Yanayosemwa huko Algeria kuhusu tuhuma za kufix mechi ya Tanzania vs Algeria

Mengi yanasemwa kuhusu matokeo ya mechi ya Tanzania vs Algeria iliyoisha kwa suluhu na kuipeleka Tanzania AFCON 2023 huku Uganda ikikosa nafasi hiyo. Nimechukua kama lisaa kufuatilia nini kinasemwa huko nje na nakileta kwenu muone jinsi wanavyotuchafua na kutuona kama hatukuwa na uwezo wa kuwafunga. Naomba niseme kuwa sisemi wala sijawahi kusema Tanzania imenunua hii mechi, hili naomba nilisisitize sana.

Nianze kwa kusema kuwa tuhuma za kufix mechi ni tuhuma nzito sana katika ulimwengu wa soka na siyo tuhuma za kuzichukulia kwa mzaha.

Katika mechi hiyo, Algeria walimiliki mpira kwa asilimia 80, ambazo ni asilimia kubwa sana katika mchezo na pia ukiangalia idadi ya pasi na usahihi wa pasi zao ukilinganisha na sisi ilikuwa ni mbingu na ardhi. Pamoja na hayo Waalgeria wengi wanadhani hiyo ni moja ya mechi mbaya zaidi kwa timu yao katika miaka 5 iliyopita. Wakati sisi tunaona walitawala mchezo, wenyewe wanaona waliboronga mnoo. Nadhani wenzetu wamejiwekea viwango vikubwa mno kwa timu zao.

“It's the 3rd or 4th worst game for the Algerian team since Belmadi's arrival. You could never have guessed that the national team would have such a level. We clearly did not feel that it is a team that occupies the first places in the FIFA rankings.....,” said Yassine Maloumi, a journalist and football specialist.

Algeria Tanzania – “One of the worst matches in Belmadi”

Nadhani wanaodhani hii mechi ilinunuliwa imechangiwa pia na mazingira yaliyozunguka mechi yenyewe. Kwanza kuna maamuzi ya kocha kuamua siku chache kabla ya mechi kutotumia uwanja uliotumika kwa mechi hiyo kwa ajili ya mazoezi ya timu yao. Tukumbuke huu uwanja eneo lake la kuchezea halikuwa kwenye kiwango kizuri na kocha huyo alikuwa anajua hilo na kwa hiyo wachezaji wa Algeria ambao wengi wamezoea kucheza kwenye viwanja vyenye viwango vya juu wangehitaji kufanyia mazoezi pale ili kuuzoea ila kocha wao alibadili mawazo na hakuwapa hiyo fursa.

Algerian team: a new strange decision by Djamel Belmadi causes a scandal

Kabla ya hapo, kuna maamuzi mengine ambayo Belmadi alikuja kujilaumu ya kuipeleka timu kuweka kambi mji tofauti na utakaochezewa mechi jambo ambalo liliongeza usumbufu kwa wachezaji.

A bitter regret for Djamel Belmadi just a few days from Tanzania!

Mtu mmoja alicomment kuwa anadhani kocha wa Algeria alikuwa anataka kumsaidia kocha wa Tanzania ambaye ni Mualgeria mwenzake akigusia kuwa inaonyesha kila wakicheza na timu inayoongozwa na kocha wa kutoka Algeria inaonekana kama wanawafanya feva.

"I noticed every time we play against Algerian manager we do favors , and I think Belmadi was trying to help the new Algerian coach for Tanzania Amrouche"

Kuna wengine wanamtuhumu pia refa alihusika katika kuipendelea Tanzania. Kocha wa Algeria Belmadi alisema refa alikuja kwenye mechi hiyo akiwa na dhamira ya kuibeba Tanzania. Mchezaji wa zamani wa Morocco Abdessalam Ouaddou amemkingia kifua Belmadi kuwa hawezi kuhusika na kufix mechi hiyo ila naye amemtuhumu refa.

“I watched the match and I have to say it’s not true. I know the two coaches and it is not in their values. […] Stop this misinformation. Algeria was weighed down by a referee who clearly came on a mission during qualifying and was certainly appointed for the cause. Algeria fights for integrity and transparency and clean football ,” Ouaddou.

