one activist
Senior Member
- Oct 13, 2012
- 114
- 14
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Mwanza imetupilia mbali ombi la Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) iliyofungua kupinga maamuzi ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Mwanza, ya kuendelea kuwatambua Meya wa Manispaa ya Ilemela, Henry Matata pamoja na Diwani wa Igoma kuwa madiwani halali, licha ya kuvuliwa uanachama na kamati kuu ya chama hicho.
Katika kesi hiyo ambayo ilikuwa ikifuatiliwa kwa ukaribu na mamia ya wafuasi wa Chadema, Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, Aisheri Sumari, alisema baada ya kusikiliza pande zote imekubaliana na maamuzi ya Hakimu Mkazi kuendelea kuwatambua madiwani hao hadi kesi ya msingi iliyofunguliwa itakapoanza kusikilizwa.
Katika maamuzi yake, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mwanza alisitisha maamuzi ya Kamati Kuu ya Chadema kuwafukuza Diwani wa Kata ya Kitangiri, Henry Matata pamoja na Diwani wa Kata ya Igoma, Adamu Chagulani, hadi pale kesi ya msingi waliyofungua itakapokamilika, ambapo kwa wakati huo aliamuru Matata aruhusiwe kuwania kiti cha Meya wa Manispaa ya Ilemela.
Hata hivyo, baadhi ya madiwani wa Chadema, Josephat Manyerere pamoja na Dan Kahungu pamoja na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa chama hicho, Benson Kigaila, walidaiwa kukiuka maamuzi ya Mahakama kwa kumzuia Matata kuwania Umeya ambapo Matata alifungua kesi kuitaka Mahakama hiyo iwafunge jela wahusika hao, hata hivyo Mahakama ilitoa hukumu ya kwenda gerezani au kulipa faini kutokana na kukaidi maamuzi ya Mahakama.
Pia Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza ilisema kuwa katika ombi la pili la Chadema la kutaka Meya huyo wa Ilemela kuadhibiwa na Mahakama kwa kitendo chake cha kufungua kesi ya kupinga kuvuliwa uanachama katika mahakama ya Hakimu Mkazi na kisha mahakama kuu, maamuzi yake yatatolewa Agosti 12 mwaka huu.
Hata hivyo, alisema shauri la pili lililofunguliwa na Chadema kuitaka mahakama hiyo kumuadhibu Matata kwa kutumia vibaya chombo hicho cha kisheria litatolewa uamuzi Agosti 12, mwaka huu.
Katika shauri hilo la pili, Chadema kinaitaka mahakama kuu kumuadhibu Matata kwa kitendo chake cha kufungua kesi ya kupinga kuvuliwa uanachama katika Mahakama ya Hakimu Mkazi na kisha kufungua kesi hiyo hiyo katika Mahakama Kuu.
Katika shauri hilo, wakili wa Chadema, Method Kimomogoro alidai kuwa kitendo ni matumizi mabaya ya taratibu za mahakama hivyo anapaswa kuadhibiwa.
Wakili Kimomogoro alidai kwamba mara baada ya kuvuliwa uanachama na Kamati Kuu, Matata na Chagulani walifungua kesi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi kupinga uamuzi huo, kwa kutaka kuendelea kutambuliwa kama madiwani na kupewa haki zao zote.
Jaji Sumari alisema kuwa madai ya Matata kutumia vibaya chombo hicho cha kisheria yatatolewa uamuzi Agosti 12, mwaka huu, lakini kuhusu mahakama hiyo kuingilia uamuzi wa Chadema utabaki kama ulivyo.
Jaji Sumari alisema kwamba Chadema ni taasisi ya umma ambayo lengo lake kuu ni kuunda Serikali za Mitaa au Serikali Kuu, hivyo mahakama inayo mamlaka ya kuingilia kati maamuzi yake yoyote ili kuona kama hayajakiuka haki za wananchi au wanachama wake.
[h=4][/h]
Katika kesi hiyo ambayo ilikuwa ikifuatiliwa kwa ukaribu na mamia ya wafuasi wa Chadema, Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, Aisheri Sumari, alisema baada ya kusikiliza pande zote imekubaliana na maamuzi ya Hakimu Mkazi kuendelea kuwatambua madiwani hao hadi kesi ya msingi iliyofunguliwa itakapoanza kusikilizwa.
Katika maamuzi yake, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mwanza alisitisha maamuzi ya Kamati Kuu ya Chadema kuwafukuza Diwani wa Kata ya Kitangiri, Henry Matata pamoja na Diwani wa Kata ya Igoma, Adamu Chagulani, hadi pale kesi ya msingi waliyofungua itakapokamilika, ambapo kwa wakati huo aliamuru Matata aruhusiwe kuwania kiti cha Meya wa Manispaa ya Ilemela.
Hata hivyo, baadhi ya madiwani wa Chadema, Josephat Manyerere pamoja na Dan Kahungu pamoja na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa chama hicho, Benson Kigaila, walidaiwa kukiuka maamuzi ya Mahakama kwa kumzuia Matata kuwania Umeya ambapo Matata alifungua kesi kuitaka Mahakama hiyo iwafunge jela wahusika hao, hata hivyo Mahakama ilitoa hukumu ya kwenda gerezani au kulipa faini kutokana na kukaidi maamuzi ya Mahakama.
Pia Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza ilisema kuwa katika ombi la pili la Chadema la kutaka Meya huyo wa Ilemela kuadhibiwa na Mahakama kwa kitendo chake cha kufungua kesi ya kupinga kuvuliwa uanachama katika mahakama ya Hakimu Mkazi na kisha mahakama kuu, maamuzi yake yatatolewa Agosti 12 mwaka huu.
Hata hivyo, alisema shauri la pili lililofunguliwa na Chadema kuitaka mahakama hiyo kumuadhibu Matata kwa kutumia vibaya chombo hicho cha kisheria litatolewa uamuzi Agosti 12, mwaka huu.
Katika shauri hilo la pili, Chadema kinaitaka mahakama kuu kumuadhibu Matata kwa kitendo chake cha kufungua kesi ya kupinga kuvuliwa uanachama katika Mahakama ya Hakimu Mkazi na kisha kufungua kesi hiyo hiyo katika Mahakama Kuu.
Katika shauri hilo, wakili wa Chadema, Method Kimomogoro alidai kuwa kitendo ni matumizi mabaya ya taratibu za mahakama hivyo anapaswa kuadhibiwa.
Wakili Kimomogoro alidai kwamba mara baada ya kuvuliwa uanachama na Kamati Kuu, Matata na Chagulani walifungua kesi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi kupinga uamuzi huo, kwa kutaka kuendelea kutambuliwa kama madiwani na kupewa haki zao zote.
Jaji Sumari alisema kuwa madai ya Matata kutumia vibaya chombo hicho cha kisheria yatatolewa uamuzi Agosti 12, mwaka huu, lakini kuhusu mahakama hiyo kuingilia uamuzi wa Chadema utabaki kama ulivyo.
Jaji Sumari alisema kwamba Chadema ni taasisi ya umma ambayo lengo lake kuu ni kuunda Serikali za Mitaa au Serikali Kuu, hivyo mahakama inayo mamlaka ya kuingilia kati maamuzi yake yoyote ili kuona kama hayajakiuka haki za wananchi au wanachama wake.
[h=4][/h]