nakumbuka timu yangu ilimtupia virago kwa kigezo kiwango kimeshuka ila baada ya kwenda Yanga aliendeleza makali yake.
Maurice Sunguti
Jamaa mwonekano wake ulikuwa kama mzee fulani, ila uliza mabeki waliokutana naye kipindi kile watakwambia kweli kama alikuwa mzee au kijana kati ya foward matata kutokea pale Yanga.
Hamis Kiiza Diego
Ulikuwa ukisikia mtangazaji kataja Kiiza ujue watu bamerokota kwa nyavu. Hakuwa na mambo mengi ila alikuwa analifahamu goli lilipo.
Emanuel Okwi
Uzuri wa huyu mwamba yeye hakui, kila mwaka ana miaka 25! Japo naye alipita Yanga ila hakua na makali kivileee japo alitoa mchango wake pia.
David Molinga
Straika fulani hivi heavy weight, mwamba kipindi Yanga inapita kwenye mapito ya jangwani aliibuka kuwa top scorer wa timu na magoli yake fulani hivi ya free kick za utatoa hutoi.
Heriter Ebener Makambo
Ndiyo yule yule mzee wa kuwajaza, jamaa alikuja kama mwamba asiyeimbwa ila baadaye aliibuka kuwa shujaa. Aliua kiwango baada ya kwenda Horoya.
Yeah, kama nawe unawakumbuka mastraika wa kigeni waliovuma pale mitaa ya Twiga na Jangwani endeleza listi.
Tukumbuke pia Yikpe naye kapita Yanga akiwa straika wa hatari ila anakwambia alilogwa tu akawa haoni goli.
Twende kwenye mada, kwa hesabu zile za darasa la nje Yanga ndiyo timu yenye kuwa na bahati ya kupata straika hatari kutoka nje ya nchi.
Anzia tu mzee wa kutetema Fistoni Kalala Mayele beki na makipa wa timu pinzani hawana hamu na huyu kiumbe.
Donald Dompo Ngoma
Mzimbabwe huyu naye alikuwa chuma haswa beki zimeteswa.
Bonifasi Ambani
Jamaa wa Ruto tu hapo naye alikuwa straika mmoja hatari, kapanda hewani akiona nyavu anaanza kulia, japo sika hakika ila nasikia mwamba baada ya kuibuka mfungaji bora na kuwanyima wenzake mpunga wakaanza kumbania kumpa pasi.
Didier Kavumbagu
Kijana toka Bujumbura/Burundi aliwika sana, beki na makipa walikua wakilala wanamwota.
Hamis Tambwe
Nakumbuka timu yangu ilimtupia virago kwa kigezo kiwango kimeshuka ila baada ya kwenda Yanga aliendeleza makali yake.
Maurice Sunguti
Jamaa mwonekano wake ulikuwa kama mzee fulani, ila uliza mabeki waliokutana naye kipindi kile watakwambia kweli kama alikuwa mzee au kijana kati ya foward matata kutokea pale Yanga.
Hamis Kiiza Diego
Ulikuwa ukisikia mtangazaji kataja Kiiza ujue watu bamerokota kwa nyavu. Hakuwa na mambo mengi ila alikuwa analifahamu goli lilipo.
Emanuel Okwi
Uzuri wa huyu mwamba yeye hakui, kila mwaka ana miaka 25! Japo naye alipita Yanga ila hakua na makali kivileee japo alitoa mchango wake pia.
David Molinga
Straika fulani hivi heavy weight, mwamba kipindi Yanga inapita kwenye mapito ya jangwani aliibuka kuwa top scorer wa timu na magoli yake fulani hivi ya free kick za utatoa hutoi.
Heriter Ebener Makambo
Ndiyo yule yule mzee wa kuwajaza, jamaa alikuja kama mwamba asiyeimbwa ila baadaye aliibuka kuwa shujaa. Aliua kiwango baada ya kwenda Horoya.
Yeah, kama nawe unawakumbuka mastraika wa kigeni waliovuma pale mitaa ya Twiga na Jangwani endeleza listi.
Tukumbuke pia Yikpe naye kapita Yanga akiwa straika wa hatari ila anakwambia alilogwa tu akawa haoni goli.