The Algerian team accused of fixing

Kilichobeba uzito zaidi katika tuhuma hizi ni kocha wa Uganda Milutin Sredojević amenukuliwa akisema waziwazi kuwa mechi hiyo imekuwa fixed ili Tanzania iweze kufuzu. Kocha huyu anayejulikana zaidi nchini kama "Micho" amewahi kuifundisha Yanga kwa hiyo tuhuma hizi zinabeba uzito zaidi kutokana na hiyo historia yake. Micho amesema kilichotokea ni aibu kwa mchezo wa soka na ameahidi kufichua zaidi siku za mbele kuhusu tuhuma hizi.

“What happened during the match between the greens and Tanzania is a shame for football… Algeria was complacent with Tanzania and offered them qualification for the Cup from Africa.”

Controversy! Algeria openly accused of having fixed its match against Tanzania

Inawezekana Micho anajaribu kulinda kibarua chake ila tuhuma hizi ni nzito kutoka kwa mtu kama yeye.

Hili jambo nawaachia wakulungwa, mimi kazi yangu imeisha.
Lakini si tumepita? Au wanataka tukapigiane penati?
 
Kumiliki mpira sio kupata matokeo....Kama unabisha nenda kafuatilie takwimu za mchezo Kati ya Spain na Russia wa kombe la dunia ambapo Spaini alitolewa kwa penalties.......
 
Kwa wote mnaoongelea kuhusu takwimu za umiliki mpira, hilo nililiongeza mimi katika mjadala huu kuonyesha hata hilo halikuwaridhisha na kuonyesha jinsi wenzetu wanavyoangalia mpira tofauti na sisi. Sijaona wala kusikia wao wakitumia kigezo hicho kusema kulikuwa na upangaji matokeo.

Nilichofanya ni kuweka kila angle niliyopata na iliyozungumzwa kabla na baada ya mchezo.
 
Mechi ilikuwa sahihi kwa hayo matokeo mana Algeria hakuna walichokuwa wanatafuta katika mechi hii walishafuzu Ina mana na hao waganda tuseme walifix na Niger wakapewa zile goli mana Niger nayo ilikuwa ishajikatia tamaa
 
Ukweli usemwe Taifa star bila msaada wa third party hatuwezi kuenda Afcon kumbukeni vizuri, kipindi kilicho pita hao Waganda ndo walio tuachia mechi na ka fuzi Afcon kule hatukufanya chochote.
Team ya taifa ni dhaifu ndo ukweli watanzania hawataki kuusikia na hu udhaifu umechangiwa na ushabiki wa timu mbili mnazijua vizuri, pale taifa star nimeangalia mpira sikuona kipaji chochote, Algeria walituachia ile match kiasi kwamba tulipaswa tuofunge kabisa 2-0 ila tulipoteza ata zile chances tulivyo achiwa ndo tukatoka sare.
Aisee unaweza Kuta Kuna mtu anakuita BABA
 
Kocha wa Niger alisema wataiachia Uganda ili ishinde iende AFCON baada ya mechi yao na Tanzania. Na jana Uganda wakashinda hawakupanga matokeo?
Hii ndo ilikuwa fixed takwimu hizo hakuna shot on target hata moja
Screenshot_20230910-204353.jpg


Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Uganda wangetaka kufuzu wangeshinda mechi zao mapema kama Algeria,mambo ya kusubiri mechi ya mwisho ndio madhara yake hayo
 
Mengi yanasemwa kuhusu matokeo ya mechi ya Tanzania vs Algeria iliyoisha kwa suluhu na kuipeleka Tanzania AFCON 2023 huku Uganda ikikosa nafasi hiyo. Nimechukua kama lisaa kufuatilia nini kinasemwa huko nje na nakileta kwenu muone jinsi wanavyotuchafua na kutuona kama hatukuwa na uwezo wa kuwafunga. Naomba niseme kuwa sisemi wala sijawahi kusema Tanzania imenunua hii mechi, hili naomba nilisisitize sana.

Nianze kwa kusema kuwa tuhuma za kufix mechi ni tuhuma nzito sana katika ulimwengu wa soka na siyo tuhuma za kuzichukulia kwa mzaha.

Katika mechi hiyo, Algeria walimiliki mpira kwa asilimia 80, ambazo ni asilimia kubwa sana katika mchezo na pia ukiangalia idadi ya pasi na usahihi wa pasi zao ukilinganisha na sisi ilikuwa ni mbingu na ardhi. Pamoja na hayo Waalgeria wengi wanadhani hiyo ni moja ya mechi mbaya zaidi kwa timu yao katika miaka 5 iliyopita. Wakati sisi tunaona walitawala mchezo, wenyewe wanaona waliboronga mnoo. Nadhani wenzetu wamejiwekea viwango vikubwa mno kwa timu zao.

