Chabruma
JF-Expert Member
- Sep 19, 2013
- 5,660
- 1,777
Habari wadau wote wa Mtandao Pendwa Tanzania, mtandao wa kila mtu bila kujali itikadi zake za kisiasa, kidini, umri na jinsia, Mtandao wa JamiiForums.
Ni matumaini yangu kuwa Mwenyezi Mungu amewaamsha salama na wengi wenu mpo kwenye majukumu ya kujipatia riziki na kujenga taifa.
Wale ambao hawajaamka vema kwa siku ya leo kwa maana ni wagonjwa, Mwenyezi Mungu awajaalie wapone kwa haraka ili waungane nasi hapo jioni wakati tutakapowaletea moja kwa moja yatakayojiri Bungeni Dodoma wakati wa Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba. Kwa wale ambao wametangulia mbele za haki, tuwaombee dua kwa Mwenyezi Mungu ili wafike kwa amani kwenye nyumba ya milele na awaondolee adhabu za kaburi
Wadau, ikiwa ni saa moja kabla ya muda wa mwisho uliopangwa kurejesha fomu, ni wagombea wanne wamejitokeza kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Bunge Maalum.
Wagombea hao ni SAMMUEL SITTA, THERESIA HUVISA, HASHIM RUNGWE na JOHN CHIPAKA. Bado sijapata taarifa za wagombea hao kurejesha fomu kwa msimamizi wa uchaguzi huo ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kanuni Prof Costa Mahalu kupitia Ofisi za Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano pamoja na Katibu wa Baraza la Wawakilishi.
Pindi tutakapopata taarifa za uhakika, tutazirusha kama kawaida. Kwa sasa tuendelee kupata maoni ya wadau mbalimbali juu ya uchaguzi huu huku tukiendelea kutafakari uchaguzi huo kwa ujumla wake.
Kama kawaida natarajia kuungwa mkono kutoka kwa wadau mbalimbali hususan Skype, Simiyu Yetu, MaishaPesa, MKUU WA KAYA, Deo Corleone, Pasco na wengi ambao sijawataja lakini wamekuwa pamoja nasi tangu tuanze utaratibu huu.
Stay Connected
=====================
UPDATE 1:
- Wabumge wameanza kuingia Ukumbini. Ndani ya Ukumbi wa Bunge, idadi ya Wabunge ni ndogo dakika 10 kabla ya Kikao Kuanza.
- Wagombea waliotimiza vigezo vya kugombea ni wawili tu na wengineo hawapo tena katika kinyang'anyiro hicho. Waliokidhi vigezo kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Kudumu wa Bunge Maalum la Katiba; Samwel J. Sitta na Hashim Rungwe!
- Kila mgombea anapewa nafasi ya Dakika tatu kujieleza kisha yatafuata maswali. Anaanza kujieleza Hashim Rungwe.
* Rungwe kamaliza kujieleza; zaidi amedai yeye ni Mtanzania wa kwanza kuwa na Yard ya Magari mwishoni mwa miaka ya 80 na yeye ni Wakili wa Kujitegemea wa Mahakama Kuu ya Tanzania
* Sitta kajieleza wasifu wake kwa ufupi na kuwahakikishia wajumbe kuwa hatapendelea upande wowote. Anataka kuwahakikishia watanzania kuwa wataona sababu ya wajumbe kupewa hata kiinua mgongo watakapomaliza zoezi hili. Kasema yeye kupewa kiti ni sawa na kumrudisha chura kwenye maji, ni wazi ataogelea tu!
*Zoezi la upigaji kura linaendelea
================================================================
UPDATES 2
MATOKEO
Jumla ya wabunge wote 629
waliopiga kura ni. 563
Kura zilizoharibika ni. 7
Hashim Rungwe. 69 (12.3%)
Sammuel Sitta. 487. (86.5%)
======================
Ni matumaini yangu kuwa Mwenyezi Mungu amewaamsha salama na wengi wenu mpo kwenye majukumu ya kujipatia riziki na kujenga taifa.
Wale ambao hawajaamka vema kwa siku ya leo kwa maana ni wagonjwa, Mwenyezi Mungu awajaalie wapone kwa haraka ili waungane nasi hapo jioni wakati tutakapowaletea moja kwa moja yatakayojiri Bungeni Dodoma wakati wa Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba. Kwa wale ambao wametangulia mbele za haki, tuwaombee dua kwa Mwenyezi Mungu ili wafike kwa amani kwenye nyumba ya milele na awaondolee adhabu za kaburi
Wadau, ikiwa ni saa moja kabla ya muda wa mwisho uliopangwa kurejesha fomu, ni wagombea wanne wamejitokeza kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Bunge Maalum.
Wagombea hao ni SAMMUEL SITTA, THERESIA HUVISA, HASHIM RUNGWE na JOHN CHIPAKA. Bado sijapata taarifa za wagombea hao kurejesha fomu kwa msimamizi wa uchaguzi huo ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kanuni Prof Costa Mahalu kupitia Ofisi za Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano pamoja na Katibu wa Baraza la Wawakilishi.
Pindi tutakapopata taarifa za uhakika, tutazirusha kama kawaida. Kwa sasa tuendelee kupata maoni ya wadau mbalimbali juu ya uchaguzi huu huku tukiendelea kutafakari uchaguzi huo kwa ujumla wake.
Kama kawaida natarajia kuungwa mkono kutoka kwa wadau mbalimbali hususan Skype, Simiyu Yetu, MaishaPesa, MKUU WA KAYA, Deo Corleone, Pasco na wengi ambao sijawataja lakini wamekuwa pamoja nasi tangu tuanze utaratibu huu.
Stay Connected
=====================
UPDATE 1:
- Wabumge wameanza kuingia Ukumbini. Ndani ya Ukumbi wa Bunge, idadi ya Wabunge ni ndogo dakika 10 kabla ya Kikao Kuanza.
- Wagombea waliotimiza vigezo vya kugombea ni wawili tu na wengineo hawapo tena katika kinyang'anyiro hicho. Waliokidhi vigezo kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Kudumu wa Bunge Maalum la Katiba; Samwel J. Sitta na Hashim Rungwe!
- Kila mgombea anapewa nafasi ya Dakika tatu kujieleza kisha yatafuata maswali. Anaanza kujieleza Hashim Rungwe.
* Rungwe kamaliza kujieleza; zaidi amedai yeye ni Mtanzania wa kwanza kuwa na Yard ya Magari mwishoni mwa miaka ya 80 na yeye ni Wakili wa Kujitegemea wa Mahakama Kuu ya Tanzania
* Sitta kajieleza wasifu wake kwa ufupi na kuwahakikishia wajumbe kuwa hatapendelea upande wowote. Anataka kuwahakikishia watanzania kuwa wataona sababu ya wajumbe kupewa hata kiinua mgongo watakapomaliza zoezi hili. Kasema yeye kupewa kiti ni sawa na kumrudisha chura kwenye maji, ni wazi ataogelea tu!
*Zoezi la upigaji kura linaendelea
================================================================
UPDATES 2
MATOKEO
Jumla ya wabunge wote 629
waliopiga kura ni. 563
Kura zilizoharibika ni. 7
Hashim Rungwe. 69 (12.3%)
Sammuel Sitta. 487. (86.5%)
======================