“It's the 3rd or 4th worst game for the Algerian team since Belmadi's arrival. You could never have guessed that the national team would have such a level. We clearly did not feel that it is a team that occupies the first places in the FIFA rankings.....,” said Yassine Maloumi, a journalist and football specialist.

Algeria Tanzania – “One of the worst matches in Belmadi”

Nadhani wanaodhani hii mechi ilinunuliwa imechangiwa pia na mazingira yaliyozunguka mechi yenyewe. Kwanza kuna maamuzi ya kocha kuamua siku chache kabla ya mechi kutotumia uwanja uliotumika kwa mechi hiyo kwa ajili ya mazoezi ya timu yao. Tukumbuke huu uwanja eneo lake la kuchezea halikuwa kwenye kiwango kizuri na kocha huyo alikuwa anajua hilo na kwa hiyo wachezaji wa Algeria ambao wengi wamezoea kucheza kwenye viwanja vyenye viwango vya juu wangehitaji kufanyia mazoezi pale ili kuuzoea ila kocha wao alibadili mawazo na hakuwapa hiyo fursa.

Algerian team: a new strange decision by Djamel Belmadi causes a scandal

Kabla ya hapo, kuna maamuzi mengine ambayo Belmadi alikuja kujilaumu ya kuipeleka timu kuweka kambi mji tofauti na utakaochezewa mechi jambo ambalo liliongeza usumbufu kwa wachezaji.

A bitter regret for Djamel Belmadi just a few days from Tanzania!

Mtu mmoja alicomment kuwa anadhani kocha wa Algeria alikuwa anataka kumsaidia kocha wa Tanzania ambaye ni Mualgeria mwenzake akigusia kuwa inaonyesha kila wakicheza na timu inayoongozwa na kocha wa kutoka Algeria inaonekana kama wanawafanya feva.

"I noticed every time we play against Algerian manager we do favors , and I think Belmadi was trying to help the new Algerian coach for Tanzania Amrouche"

Kuna wengine wanamtuhumu pia refa alihusika katika kuipendelea Tanzania. Kocha wa Algeria Belmadi alisema refa alikuja kwenye mechi hiyo akiwa na dhamira ya kuibeba Tanzania. Mchezaji wa zamani wa Morocco Abdessalam Ouaddou amemkingia kifua Belmadi kuwa hawezi kuhusika na kufix mechi hiyo ila naye amemtuhumu refa.

“I watched the match and I have to say it’s not true. I know the two coaches and it is not in their values. […] Stop this misinformation. Algeria was weighed down by a referee who clearly came on a mission during qualifying and was certainly appointed for the cause. Algeria fights for integrity and transparency and clean football ,” Ouaddou.

The Algerian team accused of fixing

Kilichobeba uzito zaidi katika tuhuma hizi ni kocha wa Uganda Milutin Sredojević amenukuliwa akisema waziwazi kuwa mechi hiyo imekuwa fixed ili Tanzania iweze kufuzu. Kocha huyu anayejulikana zaidi nchini kama "Micho" amewahi kuifundisha Yanga kwa hiyo tuhuma hizi zinabeba uzito zaidi kutokana na hiyo historia yake. Micho amesema kilichotokea ni aibu kwa mchezo wa soka na ameahidi kufichua zaidi siku za mbele kuhusu tuhuma hizi.

“What happened during the match between the greens and Tanzania is a shame for football… Algeria was complacent with Tanzania and offered them qualification for the Cup from Africa.”

Controversy! Algeria openly accused of having fixed its match against Tanzania

Inawezekana Micho anajaribu kulinda kibarua chake ila tuhuma hizi ni nzito kutoka kwa mtu kama yeye.

Hili jambo nawaachia wakulungwa, mimi kazi yangu imeisha.
Macho anajaribu kujificha kwenye kivuli cha Tanzania kwa matukio yake mwenyewe. Kwa kumbukumbu ilisemekana kocha wa Niger alitamka kuwa atahakikisha anafungwa na Uganda ili kuinyima Tanzania nafasi ya kufuzu Afcon akiwa na imani Algeria itaifunga taifa Stars.

Matokeo yamekuwa tofauti wanataka kuleta ujinga wa kuona hatukustahili kufuzu.
 
Ukweli usemwe Tz haikuwa na uwezo wakupata sare kwenye ardhi ya mwarabu..
. Kilichotokea ni kubebwa na mwarabu kutokuihitaji mechi.
 
Algeria lost at home 1-2 when hosted Cameroon towards Fifa 2022 world cup qualifier..wakati kule ugenini Cameroon walishinda 0-1.(first leg)

Kocha alikuwa huyuhuyu.
Kwny game ile host walitawala sehemu kubwa ya mechi.sasa kwann madai ya kupanga matokeo hayakuibuka tena kwny serious match kama like.

Tanzania haijaanza kutoa sare na Algeria ugenn Mara ya kwanza.

Mwaka 2011 Algeria na Tanzania walitoa sare 1-1 ktk mechi iliyochezwa kwny mji wa Blida hukohuko Algeria.

Mazingira ya sare ya 2011 hayatofautiani na ya juzi..possession kwa Algeria ilikuwa juu mno..

Nakumbuka ni shaaban kado alikuwa nyota wa mchezo kwa upande waTanzania.
 
Yaliopita si ndwele, tugange yaliopo na yajayo.
Ni fursa kwa taifa stars na Tanzania kuonekana
 
Ukweli kuwa mpira wa Tanzania umekua hautakiwi duniani, nchi nyingi bado zinaiona Taifa Stars ni ndondo club wakati sio kweli for now! Hivi Ibra Baka unampitaje Kwa mfano hata aje Ronaldo hafungi goli! Timu yetu kwasasa ina uwezo wa kupaki bus haswa na wamethibitisha Hilo dhidi ya Algeria!

Hata waseme nini Ukweli mpira wetu uko next level , wachezaji wanaweza na hawaogopi timu yoyote hata ugenini wanapiga boli na huko Afcon twende na wembe ni ule ule tukicheza na timu kali tunapaki bus na kushambulia kwa kushtukiza na tukicheza timu dhaifu tunafunguka na kushambulia kama nyuki mwanzo mwisho!

Waalgeria wote walikuja uwanjani na matokeo yao mfukoni na hasa kwa vile walitufunga nyumbani 2-0 wakajua kwao Algeria Stars tutaoga 8-0!

Sisi bongo ni bora kidogo kisoka kwa sasa na tulistahili kufuzu Afcon hasa baada ya Msuva kuifunga Uganda kwao ilitakiwa Ile mechi ya marudiano kwa Mkapa tumalize kazi ila ni ajabu wachezaji wetu wakaipuuza mechi muhimu tukakosa magoli mia kizembe sana Uganda wakatuadhibu nyumbani na kujisifu sana kulipa kisasi.

Tukutane Afcon , Taifa Stars mbele kwa mbele!
 
Porojo tu hizo, tuwape pongezi taifa stars kwa ujumla wamejitahidi sana kutoruhusu kufungwa, na kuwapa pressure timu pinzani kutoka mchezoni.

Swala la kumiliki mpira na usipate matokeo ni swala la kawaida tu mbona.
Labda hawaujui mchezo wa mpira mkuu, unaikumbuka inter ya Mourinho? Au the special one mwenyewe team zote alizofundisha na mifumo yake, anashinda sana game za hivi, possession zako ushindi wangu,

Micho aache kulia kulia. Ishaenda hiyo
 
Porojo tu hizo, tuwape pongezi taifa stars kwa ujumla wamejitahidi sana kutoruhusu kufungwa, na kuwapa pressure timu pinzani kutoka mchezoni.

Swala la kumiliki mpira na usipate matokeo ni swala la kawaida tu mbona.
Kuna mechi ya ulaya ilichezwa muda uleule ambao stars ilikuwa inakipiga na Algeria.

Nimesimuliwa kuwa timu iliyoshinda ilikuwa ni yenye low ball possession.

Kuwa na high ball possession si kigezo wala tiketi ya ulazima wa kushinda mechi.

Hata ngumi, mpiganaji anaweza akamiliki game muda mrefu halafu mpinzani akapiga moja tu ya knockout akawa mshindi.

Kunya anye kuku, akinya bata anaharisha. Imekula kwao.

Sent from my Infinix X688B using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom